sir.JAPHET
JF-Expert Member
- May 18, 2012
- 699
- 133
Na John Makambo, Tabora JESHI la Polisi mkoani Tabora, linamshikilia mkazi wa Kijiji cha Ilolangulu, Kata ya Ilolangulu Wilaya ya Uyui mkoani Tabora, kwa tuhuma za kukutwa na mabomu manne ya kutupa kwa mkono.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tabora, ACP Antony Rutta, alieleza kuwa, kulingana na taarifa zilizolifikia jeshi hilo, mabomu hayo yalikuwa yatumike kwa ajili ya kufanya shambulio ama utekaji katika mnada.
Alimtaja anayeshikiliwa kwa tuhuma hizo ni Nsimbi Masaki, ambaye alikuwa ameyahifadhi mabomu hayo katika mfuko wa sandarusi na kuyafunga pia kwa kutumia mfuko wa Rambo na kisha kuyachimbia chini.
Alisema taarifa za kiintelijensia zinabainisha kuwa, mabomu hayo yanaweza kuwa yameingia nchini kupitia nchi jirani, ambayo hakuweza kuitaja.
Alisema, jeshi hilo linaendelea kuchunguza jinsi mabomu hayo yanavyoweza kuingia nchini na kwamba mtuhumiwa huyo anatarajia kufikishwa mahakamani mara baada ya mahojiano kukamilika.
Wakati huo huo jeshi hilo linamshikilia mtuhumiwa mmoja kutokana na tuhuma za kukutwa na silaha ya gobole, ambalo linauwezo wa kutumia risasi za bunduki ya Shortgun.
Kamanda Rutta alisema kuwa, katika tukio jingine watu 8 wanashikiliwa na Polisi kwa tuhuma za kukutwa na mali zinazodhaniwa ni za wizi.
Mali hizo ni pamoja na seti moja ya tv, radio na mapanga ambayo wanadhaniwa kuyatumia kwa ajili ya kupora ama katika matukio ya ujambazi.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tabora, ACP Antony Rutta, alieleza kuwa, kulingana na taarifa zilizolifikia jeshi hilo, mabomu hayo yalikuwa yatumike kwa ajili ya kufanya shambulio ama utekaji katika mnada.
Alimtaja anayeshikiliwa kwa tuhuma hizo ni Nsimbi Masaki, ambaye alikuwa ameyahifadhi mabomu hayo katika mfuko wa sandarusi na kuyafunga pia kwa kutumia mfuko wa Rambo na kisha kuyachimbia chini.
Alisema taarifa za kiintelijensia zinabainisha kuwa, mabomu hayo yanaweza kuwa yameingia nchini kupitia nchi jirani, ambayo hakuweza kuitaja.
Alisema, jeshi hilo linaendelea kuchunguza jinsi mabomu hayo yanavyoweza kuingia nchini na kwamba mtuhumiwa huyo anatarajia kufikishwa mahakamani mara baada ya mahojiano kukamilika.
Wakati huo huo jeshi hilo linamshikilia mtuhumiwa mmoja kutokana na tuhuma za kukutwa na silaha ya gobole, ambalo linauwezo wa kutumia risasi za bunduki ya Shortgun.
Kamanda Rutta alisema kuwa, katika tukio jingine watu 8 wanashikiliwa na Polisi kwa tuhuma za kukutwa na mali zinazodhaniwa ni za wizi.
Mali hizo ni pamoja na seti moja ya tv, radio na mapanga ambayo wanadhaniwa kuyatumia kwa ajili ya kupora ama katika matukio ya ujambazi.