MTANZANIA
Askofu msaidizi wa Jimbo Katoliki la Bukoba, Methodius Kilaini, amesifu hatua ya aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Bukoba, Albert Mnali, a kuwachapa viboko walimuu wa shule za msingi za Katerero na Kanazi kutokana na kushindwa kutekeleza vizuri wajibu wao.
Pongezi hizo alizitoa jana mjini hapa, wakati akijibu hoja mbalimbali zilizotolewa na wadau wa maendeleo wakati wa kongamano la kutathmini mustakabali wa maendeleo ya Kagera kwa kipindi cha miaka 50 ya uhuru wa Tanganyika.
"Huyu mkuu wa Wilaya alikuwa na sababu zote za kuwachapa viboko walimu wazembena walioonekana kutotekeleza wajibu wao wa kazi vizuri, watendaji na viongozi wa serikali wasipotimiza vizuri wajibu wa kazi ndio wanaochangia ongezeko a umaskini katika Mkoa wa Kagera", alisema askofo Kilaini.
Alisema ni aibu kwa Mkoa wa Kagera kuwa miongozi mwa mikoa maskni wakati unazo rasilimali nyingi.
Alisema baadhi ya watumishi na viongozi wa serikali hawawajibiki ipaswavyo na badala yake wanaendekeza masuala ya ukiritimba wanapokuwa ofisini.
"Inashangaza kuona baadhi ya watumishi na viongozi wa Serikali wanaochangia kwa kuwawekea vikwazo wanaendelea kufanya kazi Mkoa wa Kagera", alsiema Askofu Kilaini.
Alisema uwajibikaji usiofaa na ukiritimba unaoendekezwa na baadhi ya viongozi na watumishi wa serikali ndio unaorudisha nyuma maendeleoa ya Kagera.
Alisema baadhi ya watumishi na viongozi wa serikali wanafanya kazi kwa utashi wao na wengine wanawawekea vikwazo.
Naye mkuu wa Mkoa wa Kagera, Kanali mstafu, Fabian Masawe, alisema kamwe hatakubali kufanya kazi na watendaji wazembe.
Askofu msaidizi wa Jimbo Katoliki la Bukoba, Methodius Kilaini, amesifu hatua ya aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Bukoba, Albert Mnali, a kuwachapa viboko walimuu wa shule za msingi za Katerero na Kanazi kutokana na kushindwa kutekeleza vizuri wajibu wao.
Pongezi hizo alizitoa jana mjini hapa, wakati akijibu hoja mbalimbali zilizotolewa na wadau wa maendeleo wakati wa kongamano la kutathmini mustakabali wa maendeleo ya Kagera kwa kipindi cha miaka 50 ya uhuru wa Tanganyika.
"Huyu mkuu wa Wilaya alikuwa na sababu zote za kuwachapa viboko walimu wazembena walioonekana kutotekeleza wajibu wao wa kazi vizuri, watendaji na viongozi wa serikali wasipotimiza vizuri wajibu wa kazi ndio wanaochangia ongezeko a umaskini katika Mkoa wa Kagera", alisema askofo Kilaini.
Alisema ni aibu kwa Mkoa wa Kagera kuwa miongozi mwa mikoa maskni wakati unazo rasilimali nyingi.
Alisema baadhi ya watumishi na viongozi wa serikali hawawajibiki ipaswavyo na badala yake wanaendekeza masuala ya ukiritimba wanapokuwa ofisini.
"Inashangaza kuona baadhi ya watumishi na viongozi wa Serikali wanaochangia kwa kuwawekea vikwazo wanaendelea kufanya kazi Mkoa wa Kagera", alsiema Askofu Kilaini.
Alisema uwajibikaji usiofaa na ukiritimba unaoendekezwa na baadhi ya viongozi na watumishi wa serikali ndio unaorudisha nyuma maendeleoa ya Kagera.
Alisema baadhi ya watumishi na viongozi wa serikali wanafanya kazi kwa utashi wao na wengine wanawawekea vikwazo.
Naye mkuu wa Mkoa wa Kagera, Kanali mstafu, Fabian Masawe, alisema kamwe hatakubali kufanya kazi na watendaji wazembe.