Akina Mama mna maoni gani kuhusu mila za 'Chagulaga'?

So far, inaonekana hakuna anaejua.

Akaja Sikonge, anatueleza ngoma za Wasukuma, tena za enzi hizo. Wakati tunataka kujua kinachoendelea sasa hivi Uyui, Tabora, ambacho local leaders wanasema kinasababisha huku kujamiana jamiana ovyo. Sikonge alichoeleza ni kama ndoa za hiari hiari hivi, hatuelezwi hizo ngono ya ovyo ovyo zinavyotokea. Anasema “hiyo ilikuwa ni OLD school. Unaweza kukuta siku hizi hawa New Generation wanamalizana na mtoto hapo hapo.” Kwa hiyo nae hajui.

Kuhani, yaani ukisoma maelezo yangu unaona kuwa SIJUI KITU? Duu mu wee una kipaji cha kubisha ili tu UBISHE. Naona hata nikuelezee na kukupa VIDEO, bado utasema kuwa hiyo ni sehemu moja tu na kuwa sikuona Tabora nzima.
Kama uliuliza kwa dhati basi angalia maelezo ya Bubu kutakakusema ya mwanzo. Ile habari imechanganywa na mwandishi wa habari hata hakufanya kazi ya ziada kuuliza na kupata ukweli halisi. Nilivyokuwa mdogo na mimi nilisikia hivyo hivyo. Nafikiri Wasukuma huwa hawataki kusema kinachofanyika huko. Sijui kama ni mwiko au lahh. Siku moja tuliamua kuwafuata ili tuangalia Porno la bure. Tulikaa hadi mtu wa mwisho akaondoka na mabinti almost yuko kwao na hakuna kilichofanyika. Ilikuwa chagulaga moja baada ya nyingine. Tukarudia mara ya pili story ni zile zile. Tukajua hii ilikuwa HABARI feki na hatukuenda tena kuangalia wanavyo chaguana.
Simtetei Kikwete. Ila kwa hili naona yuko sawa. Kama nilivyosema ni kuwa HAMNA NGOMA YA CHAGULAGA. Ila ipo ngoma ya PUVA. hata bubu kasema hilo. Hamna ya vijana kusimama na kuchagua ila humkimbiza msichana na wakimkamata humzunguka kundi na mmoja kuchaguliwa. Akichaguliwa, wengine bado husubiri na wao wapewa nafasi yao.
Inavyoonekana wanaopata Mimba wengi wao ni wanafunzi wa Secondary. Kama ni hivyo, mtu hapa anataka KUKIMBIA MAJUKUMU. Kama watoto wako Secondary, na wanapata Mimba, watia mimba ni waalimu, mi-Sugardaddy, vijana wenye senti zao, wanafunzi wenzao nk. Nafikiri muda wa kwenda ngomani unakuwa umepungua. Somo inabidi lianzishwe Secondary ili kuzuia hivi vitendo. Mliona kwenye Disco la watoto Tabora, hadi watoto wanauziwa Pombe. Na kama si janga hilo hakuna hata mmoja leo angelisema. Mkoa wa tabora kuna Uzembe wa aina nyingi sana. Viongozi wanatafuta sababu za KIJINGA ili kupeleka lawama sehemu nyingine. Kwa nini wasiseme POMBE pia zinasababisha? Disco pia linasababisha? Au na wao wana hisa huko?
Kuhani, kama una akili kweli (nafikir unazo) owanisha matukio hayo na ukumbuke kuwa Tabora ni mkoa masikini sana. Sasa ukichanganya vyote vitatu utaona kama kweli CHAGULAGA ndiyo mleta mimba.
 
Huyo DC na yule DC wa Nzega Betty wote ni wachaga na wanapiga vita chagulaga sana eti inasababisha kuongezeka kwa maambukizi ya VVU wakati si kweli, kama unajua mila za kisukuma na procedure za chagulaga huna budi kukubaliana na kuiendeleza mila hiyo ila tu kwa washenzi wasio na mila maana sie wengine wazazi wetu walikutana kwenye chagulaga, wakaoana, na sie tukazaliwa baada ya ndoa halali za kimila. Ni upuuzi leo useme ngoma au chagulaga inaleta maambukizi na kupiga marufuku huku ukiacha madisco mjini yanaendelea, cha muhimu ni elimu ya kuzuia maambukizi itolewe kwa watu wote Wasukuma, Wahaya, Wangoni, na hata Wachaga waliozoea kuitisha madisco na mbege kidogo halafu......
 
Jamani wachaga wananyimbo nyingi tu na wala sio kama hawana mila zao. Nyimbo maja ambayo nakumbuka sana ilikuwa ya nguvu kazi. ...Thomasi kawambalewayo ire kawamba lumkape matuta iyo matuta mali ya serekali miyo oooh yale ileleleileile mangiyo.

Kweli bana, tena ni wimbo maarufu wa harusi, tehe tehe tehe!
 
Kuhani, yaani ukisoma maelezo yangu unaona kuwa SIJUI KITU? Duu mu wee una kipaji cha kubisha ili tu UBISHE. Naona hata nikuelezee na kukupa VIDEO, bado utasema kuwa hiyo ni sehemu moja tu na kuwa sikuona Tabora nzima.
Kama uliuliza kwa dhati basi angalia maelezo ya Bubu kutakakusema ya mwanzo. Ile habari imechanganywa na mwandishi wa habari hata hakufanya kazi ya ziada kuuliza na kupata ukweli halisi. Nilivyokuwa mdogo na mimi nilisikia hivyo hivyo. Nafikiri Wasukuma huwa hawataki kusema kinachofanyika huko. Sijui kama ni mwiko au lahh. Siku moja tuliamua kuwafuata ili tuangalia Porno la bure. Tulikaa hadi mtu wa mwisho akaondoka na mabinti almost yuko kwao na hakuna kilichofanyika. Ilikuwa chagulaga moja baada ya nyingine. Tukarudia mara ya pili story ni zile zile. Tukajua hii ilikuwa HABARI feki na hatukuenda tena kuangalia wanavyo chaguana.
Simtetei Kikwete. Ila kwa hili naona yuko sawa. Kama nilivyosema ni kuwa HAMNA NGOMA YA CHAGULAGA. Ila ipo ngoma ya PUVA. hata bubu kasema hilo. Hamna ya vijana kusimama na kuchagua ila humkimbiza msichana na wakimkamata humzunguka kundi na mmoja kuchaguliwa. Akichaguliwa, wengine bado husubiri na wao wapewa nafasi yao.
Inavyoonekana wanaopata Mimba wengi wao ni wanafunzi wa Secondary. Kama ni hivyo, mtu hapa anataka KUKIMBIA MAJUKUMU. Kama watoto wako Secondary, na wanapata Mimba, watia mimba ni waalimu, mi-Sugardaddy, vijana wenye senti zao, wanafunzi wenzao nk. Nafikiri muda wa kwenda ngomani unakuwa umepungua. Somo inabidi lianzishwe Secondary ili kuzuia hivi vitendo. Mliona kwenye Disco la watoto Tabora, hadi watoto wanauziwa Pombe. Na kama si janga hilo hakuna hata mmoja leo angelisema. Mkoa wa tabora kuna Uzembe wa aina nyingi sana. Viongozi wanatafuta sababu za KIJINGA ili kupeleka lawama sehemu nyingine. Kwa nini wasiseme POMBE pia zinasababisha? Disco pia linasababisha? Au na wao wana hisa huko?
Kuhani, kama una akili kweli (nafikir unazo) owanisha matukio hayo na ukumbuke kuwa Tabora ni mkoa masikini sana. Sasa ukichanganya vyote vitatu utaona kama kweli CHAGULAGA ndiyo mleta mimba.


Ngosha hii ni shule tosha. Mimi ni wa huko huko sina la kuongezea.

Labda niandike kitu hapa....kitu cha mkulima hakina thamani..maana kinaonekana ni cha kishenzi. Uncivilized! Hivi mbona hakuna anayesema madisco ya mjini yanachochea VVU? kwa sababu madisco yanaendeshwa na wasomi!. I tell you..lazima tufike point tukubali..ni kweli kuna mila potofu lakini si zote. Zile nzuri tuziendeleze na tuwafunze wanetu. Jamani siyo vizuri kila kitu kukiangalia katika mtizamo hasi.

Katika hili namuunga mkono ndugu Jakaya. Mjini watu wanafanya whatever they want...lakini inakuwa justified kwa sababu wanaofanya ni wasomi. Why? Ulishasikia Usukumani watu wanakufa kwa njaa? bwana we are very hard working people. Ngoma ni one of our opportunity to have fun!

No tufike point tukubali kwamba mila zetu katika dunia ya leo zinaweza kuwa zinapwaya, lakini si vema kuzitelekeza kwa minajili ya usomi na globalization.
 
...mbaya zaidi ana kauli mbiu kuwa Tanzania bila UKIMWI inawezekana, itawezekana wapi iwapo 'Chagulaga' anaitafsiri kama mwendo mdundo?

Ndio, mdharau mila na desturi za kwao ni sawa na mtumwa, lakini Elimu ni bahari, katika Chagulaga ya miaka hii kuna kila kilicho kinyume na maadili ya haki za binadamu, haki za mtoto wa kike/mwanamke kuchagua, kusoma na kujiendeleza, na kujikinga na ngono zembe inayoweza sababisha mimba na hata magonjwa ya zinaa.

Ndivyo tulivyo, lakini tunaweza kubadilika, TUKITAKA!

Ana contradictions zake nyingi tu zinazosababishwa na kukurupuka kuzungumza bila kulitafakari jambo kwa kina. Leo unasema Tanzania bila ukimwi inawezekana, kesho unatetea 'Chagulaga' ambayo kwa namna moja au nyingine inawezekana kabisa ikawa inachangia kuongeza ukimwi. Mwe! :(
 
...ama kweli, 'chagulaga' ni moja ya mila potofu inayofaa kupingwa kwa nguvu zote kwani haina tofauti na kuhalalisha ubakaji, duh :( !!!
Ni kweli Mchongoma, na sidhani kama kuna hiari hapa mtu amekuchagulaga itakuwa imetoka wana hata muda kusema angalau wakaangalie afya zao kweli?? au ndio mbele kwa mbele??!! Ni noma kabisa....
 
Ni kweli Mchongoma, na sidhani kama kuna hiari hapa mtu amekuchagulaga itakuwa imetoka wana hata muda kusema angalau wakaangalie afya zao kweli?? au ndio mbele kwa mbele??!! Ni noma kabisa....

Ndiyo kuna hiari maana mwanamke ndo anaechagua kati ya wanaume waliopo!
kuhusu afya ni kwenda kuangalia tu kabla hawajakutana kimwili!
 
Back
Top Bottom