Akilia sana, karibu kutunguliwa...!

Ndege aliye mtini, hawezi kamwe kulia,
Labda aliye shimoni, hewa imempelea.
Hivi ni sababu gani, machozi hawezi toa?
Ndege aliye mtini, kamwe hawezi kulia.

we babu we kiboko kila fani umo? nimekuvulia kofia, bora wewe sasa teamo ndio sikudhani kabisaaaaa kumbe watu wana vipaji humu lol
 
Wakiiji zangu salamu,nikushukuru kwa hili
Nami nishike yangu kalamu, niseme moja mawili
Umesema yalo adimu, yenye mwanga kandili
Milio mingine feki, usivutike sauti

Kuna videge vizushi,kama kunguru mwangapwani
Vyashika wako utashi, Kwa milio vikighani
Sauti zao chekeshi,weza hisi umewini
Mioyo yao beleshi,utachotwa masikini.

Kuna vingine vidogo, vyafanana na shomoro
Vyapatikana ugogo, sauti zao si kero
Ila vipe tu kisogo, vyatunguliwa kwa jero
Hivi angalau kidogo, Anajua kaka Melo


Na kuna makorobindo, ya zamani sio leo
Sauti zao kishindo, yamekwepa makombeo
Manati kwao msondo, labda uje na komeo
Niliyaona Kibondo, kwa kaka Batolomeo


Duh! Kuna vichokoriko,Hivi kula kwangu mwiko
Vinalia dikodiko, Lakini,mmh! mevipiga kiwiko
Tatizo lao chereko,shebedua na vicheko
Hawa kwangu mwiko!

Kuna ndege sisubiri, alie wala acheke
Mhozo-habeshi nikiri, huyu hana makeke
Kazidi makhirikhiri,machejo na pozi zake.
Huyu mtini simtungui, Nampandia namchukua!!

Naomba MMM, Teamo, Asprin na AmanGK muwe mnakuja namna hii kila inapowezekana maana wanasema ukicheka waongeza siku. Ilikuwa full kucheka

You guys are GREAT!!!
 
Wazushi waniwangia, ndege kunifukuzia,
Hakika nawaambia, wangu namng'ang'ania,
Kamwe hawatopatia, watabaki angalia,
Ndege amekwishalia, mwajua kitofatia!
Kutunguliwa.

MMM
 
huku kwetu uswahilini, hata ndege hakuna
tumezungukwa na nyani, na ngedere wengi sana
tena tupo hatarini , kifo lini? tunaulizana
ndege alie mtini , ni ndoto kwetu kuona.

udenda umenitoka, kusoma hili shairi
ndege wa kusadikika, moyoni ameshamiri
mengi nimelazimika, akilini kufikiri
lini mimi nitamshika, nipate nijivinjari.

mnasema analia, natamani lake chozi
wengine wamebishia, kulia katu hawezi
vyovyote itavyokuaa, kuvumilia siwezi
kuhama nimeamua, naenda hamia mbezi
ndege nipate tungua, kwa manjonjo na mapozi.




ni mimi malenga wenu klorokwini a.k.a mshamba mstaarabu
 
Kumtungua hutomfaidi, kibudu si fanani
Polepole mnyatie, Koo usimkabe
Poke kwa staha
Polepole mnyakue, ndani kwako muweke
Potepote Kwa makini mchunguze, afaa kuliwa?
Ni popo masikini si ndege si mnyama
Si wa kufuga, si wa kitoweo, ni dege lisiloliwa!!!!!
 
Watani habari gani, nawasalimu jamani,
Kumi na moja i ndani, nakuja na hizi ghani,
Limenijia kichwani, wazo hili si utani,
Ndege akilia sana, karibu kutunguliwa!
Akijelengesha tungua!

Nimemuona mtini, ndege kweli chakarani,
Ana mbwembwe kama nini, na rangirangi mbawani,
Sijui ni wa Kingoni, Anaimba kama nini,
Ndege akilia sana, karibu kutunguliwa!
Akijilengesha, chukua

Kafumba macho tawini, na kawimbo mdomoni,
Ndege wenzake mtini, wamenyamaza kwa soni,
Anabadilisha tyuni, kama kasomea fani,
Ndege akilia sana, karibu kutunguliwa!
Akijilengesha pasua

Mwindaji akaja chini, na manati mkononi,
Kaangalia mtini, achague ndege gani,
Mwenye kelele mtini, akamlenga jamani,
Ndege akilia sana, karibu kutunguliwa!
Akijilengesha, kamua

Mara Puh! Ndege chini, wenzake wako angani!
Kisu kikambusu shingoni, kisiwe kibudu jamani,
Kanyonyolewa majini, akatundikwa motoni,
Ndege akilia sana, karibu kutunguliwa!
Akijilengesha nyanyua!

Ndipo nikaja amini, chunguza kwanza mtini,
Yule anojiamini, huimba sana tawini,
Ni kitoweo mtani, cha maakuli jioni,
Ndege akilia sana, karibu kutunguliwa!
Akijilengesha tumbua!

Na. M. M. Mwanakijiji (BGM) – Sauti ya Kijiji

Naona hili shairi wapewe TBC liimbwe kabla ya taarifa ya habari safi sana Mzee Mwanakijiji.
 
Wazushi waniwangia, ndege kunifukuzia,
Hakika nawaambia, wangu namng'ang'ania,
Kamwe hawatopatia, watabaki angalia,
Ndege amekwishalia, mwajua kitofatia!
Kutunguliwa.

MMM

Hapa hakuna mzushi, ukweli twakuambia,
Tatizo lako mbishi, jambo ukilishikia,
Domo unafuka moshi, hoja kiishikilia,
Achana wako ubishi, ndege halii aimba.
 
huku kwetu uswahilini, hata ndege hakuna
tumezungukwa na nyani, na ngedere wengi sana
tena tupo hatarini , kifo lini? tunaulizana
ndege alie mtini , ni ndoto kwetu kuona.

udenda umenitoka, kusoma hili shairi
ndege wa kusadikika, moyoni ameshamiri
mengi nimelazimika, akilini kufikiri
lini mimi nitamshika, nipate nijivinjari.

mnasema analia, natamani lake chozi
wengine wamebishia, kulia katu hawezi
vyovyote itavyokuaa, kuvumilia siwezi
kuhama nimeamua, naenda hamia mbezi
ndege nipate tungua, kwa manjonjo na mapozi.




ni mimi malenga wenu klorokwini a.k.a mshamba mstaarabu

Ewe kidonge mwenzangu, kumbe nawe uko ndani,
Napata kizunguzungu, umenigusa moyoni,
Ndege wa kwenu kimbungu, leo wamkataani?
Ndege huyu ndege wetu, kila shemu huishi

Labda kama baharini, kusipokuwa na miti,
Huko hakuwezekani, asijepata mititi,
Hamia kwetu nyumbani, nitakupatia hati,
Nitakupatia hati, ndege umuweke ndani.
 
Ewe kidonge mwenzangu, kumbe nawe uko ndani,
Napata kizunguzungu, umenigusa moyoni,
Ndege wa kwenu kimbungu, leo wamkataani?
Ndege huyu ndege wetu, kila shemu huishi

Labda kama baharini, kusipokuwa na miti,
Huko hakuwezekani, asijepata mititi,
Hamia kwetu nyumbani, nitakupatia hati,
Nitakupatia hati, ndege umuweke ndani.

pia mimi sikudhani, uwanja huu ni wako
na sasa nimeamini, hii pia fani yako
aspirini, klorokwini, hii dozi ni kiboko
mwanakijiji haamini, tunavyotoa milipuko.

huyo ndege unaesema, tayari nimemuona,
mwili umenitetema , leo nimeita jana
kumpata ni lazima , iwe usiku au mchana
nitamla mzima mzima, tena kwa kumtafuna.

naipanga mikakati, na mitego ya kileo
naitengeza manati, gobole pia koleo
nitamtungulia kati, apapatike na kilio
nikamle kwa chapati, nimfanye kitoweo
 
Watani habari gani, nawasalimu jamani,
Kumi na moja i ndani, nakuja na hizi ghani,
Limenijia kichwani, wazo hili si utani,
Ndege akilia sana, karibu kutunguliwa!
Akijelengesha tungua!

Nimemuona mtini, ndege kweli chakarani,
Ana mbwembwe kama nini, na rangirangi mbawani,
Sijui ni wa Kingoni, Anaimba kama nini,
Ndege akilia sana, karibu kutunguliwa!
Akijilengesha, chukua

Kafumba macho tawini, na kawimbo mdomoni,
Ndege wenzake mtini, wamenyamaza kwa soni,
Anabadilisha tyuni, kama kasomea fani,
Ndege akilia sana, karibu kutunguliwa!
Akijilengesha pasua

Mwindaji akaja chini, na manati mkononi,
Kaangalia mtini, achague ndege gani,
Mwenye kelele mtini, akamlenga jamani,
Ndege akilia sana, karibu kutunguliwa!
Akijilengesha, kamua

Mara Puh! Ndege chini, wenzake wako angani!
Kisu kikambusu shingoni, kisiwe kibudu jamani,
Kanyonyolewa majini, akatundikwa motoni,
Ndege akilia sana, karibu kutunguliwa!
Akijilengesha nyanyua!

Ndipo nikaja amini, chunguza kwanza mtini,
Yule anojiamini, huimba sana tawini,
Ni kitoweo mtani, cha maakuli jioni,
Ndege akilia sana, karibu kutunguliwa!
Akijilengesha tumbua!

Na. M. M. Mwanakijiji (BGM) – Sauti ya Kijiji

Siko kifani zaidi,ni hoja kuhusu ndege,
Ninayo yangu miadi,kama alivyo moringe,
Wengi wao makuwadi,kutaka wote waige,
Kama hoja ni ya ndege, mie nachagua bata,

Bata ndo namchagua, ndiyo wangu modeli,
Bila ya kuchakachua,kwa utulivu ni kweli,
Pakata ukidadua, pachika kwa baisikeli,
Kama hoja ni ndege, mie nachagua bata,

Mandege yako mengi, bundi njiwa kunguru,
Sijui wewe kitegi, ulimpata maguru,
Tumia hata ulegi,usije pata udhuru,
Kama hoja ni ndege,mie nachagua bata,

Utatungua wangapi,katika miti mingapi,
Usije pata makapi,kwa kuzani ni kopi,
Hoja yako ndio ipi,nipe nikupe tipi,
Kama hoja ni ndege, mie nachagua bata,

Pakata kwa raha zako, baada ya kumuoka,
Manati kitu ni chako,ya nini kukukuruka,
Huitaji mulengo wako,usije pata sumbuka,
Kama hoja ni ndege,mie nachagua bata,

Ni wewe mwanakijiji,ulezoea porini,
Kwetu yapo majiji, hewala i kibindoni,
Nenda mpaka ujiji,bata mpaka sebureni,
Kama hoja ni ndege,mie nachagua bata,

Ngoja niweke koma,bata wangu nimpakate,
Asije pata ukoma,kisha nimpe mate,
Nisije mwaga tama,kuku waule wote,
Kama hoja ni ndege,mie nachagua bata,
 
Nilikuwa ninawaza, kalamu nisiishike,
Nikae kwenye baraza, moja mbili nisishike,
Maguluma kanikwaza, ngoja mic niishike
Bata anapakatwaje, nawauliza malenga?

Ndio hapa mnambie, kwa nini wampakata?
Tena nidadavulie, ni raha gani wapata?
Ili nami nikimbie, nimsake huyo bata,
Nawauliza malenga, bata anapakatwaje?

Hommie wangu 'Sipirini, hata nawe Klorokwini,
Mwanakijiji Amani, Magulumangu mwiteni,
Aje hapa barazani, aujibu mtihani,
Bata anapakatwaje, nawauliza malenga?

'Mesikia nimeona, bata yake kuharisha,
Wala sio kunong'ona, hilo usije kubisha
Kumpakata mi naona, hilo jambo la kutisha,
Bata anapakatwaje, nawauliza malenga?

Domo lake lachokoa, vinyesi na konokono,
Alacho ndio atoa, kwani nimpe mkono?
Usije kunizodoa, haya yangu ni maono,
Bata anapakatwaje, nawauliza malenga?

Na Kaizer K. Kaizer (Sauti ya watu)
 
Nilikuwa ninawaza, kalamu nisiishike,
Nikae kwenye baraza, moja mbili nisishike,
Maguluma kanikwaza, ngoja mic niishike
Bata anapakatwaje, nawauliza malenga?

Ndio hapa mnambie, kwa nini wampakata?
Tena nidadavulie, ni raha gani wapata?
Ili nami nikimbie, nimsake huyo bata,
Nawauliza malenga, bata anapakatwaje?

Hommie wangu 'Sipirini, hata nawe Klorokwini,
Mwanakijiji Amani, Magulumangu mwiteni,
Aje hapa barazani, aujibu mtihani,
Bata anapakatwaje, nawauliza malenga?

'Mesikia nimeona, bata yake kuharisha,
Wala sio kunong'ona, hilo usije kubisha
Kumpakata mi naona, hilo jambo la kutisha,
Bata anapakatwaje, nawauliza malenga?

Domo lake lachokoa, vinyesi na konokono,
Alacho ndio atoa, kwani nimpe mkono?
Usije kunizodoa, haya yangu ni maono,
Bata anapakatwaje, nawauliza malenga?

Na Kaizer K. Kaizer (Sauti ya watu)

Pope at his best,,kumbe ndo maana ulikuwa huji mlimani!

 

Similar Discussions

Back
Top Bottom