Eiyer
JF-Expert Member
- Apr 17, 2011
- 28,258
- 20,709
Jamani,mimi naamini kujifunza hakukuishia darasani,na sipendi kufanya mambo kimazoea.Kuna hii kitu nimekua nikisikia tangu mdogo,AKILI.Je ni nini?Je ni ufahamu?Inapimwaje?Shule kwa mfano,yule anaefaulu masomo huonekana ana "akili" lakini ukija mtaani unamkuta ni mlevi,mnyanyasaji,mkatili,mpenda fujo n.k,je huyu kweli ana akili?Au ubongo ni akili?Nijuavyo mimi ubongo ni kifaa anachotumia mtu kufikiri.Sasa akili iko wapi?Inakaa mwilini?Je ni eneo lipi inakaa?Au ufahamu ndio akili,Kama ni ndio ufaham ni akili?Hebu fungukeni mtusaidie sisi wenye kutanzwa na hii kitu!