ngoshwe
JF-Expert Member
- Mar 31, 2009
- 4,131
- 925
Mara nyingi viongozi wetu wamekuwa wanafiki. Katika mambo ambayo yanaendelea kumpatia sifa kimataifa Mhe. B.W. Mkapa (Rais Mtaafu wa Tanzania) ni upeo wake wa kufahamu,kuchambua na kuweka sawa masuala mengi ya kijamii, kiuchumi na kisiasa.
Mkapa bado anatambulika katika safu za Viongozi wa Taifa letu na amekuwa akionekana kuwa mpigania haki mzuri sana kwa mataifa mengine ikiwemo kuhusika katika upatanishi wa jirani zetu wa Kenya katika mgogoro uliotokana na uchaguzi wao Mkuu wa mwaka 2007.
Mkapa anajua sana matatizo ya nchi yake ikiwemo yale ya Kikatiba pia na angeweza kusaidia kushauri kupatiwa ufumbuzi kama alivyokuwa Baba wa Taifa. Lakini cha kusikitisha yupo kimya sana hapa nyumbani na anaonekana akiongelea hukooo "nyumba za jirani" mambo ambayo kwa busara zake angeweza kabisa kuwasaidia wanasiasa wetu ndani ya chama chake kupata akili za "mbayuwayu" na kulewezesha Taifa letu likwamuke katika wimbi la matatizo ya kijamii, kiuchumi na kisiasa...
Nini Busara za vingozi kama hawa??wanasubiri mpaka wafe ndo waje kuandikwa vizuri zaidi na kuenziwa??.
Mkapa bado anatambulika katika safu za Viongozi wa Taifa letu na amekuwa akionekana kuwa mpigania haki mzuri sana kwa mataifa mengine ikiwemo kuhusika katika upatanishi wa jirani zetu wa Kenya katika mgogoro uliotokana na uchaguzi wao Mkuu wa mwaka 2007.
Mkapa anajua sana matatizo ya nchi yake ikiwemo yale ya Kikatiba pia na angeweza kusaidia kushauri kupatiwa ufumbuzi kama alivyokuwa Baba wa Taifa. Lakini cha kusikitisha yupo kimya sana hapa nyumbani na anaonekana akiongelea hukooo "nyumba za jirani" mambo ambayo kwa busara zake angeweza kabisa kuwasaidia wanasiasa wetu ndani ya chama chake kupata akili za "mbayuwayu" na kulewezesha Taifa letu likwamuke katika wimbi la matatizo ya kijamii, kiuchumi na kisiasa...
Nini Busara za vingozi kama hawa??wanasubiri mpaka wafe ndo waje kuandikwa vizuri zaidi na kuenziwa??.
Last edited by a moderator: