Ajira ni utumwa??

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,720
21,779
wapo wengi wanaojiuliza kwa nini nilifanyakazi miaka 30,najua hiyo ndio ilioandikwa kwako
leo naomba tuongee ukweli ajira ni laana na mtu anaetegemea mshara amelaaniwa.....
Kama uamini uliza wazee waliofanya kazi miaka 30 to 40 walizoea kuamshwa asbh saa 12
na kurudi majumban mwao usiku bila kukaa familia leo wanamka saa nne asbh sio kwamba wanataka
walifumbwa ufahamu ama wengine kusema walilaaniwa...IDADI kubwa leo wanaangaika wanateseka
na kutaabika wengine wanapigwa na askari (wajukuu zao)) hii ni laana

sisemi ni mbaya kufanya kazi ila ukweli ubaki ni wakati wa wewe ulie kwenye ajira kuanza kujipanga na kuangalia
baada ya miaka kdhaa unataka kuwa nani....ngoja nikwambie sisemi umelaaniwa ila ukweli unabaki ajira
ni zaidi ya laaana wapo wengi wamekuwa wanaridhika na mishara walionayo lakini waulize walipoondoka
waliondoka na nini???nikiwa sehemu moja ya kazi niliwahi kupambana sana sana na mshahara kuongezwa ingawa mwisho
walituondoa lakini Mungu alisimama na uhalali wetu na mwisho walioondoka walitukumbuka kwa nini tulingangana na kuongezwa
mishahara huku tukiomba allowance azina msaada sana kwenye kazi ulio nayo ,,
Nasema hivi kumaanisha sipendi uje kutesa familia yako kama yule ama huyu ,huu ni wakati wako kuanza
kufikiria ukiondoka kazini leo utakuwa wapi???wapo wengi wamekuwa kama misukule ya kazi wanapopata
kazi leo wanajua watakufa milele wakiwa wanafanya kazi..la hasha wakati wa kujua kesho nataka kuishi maisha
gani

Wapo wanaoamini wakitoka kazini ndio wataweza kununua gari.kujenga wewe wewe mpendwa uko kazini miaka 30
umeshindwa kununua gari ukanunue unaondoka si tutakupeleka pale sakatriki kabla ya muda wako

Sisemi kwa ubaya naomba mnielewe napenda kukujuza wewe ulie kwenye ajira uanze sasa kujitayarisha baada ya
kustaafu unataka kusihi maisha gani,wapo waliosubiri kujenga na fedha za kustaafu anza sasa jiulize je mshara ulionao
ukiondoka angalia na bei za vitu maduka ya ujenzi je utaweza kuhimili kujenga.kwa nini ukiwa kazini uasitafute kiambatanisha
cha biashara kitachakupa kuweza kununua vitu kama hivi ukiwa kazini ,,wachache wanaoweza kujenga na kumaliza nyumba
maramoja kama ra!!usijiumize kichwa anza sasa weka kibubu uanze kuweka hela nakwambia unanunua kiwanja na utajenga

Binafsi sitaki ubweteke na hako kamshahara cha laki 8 to million 1.5 etc ngoja nikwambie yawezekana Mungu amekutengea
uweze kushika zaidi ya hiyo unayopata kwenye mshahaara,,,je uoni ajira ni laana ??na kama ndio kwa nini usifungue mawazo yako
ya kushika milion mbili na nusu mpaka tatu kwa mwezi...

Mwisho nakutakia usiku Mwema na Mungu akupe ufahamu wako uweze kuwa wa maana milele
Nte "MEMA YA NCHI TUNAKULA HAPA HAPA DUNIANI""KASOME BAIBO HAKUNA NCHI MBINGUNI NCHI IKO HAPA HAPA KAMATA HAKI YAKO

ALL THE BEST
 
Fanya kazi, jenga nchi kijana, acha mawazo finyu, ajira za wahindi ndizo utumwa, kazi tembo mshahara sisimizi.
 
Ingawa sio utumwa, kazi nyingi hazimridhishi binadamu kisaikolojia hata kama zinalipa.
 
Back
Top Bottom