Waziri wa miunombinu wa serikali ya mapinduzi ya zanzibar awasilisha barua ya kujiuzulu kwa rais wa zanzibar kufuatia ajali ya meli ya skargit na rais amekubali na kumteua waziri mwingine bwana rashid seif kutoka cuf
Ndio maana hawa jamaa wanataka nchi yao.Waziri wa miunombinu wa serikali ya mapinduzi ya zanzibar awasilisha barua ya kujiuzulu kwa rais wa zanzibar kufuatia ajali ya meli ya skargit na rais amekubali na kumteua waziri mwingine bwana rashid seif kutoka cuf
[h=2]Saturday, July 21, 2012[/h][h=3]Waziri Masoud: Sioni sababu ya kujiuzulu[/h]
Asema Dhoruba Ilizamidha Mv Skagit
Na Waandishi wetu
WAZIRI wa Miundombinu na Mawasiliano, Hamad Masoud Hamad, amesema haoni sababu ya kujiuzulu nafasi yake, kufuatia janga la kuzama kwa meli ya MV.Skagit iliyopoteza maisha ya zaidi ya watu 60.
Waziri Masoud alisema meli hiyo ilizama kutokana na janga la kimaumbile, kufuatia upepo mkali uliosababisha mawimbi na hatimaye kuzama kwa boti hiyo.
Alisema haoni sababu ya msingi ya kujiuzulu kufuatia ajali ya kuzama kwa meli hiyo licha ya kutokea ndani ya kipindi cha mwaka mmoja tangu kuzama kwa meli ya MV. Spice Islander.
Alikiri kuwepo kwa maoni ya watu kumtaka ajiuzulu na kuwaeleza watu wa aina hiyo kuwa hakuna mtu anayeweza kuzuia majanga ya kimaumbile kama upepo yasitokezee.
"Kumekuwa na watu wanaotoa maoni juu ya suala la kujiuzulu, lakini bado hakuna mtu anayeweza kuzuiya upepo usitokee kwani hauko katika mamlaka yake",alisema waziri huyo.
"Kuna wengine wanasema tumemkosa kule sasa watanipatia kwa hili, nimeshapata taarifa kuwa kuna ‘private member' watapeleka hoja katika Baraza la Wawakilishi ya kujiuzulu, nimeshasikia na wimbo huu unaimbwa tena na natumiwa meseji kuulizwa nitajiuzulu wakifa wangapi kwani mimi napenda kuua", alisema..
, utaona kuwa wakati anasema kuwa hatajiuzulu NG'O tarehe 21 Julai, kumbe tarehe 20 Julai alikwisha muandikia Raisi barua ya kujiuzulu. Ukweli uko wapi?"Tarehe 20 Julai, 2012 Waziri wa Miundombinu na Mawasiliano Mheshimiwa Hamad Masoud Hamad alimuandikia barua Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mheshimia Dk Ali Mohammed Shein kumuomba ajiuzulu kufuatia ajali ya kuzama kwa meli ya Mv Skagit iliyotokea Julai 18,2012," Ilisema taarifa ya Dk Mzee.
hussein mwinyi aligoma milipuko ya mabomu mbagala,gongolamboto