Ajali ya moto: Nyumba yateketea: Imechomwa na mke wa mpangaji

Benno

JF-Expert Member
Nov 21, 2009
332
51
Ugomvi wa mke na mume ambao ni wapangaji katika nyumba hii umesababisha hasara kubwa na upotevu wa mali nyingi.

Mke na mume walianza ugomvi asubuhi; mke akidai Mwanaume hanunui Nyama. Mke alichoma godolo, mume akazima moto na kuondoka kwenda polisi staki shari kutoa polisi, mwanamke ( aisha ) akapata nafasi ya kuchoma tena godolo na ndipo moto ukashika nyumba nzima,

Kabla hajachoma godolo, alinoa kisu na kumtishia, Omari alifanikiwa kunyang'anya kisu.


Uharibifu mkubwa umetokea kwetu sote na vifaa vingi kupotea.


Zima moto walifika eneo la tukio na kusaidia juhudi za wananchi waliofanikisha kuutuliza usisambae kwa majirani.

Wapangaji wengine na ndugu wa mwenye nyumba waliokuwa wakiishi humu ndani wamepoteza kila kitu.


BI AISHA ANATAFUTWA NA POLICE: ALIKIMBIA BAADA YA MOTO KUSAMBAA
 
Zima moto waliwahi eneo latukio na kusaidia juhudi za wananchi waliokuwa wakitumia ndoo
 

Attachments

  • Photo-0014.jpg
    Photo-0014.jpg
    37.1 KB · Views: 56
  • Photo-0032.jpg
    Photo-0032.jpg
    45.7 KB · Views: 52
Ni nyama gani hiyo jamani!...nyama hii hiii tunayoifahamu wote aman ni nyama nyingine?.........dah, watu wanatiana umaskini na hali ya maisha ilivyo ngumuuu!! dah, sasa nyumba imetiwa kiberiti na sidhani kama ilikuwa na bima!!!! hawa watu wataishi vp?....huyo dada kichaa ni kumpiga miaka 30 ndani akili ikae sawa. Lakn mh, huko jela akikosa "nyama" si atachoma moto gereza na kuangamiza watu!!!!!! Lo.
 
Back
Top Bottom