Ajali ya Meli: Serikali yetu na utata wa idadi ya abiria walioangamia

Jaman tuache siasa,serikal ya zanzibar ifanye tathmin na kujua idad halis ya watu waliopoteza maisha kutokana na ajal hii,kama hao watu wa wete wamekuja na data kwamba watu 1141 wamepoteza maisha,serikal achen longolongo.
 
Masikini mtoto wa mkulima sijui atalia tena bungeni au?ndipo atakapo tambua kuwa uwaziri mkuu si bla bla!
 
Inasikitisha kwa kweli kwa kutokuwa na takwimu sahihi ya watu waliokuwepo kwenye meli.
 
kwa hii tathmini lazima serikali iumbuke..very simple!!haiwezekani idadi ya watu wanaotajwa iwe ni ile pekee ya waliopatikana maiti...ilihali watu hawalali majumbani mwao wakisubiri labda ndugu zao watarudi toka safarini..mbaya zaidi ana kumbukumbu ya either sms au call wakat ule ndugu yake analalamika meli inajaa maji/inayumba/imejaza sana...i mean ana uhakika ndugu yake alikua kwenye meli ile..si mmoja!!mamia kwa maelfu wanalia ndugu zao hawajafika...tafadhali mh mbunge endelea kutukusanyia idadi kamili.
 
go on CUF ..serikali hapa ndio imezembea na nashangaa hadi sasa hivi hakuna tamko lolote na kuvihakiki vyombo vyote vya majini
 
Huu msiba utajenga umoja miongoni mwao wa zanzibar....na mtihani kwa serikali ya umoja wa kitaifa
 
Inawezekana idadi ya waliopoteza maisha ikazidi ile ya MV Bukoba?
Serikali hii hakuna kitu inachoweza zaidi ya ufisadi na rushwa tu.
 
Mbunge wa Ole, Rajab Mbarouk alisema anakusudia kupeleka hoja binafsi bungeni ili kumwajibisha Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kwa tukio hilo.

Akizungumzia suala la Waziri Mkuu mbunge huyo alisema: “Sisi ni wasemaji wa wananchi siyo Serikali. Nina mpango wa kupeleka hoja binafsi Bungeni ili Waziri Mkuu awajibike.”

Alieleza sababu za kutaka Waziri Mkuu awajibike kuwa ni pamoja na Serikali kupuuza swali lake alilouliza bungeni kuhusu usalama wa vyombo vya majini hadi sasa.

(Naomba niiweke tena hii post hapa)

Huyo mbunge anamlinda nani? Kama ni hoja binafsi basi anatakiwa apeleke Baraza la Wawakilishi lakini sio kwenye Bunge la Muungano. Miaka yapata 3 hivi Sumatra walipigwa mararufuku kufanya kazi Zanzibar na kama nakumbuka vizuri kipindi hicho Sumatra walikuwa wanaongelea MV Serengeti kutakana na ubovu wake. Zanzibar ilisimama kidete na kusema Sumatra haina mamlaka Zanzibar.

Pili, baada ya Baraza la wawakilishi kubadilisha katiba na kuifanya Zanzibar kuwa nchi kamili, Mh Ole Rajab Mbarouk anaweza kutuambia nafasi ya Waziri Mkuu ni ipi? Kazi za Waziri Mkuu kwa upande wa Zanzibar ni zipi hasa chini ya hii serikali ya umoja wa kitaifa? Pia kwa nini arukie Waziri mkuu na sio Waziri wa uchukuzi wa Zanzibar? Nani amemtuma huyu Mbunge? Narudia, Mh mbunge anamlinda nani?
 
nani atathibitisha kuwa walikuwepo humo ni zaidi ya 3000..
Si rahisi kuthibitisha kama walikuwa 3000 kamili, lakini ni rahisi kuthibitisha idadi halisi yoyote kwani waliofariki na kuonekana, walionusurika na waliopotea ni watu ambao wana jamaa zao. Ni suala la kupita kila shehia (jina la kata kwa ZNZ) na kujua waliopotea, walionusurika na waliokufa na kuonekana.
Kutokana na takwimu zilizotolewa na Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini, idadi hiyo ni 2511. Kuna uwezekano wa kuwa watu 489 hawajaonekana ili kutimiza idadi ya 3000? Sielewi kama ambavyo serikali haielewi mmiliki wa meli.
 
Ndugu za abiria waliokuwa wakizama na meli ya MV.SPICE walianza kupata taarifa mara meli ilipoanza kuingia katika dalili za wazi za kuzama,hiyo ilikuwa ni usiku wa saa saba.Meli ilipozama na kubaki watu wachache juu ya mgongo wa meli simu ziliendelea kupigwa na wahanga hao.

Hatimae meli ilizama na baadhi ya wahanga kudandia kwenye mlingoti wa meli huku wakiendelea kuomba msaada kwa majonzi kwamba muda wowote na wao wangezama hiyo ilikuwa ni baina ya saa 9 -10 alfajiri.Baada ya hapo hakukuwa na mawasiliano tena na watu hao.Simu baina ya ndugu ndizo ziliwaamsha watu wengi kote Tanzania.
Kwa maelezo ya waliookoka shughuli hasa za uokoaji zilianza asubuhi.Ni wazi kuwa kulikuwa na uzembe katika kila nyanja.Baadhi ya nyanja uzembe ulikofanyika ni kwenye mashirika ya simu.Jee hakuna kitu cha kuonesha ongezeko la watumiaji simu muda ambap si wa kawaida?.

Uzembe mkubwa itakuwa ulifanyika Zanzibar kwenyewe. Vyombo vya Usalama na wahusika wa bandari walikuwa wapi wakashindwa kuona hali ya meli tangu saa 12.30 jioni?.Ofisi ya kukutisha tiketi kwanini haikuwa na mawasiliano na wenzao wa Dar kuonesha kuwa hakukuwa na nafasi tena ya kupakia meli itakapofika Zanzibar.
Hali ya tukio iliendelea kuripotiwa kama lilivyokuwa mpaka pale serikali ya Jakaya Kikwete na vyombo vyote vya ulinzi ilipoamka na kuteka shughuli yote.Kuanzia hapo watu wakatakiwa kupata taarifa zilizoitwa sahihi kupitia vyombo vya habari vya serikali vilivyofanya kazi kubwa ya kupotosha idadi ya waliookolewa na maiti waliopatikana.

Wabunge na wawakilishi huko Pemba wanastahiki pongezi kwa kuweza kwa muda mfupi kupata takwimu za watu waliopanda kwenye meli hiyo na ambao mpaka sasa wanahesabiwa kwamba wamekufa.Kufuatia juhudi zao gazeti la Mwananchi lilmeandika.

MV Spice ilipakia abiria 3000

Habari hii ni ya UONGO meli hii haikuzama kamaunavyotaka tumini MV Spice Islander ilipinduka na kuzama, kwahiyo hakukuwa na chance ya kupanda mlingoti, Source yako itakuwa imekudanganya
 
Kwakweli haya ni mambo ya aibu sana yanayotokea. Kwanza kabla ya safari na baada ya ajali na pili mambo hutokea mara kwa mara japo ajali tunanusulika nazo.

Kwa mtazamo wangu hapo kumetokea ajali hapa zilikuwa mbili yaani kuzama kwa meli na kupinduka. Sasa kuzama kwa meli inaweza kuwa kawaida(mimi sikubaliani) lakini kupunduka kwa meli ni uthibitisho wa poor stability wa meli hiyo. Hili la pili inaweza kusababishwa na upakiaji mbovu wa mizigo au baada ya meli kuanza kuvuja ikasababisha hali hiyo. Hata hivyo swala la overloading ni obvious. Kwa mfano Zanzibar walireport wanaondoka na abiria 500 na mzigo tani 95 lakini waliookolewa tu wanazidi 600. Therefore hawa jamaa manifest yao ni danganya toto tu.

Haya yamekwishatokea. Cha ajabu kuliko vyoote duniani, hakuna taarifa ya kupokea any SOS or distress calll katika radio station yeyote iwe ya MRCC au port control tower. Na sitarajii kama inawezekana meli kupata matatizo kama haya na iisitume SOS au may day kwa vituo nilivyovitaja. Kama walitumia VHF radio, Dar wanaweza kuwa hawakusikia lakini signal station Ya Zanzibar lazima wawe wamesikia au hakukuwa na ntu kwenye kituo. Pia meli hiyo haikuwa na HF radio(SSB) ili kuita Dar? ajabu sana, au meli haikuwa na vifaa kamili vya mawasiliano? Kuna tetesi kwamba kulikuwa na jitihada za makusudi usiku huo kuita signalstation ya Zanzibar ili kuconfirm uvumi (kwa wakati huo) lakini signal ya Zanzibar haikuwa na majibu.STRANGE. Yako mengi sana ya kustajabisha kama hakukuwa na muda wa kutupa mizigo baharini kupunguza hatari?(jettsoning).Dah nafasi sina lakini kuna mengi ya ajabu.
 
Back
Top Bottom