EasyFit
JF-Expert Member
- Jul 4, 2011
- 1,269
- 1,082
- Nusura achelewe muda wa kuchukua fomu.
Ajali hiyo ilitokea saa 5:30 asubuhi katika eneo liitwalo Parking (maegesho ya magari makubwa) Mjini Igunga, ambako mtoto huyo aligongwa na kupasuliwa kichwa na lori aina ya Mitsubishi Fuso.
CCM kilikuwa kimefanya maandalizi makubwa ambapo pikipiki aina ya Bajaji zaidi ya 20 na magari yalikuwa katika msafara wa kumpokea Dk Kafumu katika eneo hilo la Parking.
Baiskeli na pikipiki za kawaida pia zilikuwa katika mpango wa mapokezi huku zikiwa zimepambwa kwa bendera za CCM na kila upande wa mji ukiwa na bendera hizo.Kutokana na tukio hilo, Dk Kafumu alilazimika kuchukua fomu bila shamrashamra zozote kutokana na muda kutomruhusu kuahirisha uchukuaji huo.
Msimamizi wa uchaguzi jimbo la Igunga, Magayane Protas alisema pamoja na tukio hilo kutokea ni lazima fomu zichukuliwe kwa kuwa kesho (leo) hatakuwa na nafasi kutokana na kuwapo na ratiba nyingine ya kikao cha viongozi.
Nimewaambia lazima wachukue fomu leo kwa kuwa kesho (leo) nitakuwa na kikao na uongozi, alisema.
Kafumu alichukua fomu saa 8:00 mchana.
Source: Mwananchi.