cheusimangala
JF-Expert Member
- Feb 27, 2010
- 2,585
- 497
Asalam aleykum.
Mashosti ajali hii inayotuhusu kina mama imetokea hapa kwenye airport kubwa kuliko zote ulaya magharibi ambako niko transit kwa muda sasa nikisubiri boarding time kuelekea kwenye my last destination.
Katika kupoteza muda bila kusinzia uwanjani hapa niliamua kutembea tembea sehemu mbalimbali zilizoko ndani ya uwanja huu mkubwa na wenye kuvutia.Nimekua naingia kutoka duka moja na kuingia jengine.Nikiwa natoka ndani ya duka fulani la designer mkubwa wa kiitaliano huku nikiwa naelekea kwenye zile ngazi za umeme ili zinifikishe ilipo internet cafe hii ambayo ndimo ninamorusha uzi huu,kwa mbele yangu nilimuona dada fulani aki-srutt kwa madaha juu ya high heels ambayo ina kama inchi saba hivi na yeye akielekea zilimo hizo ngazi.Nikiwa nyuma ya mdada pua zangu ziliweza kufaidi harufu nzuri ya manukato ya bei ya gharama aliyojipulizia mdada huyu,kwa kweli kuanzia kichwani hadi miguuni mdada alivaa vitu vya gharama tuu,nilizipenda nywele zake ndefu nyeusi zenye mawimbi yaliyomwagika hadi mgongoni,ngozi yake nyeusi ilikua nzuri na laini kuonyesha kwamba ilikua ikihudumiwa kwa body cream/lotion za gharama ,kwakifupi mdada alikua kwenye class ya nyota tano.
Macho yangu yalivutiwa na hizo high heels alizokua amezivaa,moyo wangu ulivipenda hivyo viatu,nikajiapiza kuwa nikijua vinapouzwal azima nivinunue japo vilionekana ni vya ghali sana.Hapa nikajiambia sijui nitapataje mwanya wa kumuuliza huyu mdada aliponunua hivyo viatu vyake.
Basi tukafika kwenye ngazi mdada akawa wa kwanza kupanda mim nikawa nyuma yake na watu wengine wengi tu pia walikuwepo,wote wakiwa wazungu isipokua mim na huyu mdada tu ndio tulikua weusi.
Ngazi ikawa ikitushusha taratiibu huku yule mdada akiwa amepouzi kwa mapozi yanayoonesha kuwa alijua amependeza na kweli mdada alikua kapendeza hata sura yake ilikua ni nzuri japo hainifikii yangu,pia dada alionesha kuwa ni mdada mwenye kujiamini.
Tulipofika chini dada akaanza kunyanyua mguu wake wa chupa ya bia kwa madaha kwa lengo la kutoka kwenye ngazi hizo lakini maskini ya mungu sijui ilikuaje mdada akateleza na kudondoka na kulalia mgongo kitendo kilichofanya yesuuuu initoke.Mara moja kuna mtu akabonyeza kitufe cha kuzima hizo ngazi ziache kuzunguka,na ziliposimama mama mmoja wa kizungu akampa mdada mkono kwa lengo la kumsaidia kunyanyuka lakini mdada aliponyanyuka wazungu woote waliokuwepo pale pamoja na mim cheusie tulijikuta tukibaki midomo wazi huku kauli zikiwa zimetukatika kwa sekunde nyingi,sikuamini nilichokiona,kumbe mdada yule aliyekua mrembo but not now any more alikua kavaa wigi,sasa alipodondoka wigi lake likanasa kwenye zile ngazi na aliposaidiwa kunyanyuka wigi likabaki pale chini ndo sasa kila mtu aliyeko pale akashuhudia kichwa chake halisi kilivyo,yaani yule mdada nywele zake zilikua ni chafu zinanuka uvundo,juu juu ya nywele kulikua na maukoko kama magamba ya vidondo,uwiiii,huko kichwani kulikia kuna kama mauzi mauzi ya mablanketi,kuna upande alikua kasuka mabutu ,upande kasuka mistari kuna upande hajasuka kuna sehemu hakuna nywele zimenyonyoka kama wale watoto wanaokuwaga na yale sijui ndo yanaitwa mapunye sijui mashilingi,kumbe lile wigi lilikua limeficha mengi,dada ana uchogo balaa halafu kichwa chenyewe kidogo ka ngogwe halafu kwa mbele ana komwe sasa,yaani kwaharaka utadhani yule I.T .
Wanaume wote waliokua wakimkodolea macho hapo mwanzo sikujua waliondoka saa ngapi,mdada alikua anaona aibu,yale mapozi ya najua nimependeza na ya kujiamini yakayeyuka.Wazungu wote wakakaa pembeni wakimshangaa nikabaki mim na mdada na mim nikataka kuondoka maana wazungu walikua wanaangalia kichwa cha mdada halafu wanaangalia lile wigi lililonasa pale chini halafu wanangalia kichwani kwangu nikasema hapa lazima nisepe ila nikakumbuka kuwa nataka anambie alinunua wapi viatu vyake hivyo nikasema huu ndo wakati wakujua.
Nikajifanya kauzu,nikainama pale chini nikajaribu kuvuta lile wigi halikuchomoka,nikamuuliza do you speak english?Akanambaia kwa kishwahili,ndio ila na mim naongea kiswahili,nikamwambia umejuaje kuwa mim naongea kishwahili akasema nimekusikia ukisema yesuuuu,basi nikamwambia abonyeze pale yule mtu alipobonyeza ili ngazi ziwake labda wigi lake litachomoka.Anyway,kwa kifupi nimefanikiwa kumchomolea wigi lake akalivaa haraka haraka nakuondoka ila nimeshajua viatu vyake vinauzwa wapi na pia nimejua ni mtanzania mwenzangu.
Haya mim nawarushia huu uzi labda kuna chochote kina dada wenzangu mtakua mmjejifunza,nikisharusha huu uzi naenda kutafuta vile viatu maana yule mdada kasema hilo duka hata humu ndani lipo,baada ya hapo muda si mrefu nitakuwa on board.Sitaweza kucoment lolote kwa sasa ila nikifika niendako na kupumzika nitakuja kuwacheki.
Nitakieni safari njema.
Mashosti ajali hii inayotuhusu kina mama imetokea hapa kwenye airport kubwa kuliko zote ulaya magharibi ambako niko transit kwa muda sasa nikisubiri boarding time kuelekea kwenye my last destination.
Katika kupoteza muda bila kusinzia uwanjani hapa niliamua kutembea tembea sehemu mbalimbali zilizoko ndani ya uwanja huu mkubwa na wenye kuvutia.Nimekua naingia kutoka duka moja na kuingia jengine.Nikiwa natoka ndani ya duka fulani la designer mkubwa wa kiitaliano huku nikiwa naelekea kwenye zile ngazi za umeme ili zinifikishe ilipo internet cafe hii ambayo ndimo ninamorusha uzi huu,kwa mbele yangu nilimuona dada fulani aki-srutt kwa madaha juu ya high heels ambayo ina kama inchi saba hivi na yeye akielekea zilimo hizo ngazi.Nikiwa nyuma ya mdada pua zangu ziliweza kufaidi harufu nzuri ya manukato ya bei ya gharama aliyojipulizia mdada huyu,kwa kweli kuanzia kichwani hadi miguuni mdada alivaa vitu vya gharama tuu,nilizipenda nywele zake ndefu nyeusi zenye mawimbi yaliyomwagika hadi mgongoni,ngozi yake nyeusi ilikua nzuri na laini kuonyesha kwamba ilikua ikihudumiwa kwa body cream/lotion za gharama ,kwakifupi mdada alikua kwenye class ya nyota tano.
Macho yangu yalivutiwa na hizo high heels alizokua amezivaa,moyo wangu ulivipenda hivyo viatu,nikajiapiza kuwa nikijua vinapouzwal azima nivinunue japo vilionekana ni vya ghali sana.Hapa nikajiambia sijui nitapataje mwanya wa kumuuliza huyu mdada aliponunua hivyo viatu vyake.
Basi tukafika kwenye ngazi mdada akawa wa kwanza kupanda mim nikawa nyuma yake na watu wengine wengi tu pia walikuwepo,wote wakiwa wazungu isipokua mim na huyu mdada tu ndio tulikua weusi.
Ngazi ikawa ikitushusha taratiibu huku yule mdada akiwa amepouzi kwa mapozi yanayoonesha kuwa alijua amependeza na kweli mdada alikua kapendeza hata sura yake ilikua ni nzuri japo hainifikii yangu,pia dada alionesha kuwa ni mdada mwenye kujiamini.
Tulipofika chini dada akaanza kunyanyua mguu wake wa chupa ya bia kwa madaha kwa lengo la kutoka kwenye ngazi hizo lakini maskini ya mungu sijui ilikuaje mdada akateleza na kudondoka na kulalia mgongo kitendo kilichofanya yesuuuu initoke.Mara moja kuna mtu akabonyeza kitufe cha kuzima hizo ngazi ziache kuzunguka,na ziliposimama mama mmoja wa kizungu akampa mdada mkono kwa lengo la kumsaidia kunyanyuka lakini mdada aliponyanyuka wazungu woote waliokuwepo pale pamoja na mim cheusie tulijikuta tukibaki midomo wazi huku kauli zikiwa zimetukatika kwa sekunde nyingi,sikuamini nilichokiona,kumbe mdada yule aliyekua mrembo but not now any more alikua kavaa wigi,sasa alipodondoka wigi lake likanasa kwenye zile ngazi na aliposaidiwa kunyanyuka wigi likabaki pale chini ndo sasa kila mtu aliyeko pale akashuhudia kichwa chake halisi kilivyo,yaani yule mdada nywele zake zilikua ni chafu zinanuka uvundo,juu juu ya nywele kulikua na maukoko kama magamba ya vidondo,uwiiii,huko kichwani kulikia kuna kama mauzi mauzi ya mablanketi,kuna upande alikua kasuka mabutu ,upande kasuka mistari kuna upande hajasuka kuna sehemu hakuna nywele zimenyonyoka kama wale watoto wanaokuwaga na yale sijui ndo yanaitwa mapunye sijui mashilingi,kumbe lile wigi lilikua limeficha mengi,dada ana uchogo balaa halafu kichwa chenyewe kidogo ka ngogwe halafu kwa mbele ana komwe sasa,yaani kwaharaka utadhani yule I.T .
Wanaume wote waliokua wakimkodolea macho hapo mwanzo sikujua waliondoka saa ngapi,mdada alikua anaona aibu,yale mapozi ya najua nimependeza na ya kujiamini yakayeyuka.Wazungu wote wakakaa pembeni wakimshangaa nikabaki mim na mdada na mim nikataka kuondoka maana wazungu walikua wanaangalia kichwa cha mdada halafu wanaangalia lile wigi lililonasa pale chini halafu wanangalia kichwani kwangu nikasema hapa lazima nisepe ila nikakumbuka kuwa nataka anambie alinunua wapi viatu vyake hivyo nikasema huu ndo wakati wakujua.
Nikajifanya kauzu,nikainama pale chini nikajaribu kuvuta lile wigi halikuchomoka,nikamuuliza do you speak english?Akanambaia kwa kishwahili,ndio ila na mim naongea kiswahili,nikamwambia umejuaje kuwa mim naongea kishwahili akasema nimekusikia ukisema yesuuuu,basi nikamwambia abonyeze pale yule mtu alipobonyeza ili ngazi ziwake labda wigi lake litachomoka.Anyway,kwa kifupi nimefanikiwa kumchomolea wigi lake akalivaa haraka haraka nakuondoka ila nimeshajua viatu vyake vinauzwa wapi na pia nimejua ni mtanzania mwenzangu.
Haya mim nawarushia huu uzi labda kuna chochote kina dada wenzangu mtakua mmjejifunza,nikisharusha huu uzi naenda kutafuta vile viatu maana yule mdada kasema hilo duka hata humu ndani lipo,baada ya hapo muda si mrefu nitakuwa on board.Sitaweza kucoment lolote kwa sasa ila nikifika niendako na kupumzika nitakuja kuwacheki.
Nitakieni safari njema.