Ajali Tanzania: Mawazo mbadala kuhusu udhibiti wa ajali Tanzania

KIKOSI cha polisi wa usalama barabarani kimeanzisha mpango kazi kwa kuwashirikisha askari wa vikosi vingine kama njia ya kupunguza ajali na malalamiko kwa askari wake.

Kauli hiyo imetolewa jana na Ofisa Mnadhimu wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Kamishna Msaidizi Mohammed Mpinga alipotoa taarifa ya kikosi chake nchini.

Alisema mpango huo utasaidia kudhibiti vitendo vya rushwa, ajali na kupunguza lawama kwa polisi wa usalama barabarani.

Akizungumzia utoaji wa leseni mpya, Kamanda Mpinga alisema mikoa tisa imetengwa na kujengewa uwezo wa kutengeneza mifumo ya kompyuta kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mapato (TRA).

Aliitaja mikoa itakayohusika kwa utoaji wa leseni awamu ya kwanza kuwa ni Arusha, Kilimanjaro, Tanga, Ilala, Temeke, Kinondoni, Mbeya, Dodoma na Mwanza.

Kamanda huyo alisema utaratibu wa vikosi kazi utaenea kila mkoa na kusaidia katika kupambana na makosa ya usalama barabarani na ajali kwa ufanisi.
 
Kwanini wasijaribu kuweka traffic police kwnye kila basi linalo safiri kwenda mikoani kwa gharama za hizo company ? au hata kwenye mabasi ya kampuni zinazo pata hajali zaidi ,nadhani hilo litapunguza idadi ya ajali maana kama ndani ya basi kuna traffic police sidhani kama dreva anaweza endesha mwendo kasi au hata hizo overtake zao zisizo na akili haziwezi fanyika na hata itakapo tokea hiyo ajali huyo police ata wajibika kueleza ilitokeaje na yeye alikuaw api kuweza saidi hilo lisitokee, .. sidhani kama kuna njia nyingine ya kupunguz vifo vizivyo na ulazima.

Tunajau suala la rushwa lipo, so ina wezekana huyo police atahongwa na speed ikawa pale pale, nadhani pia wasafiri washirikishwe kwa kutoa taarifa kw anjia ya sms

Ifanyike kama hivi, KIla ticket iweime andikwa number ambayo abiria anaweza sms kueleza kuhusu uendeshaji wa dreva ukoje na wa hatari kiasi gani .

Police anapo ingia kwenye basi atakiwe atangaze number yake ya utambulisho amabayo anakua amepewa na mamalaka ya usafiri kwa abiria.

Baada ya kutangaza namba anatakiwa kuwaelezea kua yeye yuko pale kuweza ku kudhibiti uendeshaji mbovu wa madereva ,kama aabiria wakiona kua kuna speed na uendeshaji mbaya wan weza ku sms mesege kwenye number fulani, mbayo hizo sms zitatumika kama kielelezo cha jinsi hali ilivyo kuwa kwa uendeshaji wabasi kwa safdari nzima, endapo ajali itatokea huo ujumbe utaweza kua ni moja ya ushahidi wa kutuhumu hyo police hakua ana fanya kazi yake vizuri.

Zoezi zima lina weza kua na gaharama ila gharama zote ziwe kwa wenye makampuni ya mabasi kwa gharama za safari na posho kwa huyo police .Sidhani kama gharama ni tatizo hasaa ukizingatia ajali zinavyo wapa watu garama za maisha na ulemavu , kuepuka yote hayo na dhani ni jamb muhimu kifanyike kuweza kupunguz ahizi ajali zisizo za lazima.

Tunaweza kuanzia hapa au kuboresha zaidi hiki nilicho kiongelea
maoni wadau
__________________
 
Ingawa mara nyingi watu wanasema ajali haina kinga, mimi nasema ajali nyingi zinazotokea hapa nchini zina kinga, ambayo ni kuendesha gari kwa kuheshimu sheria za barabarani na kwa uangalifu. Kama idadi kubwa ya madereva watazingatia haya, wataweza kupunguza ajali nyingi sana! Kungekuwa na mfumo mzuri wa kuwathibiti madereva wahuni (wanaoendesha magari kihuni) tungeweza kuzuia ajali nyingi sina.

Lakini kuendelea kuhuzunika na kutoa ubani kwa wafiwa hakusaidii kitu kama taifa linaendelea kupoteza raslimali watu kila siku kutokana na ajali za barabarani na majini na kufanya wanaosalimika katika ajali hizo kuwa na ulemavu wa kudumu na wao wenyewe kuwa tegemezi. Ajali iliyotokea huko Morogoro juzi na ajali zingine zinazotokea hapa nchini zinatutia huzuni sana. Inasikitisha!

Ombi langu kwa wabunge wetu ni kuwasilisha mswada bungeni ili Sheria ya Usalama Barabarani ifanyiwe marekebisho na kumfanya dereva anayesababisha ajali kwa uzembe wake awajibike zaidi - ikiwa ni pamoja na kulipa fidia (na kama hana hela afanye kazi za kijamii ili hela hiyo ipelekwe kwenye familia za walioachwa na wapendwa wao au majeruhi) na kuwa na kesi ya kusababisha kifo/vifo au ulemavu wa muda au wa kudumu kwa majeruhi.

Ili kuwathibiti wenye magari wasiwaajiri madereva wahuni kwa kukwepa kuwalipa madereva wazuri mshahara mzuri, hawa nao wawajibike 'vicariously'. Inawezekana sheria ya zamani inasema hivi lakini ingepewa meno zaidi. Kitu kingine ni kubeba abiria kulingana na uwezo wa gari na siyo tamaa ya mwenye gari, dereva au kondakta. Lakini kwa hali ilivyo sasa hivi, abiria na mizigo wana thamani sawa. Hebu angalia magari ya abiria yanavyojazwa watu utafikiri ni kokoto! Hii ni hatari sana!

Vilevile speed ya magari ithibitiwe! Mbona Ulaya magari mengi yanaenda mwendo unaokubalika kisheria lakini hapa kwetu sivyo? Jamani, inasikitisha sana na hasa haya magari ya daladala kuona yanaendeshwa na madereva na makondakta wahuni (baadhi yao wakiwa wala unga, wapiga debe)! Hivi kwa nini serikali haliweki mfumo mzuri wa kuwathibiti hawa wahuni wanaotuangamiza au kutufanya tuwe na vilema vya kudumu kila siku?
 
Ingawa mara nyingi watu wanasema ajali haina kinga, mimi nasema ajali nyingi zinazotokea hapa nchini zina kinga, ambayo ni kuendesha gari kwa kuheshimu sheria za barabarani na kwa uangalifu. Kama idadi kubwa ya madereva watazingatia haya, wataweza kupunguza ajali nyingi sana! Kungekuwa na mfumo mzuri wa kuwathibiti madereva wahuni (wanaoendesha magari kihuni) tungeweza kuzuia ajali nyingi sina.

Lakini kuendelea kuhuzunika na kutoa ubani kwa wafiwa hakusaidii kitu kama taifa linaendelea kupoteza raslimali watu kila siku kutokana na ajali za barabarani na majini na kufanya wanaosalimika katika ajali hizo kuwa na ulemavu wa kudumu na wao wenyewe kuwa tegemezi. Ajali iliyotokea huko Morogoro juzi na ajali zingine zinazotokea hapa nchini zinatutia huzuni sana. Inasikitisha!

Ombi langu kwa wabunge wetu ni kuwasilisha mswada bungeni ili Sheria ya Usalama Barabarani ifanyiwe marekebisho na kumfanya dereva anayesababisha ajali kwa uzembe wake awajibike zaidi - ikiwa ni pamoja na kulipa fidia (na kama hana hela afanye kazi za kijamii ili hela hiyo ipelekwe kwenye familia za walioachwa na wapendwa wao au majeruhi) na kuwa na kesi ya kusababisha kifo/vifo au ulemavu wa muda au wa kudumu kwa majeruhi.

Ili kuwathibiti wenye magari wasiwaajiri madereva wahuni kwa kukwepa kuwalipa madereva wazuri mshahara mzuri, hawa nao wawajibike 'vicariously'. Inawezekana sheria ya zamani inasema hivi lakini ingepewa meno zaidi. Kitu kingine ni kubeba abiria kulingana na uwezo wa gari na siyo tamaa ya mwenye gari, dereva au kondakta. Lakini kwa hali ilivyo sasa hivi, abiria na mizigo wana thamani sawa. Hebu angalia magari ya abiria yanavyojazwa watu utafikiri ni kokoto! Hii ni hatari sana!

Vilevile speed ya magari ithibitiwe! Mbona Ulaya magari mengi yanaenda mwendo unaokubalika kisheria lakini hapa kwetu sivyo? Jamani, inasikitisha sana na hasa haya magari ya daladala kuona yanaendeshwa na madereva na makondakta wahuni (baadhi yao wakiwa wala unga, wapiga debe)! Hivi kwa nini serikali haliweki mfumo mzuri wa kuwathibiti hawa wahuni wanaotuangamiza au kutufanya tuwe na vilema vya kudumu kila siku?

Mkuu tatizo serikali na wahusika wake wako bize kubadili sheria ambazo zitawanufaisha, kama sheria za manunuzi ya uma, hii itakuwa ngumu sana kudhibiti mambo mengine ambayo yanawagusa watanzania moja kwa moja.

Vile vile udhibiti wa viwango bora vya magari ya kusafirisha abiria nalo ni jambo muhimu sana, kitu ambacho serikali imekuwa ikicheza makida makida kwa muda mrefu sana!

Embu angalia hizo picha kwenye attachment utaelewa naongelea nini.

Kingine ni kuwa na utaratibu wa kutosha kwa kutoa leseni za kuendeshea....hapa kila mmoja atakubaliana na mimi kwamba Tanzania, watu wengi wanaanza kujifunza kuendesha magari baada ya kupata leseni. Yaani leseni wanaletewa nyumbani, hata ukiwa kipofu au mlemavu au kiziwi, leseni unapata kwa kiulaini mno, coz presence yako pale mayfair kwenye leseni mpya haina uzito

Nawaachia wana JF waendelee kuchangia!

Alamsiki
 

Attachments

  • SEHEMU_YA_MABAKI_T_351_BGE_PIX_NO_5.JPG
    SEHEMU_YA_MABAKI_T_351_BGE_PIX_NO_5.JPG
    83.4 KB · Views: 173
  • SEHEMU_YA_MABAKI_T_351_BGE_PIX_NO_4.JPG
    SEHEMU_YA_MABAKI_T_351_BGE_PIX_NO_4.JPG
    27.7 KB · Views: 134
Asilimia zaidi ya 50 ya magari yaliyopo barabarani hayafai kutembea.Kwa nini tusianzishe mfumo wa kupima magari kila mwaka na kuyapa leseni ya kutembea?leseni hii iwe centralised nchi nzima na Ministry of Transport ndiyo iwe wakala wa hizi leseni.Kwani road license ina kazi gani?Magari yanatakiwa kupita kwenye system maalum kuyapima kuanzia mikanda mpaka bolt and nut zote zilizo kwenye gari.Kuwe na official centres za kufanyi haya yote.Tuanzishe point system as well.Ukikutwa unaendesha umelewa,utolewe points kwenye license yako pamoja na faini na kufikishwa mahakamani.TRA should collect all the moneys collected from all these.Kwa nini tunaogopana?Sheria za uwajibikaji zinabidi zianziswe kuokoa maisha ya yetu sote na siyo kuuana kiuzembe.
 
wakati tunaendelea na huu mjadala, watu watatu wamekufa hapo hapo, baada ya canter kugongana na basi la lucky star uso kwa uso, wakati basi hilo lilkikwepa mwendesha baiskeli, huko mikumi leo SOURCE: RADIO ONE
 
Wanajamvi
Zifuatazo ni baadhi tu ya picha jinsi gani madereva wetu wa mabasi makubwa ya abiria hasa yanaokwenda mikoani jinsi wanavyoendesha
.
18.jpg

Haya ni mabasi ya Sabi Baba, Abood, Ilas na Nganga yafanyayo safari zake kati ya Dar - Mbeya - Tunduma yakijaribu kulipita gari la tank la mafuta huku yakiwa yameongozana katika kona za milima ya Iyovi madereva wakiwa hawana wasiwasi wowote. Hivi mfano wakati wanaenda namna hii alafu mbele linatokea gari lingine tena likiwa kwenye spidi ni nini kitatokea?
19.jpg

Picha hii ni mwendelezo wa kilichojiri baada ya picha ya kwanza hapo juu
 
Mkuu umesomeka vizuri, naona hapo Nganga aliamua kujificha nyuma ya lori,angalau hakufanya upuuzi huu walioufanya Sai Baba, Abood na Ilasi zote za Tunduma hizo. Iyovi ni sehemu ya hatari tupu lkn jamaa wanalala na kona zile wakipiga overtake za kufa mtu! kimsingi madereva wetu chanzo kikubwa sana cha ajali kwa careless driving yao,followed by ubovu wa barabara na magari yenyewe!
 
  • Wajameni....enough is enough sasa....mpaka pale wanapoondoka duniani ghafla wapendwa wa wengi kwa kupitia hizi ajali za barabarani ndipo watu tz hujiuliza kwanini inakuwa hivi!! watanzania na watawala siku zote sijui inakuwaje hazipatikani njia muafaka za kuzuia hizi ajali za barabarani??.
  • Kwa taarifa tu za kusikitisha ni kwamba ajali za barabarani tz(yaani road traffic accidents-RTA)zinaongoza kwa kusababisha vifo na ulemavu tz (number one cause of morbidity and mortality in tz).......ikimaanisha ajali za barabarani zinazidi hata maradhi yote yakiwekwa pamoja kwa kuongoza kusababisha vifo na ulemavu kwa raia....hili linafaamika kwa serikali.Ninachojiuliza siku zoote...je inakuwaje hatuoni serikali inapambana na hizi ajali za barabarani kwa kasi kama inayotumika kupambana na maradhi ya kuambukiza? (e.g HIV/AIDS,TB au malaria)na pia maradhi yasiyoambukiza?(e.g kisukari na magonjwa ya moyo).Nasema hivi kwasababu ni ukweli usiopingika kuwa hizi ajali hapa tz sasa zimekuwa nongwa na wanapotea raia na hata viongozi na wanasiasa........ajali haziangalii maskini wala tajiri......wala hazisubiri eti mtu atapatiwa huduma nje ya nchi.....ajali zinakata maisha fasta(kwa tajiri na maskini)na tumeona hata viongozi na wanasiasa wa chama tawala wakiathirika kwa hili(hata wenye ukimwi wana maisha marefu siku hizi)...na ningetegemea serikali wapambane na ajali za barabarani kama vile wanavyojitapa kupambana na adui maradhi hapa tz.Ukitaka kujua balaa la ajali za barabarani tz basi tembelea kwenye idara za upasuaji(surgery)kwenye mahospitali yetu.........nenda pale MOI au Tumbi hospital alafu ujionee mortality na morbidity cases.....utalia.....kwa kifupi tembelea hospitali za rufaa tz upite idara za upasuaji na mifupa uone balaa lililopo........kule kcmc moshi wagonjwa wa wodi za mifupa(orthopaedics)kuna wakati wanakosa hata vitanda wanalala chini kwa corridor...ulizeni...
  • Ifike mahali sasa haya mambo yawe historia tz kwani inawezekana.....iweje wenzetu nchi nyingine wameweza kupunguza ajali???huwa viongozi wanajifunza nini wanapotembelea nchi za wenzetu???,hivi kweli tz tumeshindwa kuweka camera barabarani za ku monitor speed??hawa traffic kazi yao nini tz?.
  • Tanzania nchi ya jabu sana sana,...ni tz pekee utaona watu wanaenda bar kulewa na magari yao....mh!tena woote...raia wa kawaida na hata viongozi....wanakwenda bar na magari yao wanalewa alafu baadae wanarudi na magari yao manyumbani...only in tz yaani....kwa wale tuliokaa nje ya nchi mnajua zero tolerance iliyopo kwa kuendesha ukiwa hata umeonja kileo(alcohol)...lakini tz hili linawezekana kwani ni sehemu ya maisha ya watu....nobody cares...kupata leseni ya udereva tz si deal..unaweza kuhonga tu hela ukapata leseni...huitaji hata kukaa darasani kujifunza gari kwa muda mrefu...tena unaweza hata kuendesha gari bila leseni tz..tumeona hata viongozi wakiua raia wakiwa hawana leseni au wamelewa.....haya yanaonekana ya kawaida tu kwani hata adhabu zenyewe mahakamani zina mashaka......kwa kifupi niseme tu tz watu wanaishi kwa kudra za mungu saaana......Nchi inapokosa umadhubuti kwenye sheria na utendaji.... things like these(RTAs)are a common occurance......tafakari....
 
  • Wajameni....enough is enough sasa....mpaka pale wanapoondoka duniani ghafla wapendwa wa wengi kwa kupitia hizi ajali za barabarani ndipo watu tz hujiuliza kwanini inakuwa hivi!! watanzania na watawala siku zote sijui inakuwaje hazipatikani njia muafaka za kuzuia hizi ajali za barabarani??.
  • Kwa taarifa tu za kusikitisha ni kwamba ajali za barabarani tz(yaani road traffic accidents-RTA)zinaongoza kwa kusababisha vifo na ulemavu tz (number one cause of morbidity and mortality in tz).......ikimaanisha ajali za barabarani zinazidi hata maradhi yote yakiwekwa pamoja kwa kuongoza kusababisha vifo na ulemavu kwa raia....hili linafaamika kwa serikali.Ninachojiuliza siku zoote...je inakuwaje hatuoni serikali inapambana na hizi ajali za barabarani kwa kasi kama inayotumika kupambana na maradhi ya kuambukiza? (e.g HIV/AIDS,TB au malaria)na pia maradhi yasiyoambukiza?(e.g kisukari na magonjwa ya moyo).Nasema hivi kwasababu ni ukweli usiopingika kuwa hizi ajali hapa tz sasa zimekuwa nongwa na wanapotea raia na hata viongozi na wanasiasa........ajali haziangalii maskini wala tajiri......wala hazisubiri eti mtu atapatiwa huduma nje ya nchi.....ajali zinakata maisha fasta(kwa tajiri na maskini)na tumeona hata viongozi na wanasiasa wa chama tawala wakiathirika kwa hili(hata wenye ukimwi wana maisha marefu siku hizi)...na ningetegemea serikali wapambane na ajali za barabarani kama vile wanavyojitapa kupambana na adui maradhi hapa tz.Ukitaka kujua balaa la ajali za barabarani tz basi tembelea kwenye idara za upasuaji(surgery)kwenye mahospitali yetu.........nenda pale MOI au Tumbi hospital alafu ujionee mortality na morbidity cases.....utalia.....kwa kifupi tembelea hospitali za rufaa tz upite idara za upasuaji na mifupa uone balaa lililopo........kule kcmc moshi wagonjwa wa wodi za mifupa(orthopaedics)kuna wakati wanakosa hata vitanda wanalala chini kwa corridor...ulizeni...
  • Ifike mahali sasa haya mambo yawe historia tz kwani inawezekana.....iweje wenzetu nchi nyingine wameweza kupunguza ajali???huwa viongozi wanajifunza nini wanapotembelea nchi za wenzetu???,hivi kweli tz tumeshindwa kuweka camera barabarani za ku monitor speed??hawa traffic kazi yao nini tz?.
  • Tanzania nchi ya jabu sana sana,...ni tz pekee utaona watu wanaenda bar kulewa na magari yao....mh!tena woote...raia wa kawaida na hata viongozi....wanakwenda bar na magari yao wanalewa alafu baadae wanarudi na magari yao manyumbani...only in tz yaani....kwa wale tuliokaa nje ya nchi mnajua zero tolerance iliyopo kwa kuendesha ukiwa hata umeonja kileo(alcohol)...lakini tz hili linawezekana kwani ni sehemu ya maisha ya watu....nobody cares...kupata leseni ya udereva tz si deal..unaweza kuhonga tu hela ukapata leseni...huitaji hata kukaa darasani kujifunza gari kwa muda mrefu...tena unaweza hata kuendesha gari bila leseni tz..tumeona hata viongozi wakiua raia wakiwa hawana leseni au wamelewa.....haya yanaonekana ya kawaida tu kwani hata adhabu zenyewe mahakamani zina mashaka......kwa kifupi niseme tu tz watu wanaishi kwa kudra za mungu saaana......Nchi inapokosa umadhubuti kwenye sheria na utendaji.... things like these(RTAs)are a common occurance......tafakari....

mkuu huweziamini nipo kwenye basi ndio nato mizani ya dikese nimekutana na ajali ya gari sasa hivi,ukweli bora ya maradhi kuliko hizi ajali zinazotukuta sisi watanzania.gari iliyopata ajali ni toyota colora.mungu tusaidie hata trafi hakuna wamekaa barabarani wanachanga hela ya mboga tu.innakera.
 
Hapa JF tumepiga kelele weee kuhusu hizi ajali.......naona wahusika wameziba masikio..........ngoja nikaongeze hii kero ya ajali kwenye mada aliyoianzisha Mh Regia (RIP).........dahh
 
Ingekuwa ni kuchukua hatua wangekua wameshalimaliza tatizo kwani hili ni tatizo la siku nyingi sana
 
Ndg zangu wanajf,nianze kwa kuipongeza serikali ktk mkakati wao wakupunguza ajali zinazo gharimu maisha ya watanzania.
Nirudi kwenye mafanikio ambayo wamefikiwa ktk hili:
1.Imewezakusimamia na kuhakikisha madereva wote wa mabasi wanaenda kusoma na hili limetekelezwa kwa95%.
2.baada ya mafunzo hayo tumeshudia ajali za mabasi zikipungua ukiacha zile za uchakavu wa gari na kupasuka matairi.
3.hili limepelekea madereva kuwa makini kwa kuzingatia sheria za babarani kuliko tunavyofikiria.
Lakini imeshindwa ktk haya:
1.kuto simamia na madereva wa malori au magari ya mizigo kwenda kusoma.
2.Kutofanya hivi imekuwa kero babarani coz barabara zetu ni zakupishana kwa hawa wote wawili mwenye elimu na asiye na elimu.
3.Ndg zangu hawa wa malori husababisha ajali nyingi sana humo njiani,ama kudondosha magari yao wenyewe au kusabishia ajali kwa mabasi kama ile ya juzi j5 pale Mbeya,na kupelekea vifo na majeruhi kwa wasio na makosa.
Najiuliza serikali imeshindwa je na hawa nao kuwapeleka kwenye mafunzo?au huu ulikuwa mradi wa m2 ameshavuna ametosheka?
Kama imeshindwa kwanini basi wasiwaamuru kuwa muda wa kusafirisha mizigo yao ianzie mida ya jioni na siyo mida wanayofanya sasa na kusababisha ajali. Au wapi panakikwazo?
 
Ajali sasa imekuwa jambo la kawaida hapa tanzania. Watu wengi wanapoteaza maisha kwa sababu ya uzembe wa madereva ambao wanaendesha magari kwa spidi zilizopitiliza. Cha ajabu na cha kusikitisha Askari wa usalama Barabarani wako wengi sana njiani lkn haionyeshi kuwa suluhu ya kuzuia ajali. kipindi cha nyuma utafiti ulifanyika na kugundulika kuwa sababu moja wapo zinazosababisha ajali kwa wingi ni aina ya mabasi yanayotumika hayafai kwa matumizi ya kusafrisha abiria. Sababu kubwa ya kutofaa ni kwamba mabasi mengi ni ya magari ambayo yalitengenezwa kwa ajili ya mizigo lkn watu wakaziundia bodi na kufanya mabasi ya abiria. Sasa inashangaza sana kwa sababu serikali iliwahi kukataza na kutoa mda kwa wale wote ambao magari yao hayafai kwa sababu ni muundo wa malori lakini sijui serikali iliishia wapi na watu wanaendelea kupoteza maisha. Mimi najiuliza ni kwa nini hii serikali inashindwa kusimamia sheria inayoyojiwekea yenyewe?. Sasa watanzania tumechoshwa kila siku kusikia ajali.
 
Twaweza kuilaumu serikali ndio,lakini na watanzania kama abaria mara nyingi huwa hawafanyi sehemu yao,
Mfano: kwa uzoefu wangu wa kusafiri muda mrefu nimegundua kwamba abiria wengi huwa hawapendi kuona basi lao linapitwa na mabasi mengine.
Kama hiyo haitoshi kuna namba wakati mwingine zimo ndani ya mabasi kwa ajili ya kutoa taarifa pindi waonapo dereva anaenda ndivyo sivyo lakini hakuna hata mmoja anaesema chochote,
Na zaidi ni kwamba ukionekana kumzuia dereva kuendesha kwa spidi kali unaonekana MNOKO.
 
Serikali inahitaj umakn san wa hali ya juu,kupunguza hiz ajar japo ajari inatokea mda wwte ule paspo jua
 
Wanajamii tumekua tukijadili mambo mengi Jukwaani , mingi ya mijadala husika inagusa masuala ya kusiasa! Binafc naumizwa sana kusikia ajali za barabarani kila kukicha! Ukweli ukiona majeruhi, maiti zitokanazo na ajali zinatisha, majeruhi wanatisha!
Wakati watu wanapoteza maisha kila iitwapo leo, wanasiasa wametuweka busy kujadili siasa tu!
Ni ombi langu leo kuomba Wanajamvi, tujadili nini kifanyike kupunguza ama kuondoa kabisa tatizo la ajali, mjadala wetu uzingatie wadau wote wanaohusika na usafiri wa barabarani tu; Sumatra, Traffic pamoja na abiria! Nini kifanyike ili kuondoa tatizo hili?
Ni imani yangu ajali hizi zinaepukika kila mdau akiwajibika kwa nafasi yake! Karibu!
 
overhauling kubwa ya jeshi la polisi na trafiki inahitajika, rushwa ni tatizo sugu, vijana wadogo wana leseni lakini hawafahamu hata mlango wa chuo hata kimoja cha udereva
 
Back
Top Bottom