Ajali Panda Mbili:Basi la Taqwa lapinduka, laungua, maafa makubwa!

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,466
113,548
Nimeona TBC News usiku huu, kumetokea ajali nyingine ya basi la abiria katika kijiji cha Pandambili, Dodoma, ni basi la Taqwa lililokuwa likielekea Bujumbura, limepinduka na limeteketea kwa moto, Watu wengi wamepoteza maisha akiwemo dereva wa gari hilo.

TBC ilionyesha live basi likiungua na fire zikifika wakati basi limeishateketea.

Pia leo nimeshuhudia efective reporting ya vyombo vyetu vya habari, kuleta live kwa maana haswa ya live kama kwenye CNN.

Ni Pandambili ndipo palipotokea ajali iliyokatisha maisha ya Mbunge wa Tarime, Chacha Wangwe.

Mlioko Dodoma naomba tupatieni more update..

Kwa mujibu wa Blog ya Likwengule inayomilikiwa na Beda Msimbe taarifa ndio hii

Mtu mmoja amefariki dunia na wengine kupata majeraha baada ya basi walilokuwa wakisafiria kuelekea Bujumbura wakitokea Dar es salaam kupinduka,kushika moto na kuteketea katika eneo la Tanana, Kongwa mkoani Dodoma.
Taarifa kutoka eneo la ajali zinadai kuwa basi hilo lilipinduka kwanza kabla ya kushika moto na kuteketea.Mtu aliyefariki katika ajali hiyo ametambuliwa kuwa ni dereva wa basi.
Majira ya alasiri baada ya moto kuzimwa juhudi zilikuwa zinafanyika kulinyanyua ili kuweza kutambua idadi halisi ya maisha yaliyopotea.
Basi hilo la Taqwa lilipata ajali majira ya mchana na hakuna uhakika wa mali zilizoweza kuokolewa.

Mod, rekebisha headline, siyo breaking news tena, kumbe ajali imetokea asubuhi, mimi nimeiona TBC breaking news usiku huu nikafikiri ndio saa hizi kumbe ni recorded.
Mpaka sasa comfirmed dead ni wawili, dereva na mtoto mdogo mmoja.

Mungu awafaruji wafiwa, na uponyaji wa haraka kwa majeruhi.
 
Nimeipata hii toka Blog ya Likwengule

Kamanda wa polisi mkoani Dodoma Zelothe Stephen (pichani) amesema kuwa mpaka sasa ni vigumu kutambua idadi kamili ya watu waliokufa kutokana na ajali ya basi la Taqwa ambalo lilipinduka na kuungua leo asubuhi.
Stephen alisema kuwa wanashindwa kutambua idadi kamili ya watu waliokufa kutokana na gari hilo kutekeatea na kuwa upelelezi unaendelea ili kujua idadi ya watu waliokufa.
Licha ya basi hilo kuwa na uwezo wa kubeba abiria zaidi ya 60 utingo wa basi hilo Mohamed Shaban alisema kuwa gari hilo lilikuwa na abiria 40 ambapo kati yao 35 walipandia Jijini Dar es Salaam na wengine watano walipandia Morogoro.
Gari la zima moto kutoka Dodoma lilifika katika eneo la ajali, basi hilo likiwa linaishia majira ya saa nane mchana na wakaishia kuzima cheche zilizobaki.
Kaimu Mganga mkuu wa Hospitali kuu ya Mkoa wa Dodoma Jacob Chembele alisema kuwa alipokea jumla ya majeruhi 18 mnamo majira ya saa 8mchana ambapo kati yao 15 walitibiwa na kuruhusiwa na wengine watatu bado wamelazwa kutokana na hali zao kutokuwa nzuri.
Dk Chembele aliwataja majeruhi waliolazwa wakiwemo raia wawili wa nchini Rwanda kuwa ni Fatuma Safari (30),Uwitonze Marie( 36)na mkazi wa Wilaya ya Manyoni Anna Francis (18)wote wamelazwa wodi namba 10 katika hospitali hiyo kuu ya Mkoa wa Dodoma.
Kaimu mganga mkuu huyo alisema kuwa majeruhi wengine watano wamepelekwa katika zahanati ya Wilaya ya Kongwa ambapo walitibiwa na kuruhusiwa ila wanatarajiwa kupelekwa katika hospitali hiyo ya Mkoa kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi zaidi.
BASI la Taqwa linalofanya safari zake kutoka Dar es Salaam kwenda nchini Rwanda limepinduka na kuwaka moto na katika eneo la Pandambili huku idadi ya watu waliokufa katika ajali hiyo kutofahamika na wengine 23 kujeruhiwa vibaya.
Licha ya idadi ya watu waliokufa mpaka sasa kutofahamika ni maiti mbili tu ndizo zilizopatikana ikiwemo maiti moja inayodhaniwa kuwa na dereva wa basi hilo Hasimu Abd (34), na maiti ya mtoto mdogo ambaye hajajulikana umri wake wala jina.
Basi hilo aina ya Scania lenye namba za usajili T 985 ARK lililokuwa lina toka Dar es saalam kwenda Kigali Rwanda (awali niliandika ni Bujumbura)limepinduka katika eneo la Pandambili wilayani Kongwa mjini hapa.
Tukio hilo limetokea leo saa 5 asubuhi baada ya basi hilo kuacha njia na kupinduka na baadaye kuwaka moto wakati likijaribu kulipita lori lililokuwa mbele ya barabara hiyo.
 
Hii ni taarifa ya Msimbe, Mzee wa Likwengule kwenye blog yake

Ajali ya basi la Taqwa limebakisha mifupa mitupu huku ikiwa vigumu kujua idadi ya watu waliokuwa ndani ya basi hilo .
Kwa mujibu wa taarifa za hadohado zilizopatikana kutoka kwa mdau wa blogu hii watu waliotoka wakiwa majeruhi ni 23 katika basi ambalo inadaiwa kuwa na abiria zaidi ya 40.
Mdau amesema kwamba ni vigumu kuelezwa mifupa iliyokuwapo humo na hivyo kazi hiyo kubaki zaidi kwa utambuzi wamadaktari.
Taarifa zaidi kutoka Dodoma mjini zinasema kwamba watu waliotoka bila majeraha ni 21, huku 23 wakiwa wamejeruhiwa na mtu aliyekufa ni mmoja.
Basi hilo lililokuwa likisafiri kuelekea Bujumbura lilitokea Dar es salaam.
Imeelezwa kuwa basi hilo lilipinduka,kushika moto na kuteketea katika eneo la Tanana, Kongwa mkoani Dodoma.
Idadi kamili ya abiria waliokuwa katika basi hilo hadi jana jioni haikuwa inajulikana kwani Taqwa walikuwa hawajatoa chati polisi.
 
Mod, rekebisha headline, siyo breaking news tena, kumbe ajali imetokea asubuhi, mimi nimeiona TBC breaking news usiku huu nikafikiri ndio saa hizi kumbe ni recorded.
Mpaka sasa comfirmed dead ni wawili, dereva na mtoto mdogo mmoja.

Mungu awafaruji wafiwa, na uponyaji wa haraka kwa majeruhi.
 
Uzoefu unaonyesha kwamba ajali nyingi sana hutokea kipindi cha kuelekea mwisho wa mwaka. Kuna mtaalamu mmoja aliwahi kugusia kwamba shamrashamra za sikukuu zina madhara fulani kisaikolojia kwa watu. Sijui ukweli kuhusu hili ukoje.

Poleni sana kwa wale waliofiwa na poleni sana kwa wale waliojeruhiwa. Madereva (meaning all divers and not just bus drivers) kuweni makini sana kipindi hiki tunapoelekea mwisho wa mwaka.
 
Back
Top Bottom