Mie na mmbongo mwenzangu tuko mji mmoja hapa Ghuba, shughuli yetu ni 'maboxi'. Tunaishi kwenye shared apartment, tupo wabongo 2, mhindi na mhabeshi.
Mwenzangu jana kapata 'ajali'. Hawa housemate wetu wanakula sana pilipili na ukali wake hauna kifani! Hata sie tumeizoea kwa kiasi fulani.
Jana jioni, jamaa yangu alikuwa zamu jikoni na wakati anakatakata viungo, akatoka mara moja kwenda haja ndogo nahuko katika kujisaidia akijishika sehemu-sehemu na ndipo balaa likamkuta! Basi pilipili zimemwasha akawa analia kama mtoto mdogo, jana chakula cha jioni hakula, alijaribu kuoga maji mengi haikusaidia, amejifungia chumbani kalala mtupu, amewasha feni na ac lakini nafuu haikupatikana.
Leo huku ni mwisho wa wiki na kazi ni nusu siku lakini jamaa mzigoni hakutokea.
Naomba ushauri kwa haya yafuatayo:
1. Huduma ya kwanza: ukipatwa na ajali kama hii, unafanyaje? sitashangaa na mie yakanifika!
2. Matibabu: Je, inawezekana kuwa atakuwa amepata madhara kiafya na kama ni hivyo yapo matibabu yake?
3. Insurance: Je, watu wa bima wana policy inyohusu ajali kama hizi? maanake mtu unaweza kupoteza kiungo muhimu maishani mwako!
NAWASILISHA.
Mwenzangu jana kapata 'ajali'. Hawa housemate wetu wanakula sana pilipili na ukali wake hauna kifani! Hata sie tumeizoea kwa kiasi fulani.
Jana jioni, jamaa yangu alikuwa zamu jikoni na wakati anakatakata viungo, akatoka mara moja kwenda haja ndogo nahuko katika kujisaidia akijishika sehemu-sehemu na ndipo balaa likamkuta! Basi pilipili zimemwasha akawa analia kama mtoto mdogo, jana chakula cha jioni hakula, alijaribu kuoga maji mengi haikusaidia, amejifungia chumbani kalala mtupu, amewasha feni na ac lakini nafuu haikupatikana.
Leo huku ni mwisho wa wiki na kazi ni nusu siku lakini jamaa mzigoni hakutokea.
Naomba ushauri kwa haya yafuatayo:
1. Huduma ya kwanza: ukipatwa na ajali kama hii, unafanyaje? sitashangaa na mie yakanifika!
2. Matibabu: Je, inawezekana kuwa atakuwa amepata madhara kiafya na kama ni hivyo yapo matibabu yake?
3. Insurance: Je, watu wa bima wana policy inyohusu ajali kama hizi? maanake mtu unaweza kupoteza kiungo muhimu maishani mwako!
NAWASILISHA.