Ajali ilivyokuwa same

Yona F. Maro

R I P
Nov 2, 2006
4,202
218
Leo Kwa mara ya kwanza nimebahatika kukutwa na ajali ya basi lakini dereva alifanikiwa kukwepa gari ya mbele na kuingiza gari porini baadaye wakalitoa na tukaendelea na safari kama kawaida

Nashukuru kwamba nimefika salama mkoani arusha , Dereva aliyekuwa anaendesha basi letu alikuwa anakunywa maji ndio ghafla akakutana na gari lingine la mizigo lilitokuwa limebeba nguzo za tanesco , Eneo lile ni eneo lenye upepo sana pamoja na kona kona , watu wengi wanaopita pale huwa wanashauriwa kupunguza mwendo kwa sababu hizo dereva wetu hakupunguza mwendo aliendelea ndio ghafla kwenye kona kukawa na gari hilo akaamua kuingiza gari porini .

Ingawa abiria wengi sana walitaka kushuka kwenye gari kwenda kumpiga dereva mwenye hiyo gari ya mizigo lakini baadaye gari liliondoka ndio baadaye sasa tukawa tunaangalia jinsi dereva anavyoendesha karibu ye hedaru kukawa na gari lingine la mizigo kama lile lile akaendelea kunywa maji yake pamoja na kupiga story na baadhi ya watu waliokuwa pale mbele napo akataka kufanya vituko ndio lawama sasa zikaanza kushushiwa upande wake .

Baada ya hapo kuna Sehemu nyingine ukitoka kwenye daraja kabla ya kufika kwa saddala kuna mlima pale na kona , alijaribu kupita gari zingine 3 coaster zenye abiria waliokuwa wanakuja arusha watu wakampigia kelele lakini hakusikia

Angalau tumefika salama namba za gari hilo ni 3644 Happy Nation la saa 12 nimejaribu kumpigia mwenye namba ambayo imeandikwa kwenye tiketi ambayo ni 0754 668389 Lakini haipatikani pamoja na yote hata hawakuandika majina ya abiria ambao walikuwemo ndani ya gari lao .

Natakiwa kwenda kufanya shuguli zingine sasa , Jioni Njema
 
Pole mzee....inaonekana huyo dereva ni muhuni tena wakijiweni! Shukuruni kwa kuwa mmefika salama at the end!
 
Pole sana aisee, ila kheri mmefika salama japo kwa mashaka mashaka.

Nchini kwetu kuna aina kama bili hivi ya wafanya biashara (kusafirisha abiria):-
1. Kuna wale wanaofanya biashara hiyo kwa utaalam (namaanisha professionally). Hawa hata staff wao huwa naona wana maadili na wanaheshimu kazi zao. Mfano wanavaa na kuongea vizuri na hivyo kumfanya abiria kufurahia safari na kutamani wakati mwingine huduma yao.

2. Kundi la pili ni wale wanaofanya biashara ya mazoea (kibabaishaji), mabasi yao ni yale yale ya zamani yenye viwango vya chini (ya kuunga unga). Lakini kibaya zaidi ni huduma zitolewazo ndani ya hayo mabasi, mfano abiria ukifika unagombaniwa ka mpira wa kona, wafanyakazi ni wengi sana (maarufu kama mashanta ambao huambatana na basi na kwa mda mchache tu baada ya safari kuanza hushushwa baada ya kupata malipo yao). Haitoshi, wafanyakazi wao wengi hawana utu kabisa, midomo yao ni michafu na pia hawaeheshimu kazi zao. Usishangae kukuta kuku na watu wengine kwenye vigoda...kazi ipo.
 
Mkuu shy yaani huoni haya kusema "nimebahatika"? we kukutana na ajali unaona bahati la haula la kwata
 
hawa madereva wetu ni wa ajabu sana.i remember kuna drive wa champioin aliuwa watu 23 kabla ya mlandizi kwa mtindo huo huo yeye alikuwa anasome meseji kwenye simu kuja kustuka mbele kula roli la mafuta akalivaa na ikawa mwisho wa maisha ya watu 23...it was 2006..pole mkuu na hongera kwa kufika salama Arusha
 
hawa madereva wetu ni wa ajabu sana.i remember kuna drive wa champioin aliuwa watu 23 kabla ya mlandizi kwa mtindo huo huo yeye alikuwa anasome meseji kwenye simu kuja kustuka mbele kula roli la mafuta akalivaa na ikawa mwisho wa maisha ya watu 23...it was 2006..pole mkuu na hongera kwa kufika salama Arusha

Pole na hiyo misukosuko na hongera kwa kufika salama inabidi uende pale Mrina kuna vipozeo flani ukajipongeze.
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom