AJABU: Chenge aitetea DOWANS ilipwe!

Hongera chenge, Bravo Fisadi masterminder,
Waonyeshe njia, watanabaishe kuwa hii nchni haina dola wala kiongozi yoyote anayeweza kuwazuia nyie kufanya lolote mnalotaka.

Wadhiirishie kuwa kelele za chura (Nape) hazimzui mgombe kunywa maji (Fisadi hatetereki).
Waambie kwa vitendo kuwa hakuna aliye juu yenu hapa katika ardhi ya Tanzania, waambie hao wasiokujueni kuwa hata raia hawawezi ni mwenzenu.

Kazi nzuri sana chenge Bravo! Kwani ulipowaambi wewe unavijinti kwani si walibisha! Mbona walipojua ya EPA, Meremeta na Dowans walikubali kuwa zako kweli vijisenti!
 
Nakumbuka Bunge lililopita, Mbunge mpya kwa tiketi ya cdm, Tundu Lissu, alipokuwa anajitafutia umaarufu Bungeni kwa kufanya u"tundu" na kuzua malumbano kwa kila hoja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, alisimama Chenge na kumpa Tundu hoja moja tuu ya kisheria ambayo ilimfanya Tundu kuwacha utundu wake wa kulumbana, kwani kwa pale ilidhihirika wazi kuwa Tundu ni katoto kwa Chenge kisheria. Nani anaekumbuka?

Kwa mantiki hiyo, ikiwa Chenge kasema fedha ya Dowans walipwe, basi ujuwe kaiona sheria kwa jicho la wazi na anajuwa kutokuwalipa Dowans kunaweza kuleta utata zaidi na kuliingiza Taifa kwenye utata zaidi, Jee, inawezekana kuwa hata Symbion hawatakubali kulipia mitambo ambayo bado ina deni?
Kwa maelezo yako ni kama unataka kutuambia kwamba Chenge anajua sheria sana siyo?Inawezekana anaijua sheria lakini kujua kwake sheria hakujaisaidia hii nchi.Serikali iliingia kwenye mikataba mibovu ya madini Chenge akiwa mwanasheria mkuu je wwakati huo alikua haijui hiyo sheria?au aliijua ila alikua ana masilahi binafsi?na kama niko sahihi basi hata sasa inawezekana ana masilahi binafsi kwenye hili suala la Dowans.Hoja si kujua sheria tu,na hiyo sheria unaiyumia vipi kwa masilahi ya Taifa!
 
Hawa jamaa hawana huruma kwakweli.

Moja ya sababu ya umaskini wa watanzania ni kuwa wanawaonea huruma mafisadi wanaosababisha uchumi wao uzorote wakati wenyewe hawaionei huruma nchi. Ili nchi yetu iendelee ni lazima viongozi wetu waache kuchekacheka na kuwaadhibu wahalifu kwa mujibu wa sheria zetu hata ikibidi zibadishwe. Nchi ya China kwa mfano imepata maendeleo yake kwa kasi kwasababu hawawaonei huruma mafisadi na ndio maana wakipatikana hupewa hukumu ya kifo; hata hapa karibu kwetu Africa, nchi ya Ghana ilipokombolewa na Lt. Rawlings kitu cha kwanza alichofanya ni kuwanyonga mafisadi wakina Achempong na genge lake na ndio maana tunaona hali ya uchumi ya Ghana imekua kwa kasi kubwa!!! Tusipochukua hatua madhubuti dhidi ya ufisadi kila siku tutakuwa watu wakulalamika kuwa hatujui chanzo cha umaskini wa nchi yetu.
 
Kiongozi umeongea point sana, haina maana kuwasamehe hawa jamaa wa migodi kodi kwenye mafuta, yaani Madini wanachimba kwa manufaa ya nchi zao na familia zao na vizazi vyao halafu sisi tunawasamehe Kodi ambayo ingechangia kuboresha maisha ya wananchi wetu,
Hivi yupi bora! Mwananchi au mwekezaji? sasa kwa nini unaweka kodi kwenye mafuta anayotumia mwananchi halafu unamsamehe mwizi wa raslimali za nchi yetu? jamani mtanzania wa leo analipa kodi kibao na nzito na hii ni kwa ubinafsi wa viongozi wa ccm.

ifikie wakati watanzania tuache unafiki tuuone ukweli huu usani wa kuchezeana na huku maisha yanakwenda, fanya mabadiliko sasa na usingoje kesho maana wewe leo una let’s say 30 or 50 or 60 years miaka 5 ijayo utakuwa umesogelea kaburi na huu usani utaendelea ni lini utaishi katika nchi nzuri uliyopewa na Mungu wako! hawa jamaa wachache wanaishi maisha na wanataengeneza maisha ya jamii zao, watoto wao wajukuu na hata vitukuu, je sisi wabongo wa kawaida hatuhitaji kuwacha watoto wetu wakiwa na maisha ya uhakika? angali watoto wote wa Vigogo wanasomea hapa kwetu? unafikiri ni kwa nini wapo USA, UK na kwingineko ni kwa sababu ya wizi na dhuluma ya baba zao, sisemi kwamba ni wote! wapo waliotafuta wao wenyewe lakini wengi wao ni ufisadi wa wazazi wao ndio umewafikisha hapo na ndio huwa wanawacheka wananchi wasumbukao kitaa.

Ndugu zangu tufumbuke macho, kuna Mchungaji mmoja aliwahi kusema saa ya ukombozi ni sasa na walio wengi walimponda lakini kadri siku zinavyozidi ushuhuda wake unazidi kujizihirisha.

Acha unafiki mtanzania na sasa uchukue hatua. Asilimia 60 ya wabunge wa ccm hawapaswi kurudi bungeni 2015 hamasisha watu wawabwage na ndipo tutapata ukombozi, jamani kwa kila mtu anayependa mabadiliko ya kweli hamasisha katika wilaya yako unakotoka, ili next Bunge Chadema iwe na wabunge walau kuanzia 55% na ndipo utaona nchi itakavyobadilika.

mkuu nakuunga mkono asilimia 100.. wote tukifuata ushauri wako tutalikomboa taifa letu
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Uamuzi aliouchukua Mbunge wa Bariadi Magharibi (CCM), Andrew Chenge (Mzee wa vijisenti/'Mr. Clean) wa kuongeza nguvu Dowans kwa kutoa ushauri wa kisheria ili ilipwe bilioni 94 na Tanesco=Tanzania, unadhihirisha jinsi alivyoumizwa na uamuzi wa chama chake CCM wa kuvuliwa gamba na sasa ameamua kuwasaidia Dowans ili Tanzania ilipe mabilioni ya fedha. Ikumbukwe huyu jamaa alikuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali na amesaini mikataba mingi na huenda alishirikishwa kwa kuomba ushauri katika suala la Dowans lakini leo ameamua kuvuaa miwani ya mbao na kuitetea.
 
Mbunge wa Bariadi pamoja na tuhuma nzito zinazo onyesha negative atitude kwa WATZ kama vile tuhuma dhidi ya rada, kumiliki mabilion ya fedha nje ya nchi, kutia mkono wa kumuondoa spika SITTA aliye pendwa na WATZ wengi kuwa spika wa Bunge Leo napata habari mbaya kwetu kuwa CHENGE amepeleka ushauri mzito wa kisheria ili DOWANS walipwe sh. 94 bil. (source GAZETI LA NIPASHE) CHENGE kama kuna kosa WATZ wamekufanyia basi wasamehe bure !!!! Mbona wao awnakupenda wamekupa ubunge (kama hukuchakachua) kuonyesha wanakupenda tusamehe tu hata kama una mgawo DOWANS

ENYI WANA WA TAMAA! Wekeni mbali vazi la majivuno na mjivue vazi la ufedhuli.ewe asili halisi ya shauku! Weka mbali tama na tafuteni kuridhika kwa maana mwenye tamaa daima amenyimwa, na mwenye kuridhika daima amependwa na kusifiwa na mngu
 
U wapi uzalendo wa viongozi kwa Taifa lao.,bila hata aibu unaisaidia kampuni 'inayoidai' serikali unayoitumikia ili iweje?.Nilitegemea angesaidia serikali na nchi yake isiingie au jinsi ya kujitoa katika katika migogoro ya kisheria...

Nani kakwambia kuwa nchi hii ina viongozi wazalendo?Huoni jinsi mambo yanavyokwenda, wachimbaji wadogo wakijigundulia madini na kuanza kujitafutia riziki kesho yake viongozi wako hao unaowaita wazalendo wanawaita wawekezeji uchwara na kuwatimua wananchi.
 
Bongolala, wakati nasubiri kulisoma hilo Nipashe, ningependa kusisitiza mahitaji ya kisheria na mahitaji halisi ni vitu viwili tofauti. Mahitaji ya kisheria ni laz`ima yatekelezwe no matter what, hata kama sio mahitaji halisi.

Tozo la Dowans lililotolewa na ICC ni hitaji la kisheria, kwa mujibu wa mkataba husika, uamuzi wa ICC ni uamuzi wa mwisho, haupingiwi na mahakama yoyote labda kufanyiwa mapitio na ICC yenyewe, hivyo kitendo cha kuusajili mahakama za nchini, ni kwa lengo la kuusajili uamuzi ule kwa utekelezaji tuu.

Siungi mkono tozo hiyo ya ICC kwasababu sio tozo halali, ila kisheria, maadamu wanasheria vichwa maji wetu waliukubali ule mkataba, na hivyo ndivyo mkataba unavyosema, then tozo hiyo imehalalishwa na mkataba mbovu ule, hivyo toso ile ni halali kisheria.

Nawaombeni wana jf na wananchi wote wa Tanzania, lazima tuukubali ukweli mchungu kwa kumeza kidonge kichungu cha tozo hii, tutatake tusitake, lazima tutalipa tuu, hatuna popote pa kutokea unless Tanzania kama nchi, tujitoe ICC na kuwafukuzia mbali hawa wanyonyaji wote wanaojiita wawekezaji wa kwendo makao n a mitaji yao, wakatumie fedha zao kutengeneza madini yao na sisi watuachie almasi zetu, Wasukuma tuzichezee bao, na dhahabu zetu tuziache humo humo ardhini, tubaki na umasikini wetu huku tumekalia malia zetu, kuliko kuwaruhusu wazipore kubadilishana na pipi huku wakituacha na umasini wetu palepale.

Mkuu umenena vyema. Chenge kama mwanasheria ana haki ya kufanya hivyo. Tatizo ni hao walioingia mkataba huo ambao pamoja na wanasheria wao. Pia kuna wanasheria walioshauri mkataba uvunjwe na kisha wanasema ni haki tozo ilipwe. Tuasiangalie tulioangukia, tuangalie tulipojikwaa.
 
Mbunge wa Bariadi pamoja na tuhuma nzito zinazo onyesha negative atitude kwa WATZ kama vile tuhuma dhidi ya rada, kumiliki mabilion ya fedha nje ya nchi, kutia mkono wa kumuondoa spika SITTA aliye pendwa na WATZ wengi kuwa spika wa Bunge Leo napata habari mbaya kwetu kuwa CHENGE amepeleka ushauri mzito wa kisheria ili DOWANS walipwe sh. 94 bil. (source GAZETI LA NIPASHE) CHENGE kama kuna kosa WATZ wamekufanyia basi wasamehe bure !!!! Mbona wao awnakupenda wamekupa ubunge (kama hukuchakachua) kuonyesha wanakupenda tusamehe tu hata kama una mgawo DOWANS


malalamiko menngi ya nini? ukilalamika unapata faida gani??

Kwani si yote haya kila mtu anayaona listen my friend everybody for himself but God for us all
 
Awali nilidhani upo humu kutetea CCM na mafisadi kumbe I was wrong. Wewe upo si kwa ajili ya CCM ila kwa ajili ya JK na udini.
Hilo nimelinusa. Hata hivyo wenye fikra pevu wanakudharau.
Mkuu kumbe ulikuwa haulijui hilo? wenzio tulishamshitukia kitaaaambo
huyo ni mdini sana alafu ni mchawi
 
Chenge anaweza kuwa ni mjuvi wa sheria anayoitumia kwa maslahi yake binafsi na ndiyo maana 'mtaalamu mzanzibar' J Shamhuna alimtolea uvivu pale alipojidai kupindisha vifungu ilhali akijua kabisa kuwa wazenji wanatambua kuwa znz ni nchi.
 
Uamuzi aliouchukua Mbunge wa Bariadi Magharibi (CCM), Andrew Chenge (Mzee wa vijisenti/'Mr. Clean) wa kuongeza nguvu Dowans kwa kutoa ushauri wa kisheria ili ilipwe bilioni 94 na Tanesco=Tanzania, unadhihirisha jinsi alivyoumizwa na uamuzi wa chama chake CCM wa kuvuliwa gamba na sasa ameamua kuwasaidia Dowans ili Tanzania ilipe mabilioni ya fedha. Ikumbukwe huyu jamaa alikuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali na amesaini mikataba mingi na huenda alishirikishwa kwa kuomba ushauri katika suala la Dowans lakini leo ameamua kuvuaa miwani ya mbao na kuitetea.


so unataka tufanyeje embu sometimes tuwe tunaongea vitu vya msingi vinavyo tupleka kwenye solution ya hilo jambo sio malalamiko tuuuuu
 
Mwizi mkubwa huyu na alipokuwa AG alitumia elimu kuibia watanzania kwa kusaini mikataka ya kifisadi na sasa anaendeleza ufisadi
 
Nakumbuka Bunge lililopita, Mbunge mpya kwa tiketi ya cdm, Tundu Lissu, alipokuwa anajitafutia umaarufu Bungeni kwa kufanya u"tundu" na kuzua malumbano kwa kila hoja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, alisimama Chenge na kumpa Tundu hoja moja tuu ya kisheria ambayo ilimfanya Tundu kuwacha utundu wake wa kulumbana, kwani kwa pale ilidhihirika wazi kuwa Tundu ni katoto kwa Chenge kisheria. Nani anaekumbuka?

Kwa mantiki hiyo, ikiwa Chenge kasema fedha ya Dowans walipwe, basi ujuwe kaiona sheria kwa jicho la wazi na anajuwa kutokuwalipa Dowans kunaweza kuleta utata zaidi na kuliingiza Taifa kwenye utata zaidi, Jee, inawezekana kuwa hata Symbion hawatakubali kulipia mitambo ambayo bado ina deni?

Tatizo ni kwamba Sehemu ambayo akili inapaswa kuingilia Umeifunika. Nenda kavue huo ujinga kwanza ndipo ubongo wako ufunguke na kuchangia points zenye akili. Nyau we!!
 
Mbunge wa Bariadi pamoja na tuhuma nzito zinazo onyesha negative atitude kwa WATZ kama vile tuhuma dhidi ya rada, kumiliki mabilion ya fedha nje ya nchi, kutia mkono wa kumuondoa spika SITTA aliye pendwa na WATZ wengi kuwa spika wa Bunge Leo napata habari mbaya kwetu kuwa CHENGE amepeleka ushauri mzito wa kisheria ili DOWANS walipwe sh. 94 bil. (source GAZETI LA NIPASHE) CHENGE kama kuna kosa WATZ wamekufanyia basi wasamehe bure !!!! Mbona wao awnakupenda wamekupa ubunge (kama hukuchakachua) kuonyesha wanakupenda tusamehe tu hata kama una mgawo DOWANS


Kuna jopo la wanasheria wa CCM waliojitolea kuitetea Serikali ndidi ya mzigo huu wakiongozwa na Mh. Nimrodi Mkono; ina maana Mh. Chenge hakuwa mmoja wa hilo jopo?
 
ENYI WANA WA TAMAA! Wekeni mbali vazi la majivuno na mjivue vazi la ufedhuli.ewe asili halisi ya shauku! Weka mbali tama na tafuteni kuridhika kwa maana mwenye tamaa daima amenyimwa, na mwenye kuridhika daima amependwa na kusifiwa na mngu


Asee hili andiko nimelipenda liko kwenye kitabu gani?
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom