kalamuzuvendi
Member
- Nov 19, 2010
- 65
- 3
Nanukuu sehemu hii ya Hotuba aliyotoa JK ya mwaka Mpya.
Najua wapo baadhi ya wanasiasa na vyama vya siasa ambavyo vimepanga mikakati ya kuendeleza malumbano yauchaguzi na kutaka Watanzania waishi kama vile nchi ipo kwenye kampeni za uchaguzi.Wamepanga wakati wote kutafuta jambo au hata kuzua jambo ili kuwachochea wananchi waichukie Serikali. Wamepanga kuchochea migomo vyuoni na maandamano ya wananchi mara kwamara. Kwao wao huo ndiyo mkakati wa kujijenga kisiasa ilikujiandalia ushindi kwenye uchaguzi wa mwaka 2015.
Nawatanabaisha ndugu zangu myajue hayo ili msipoteze mudawenu muhimu wa kujiendeleza na kugeuzwa kuwa mbuzi wa kafara kwa ajili ya kuendeleza maslahi ya kisiasa ya watu fulani. Kwa jinsi watu hao walivyokuwa wabinafsi na wasivyokuwa na huruma na wenzao, wako tayari kuchochea ghasia bila kujali madharayatakayo wakuta watu watakaoshiriki. Wao hasa wanachotaka nighasia kutokea na vyombo vya dola kuingilia ati waiambie jumuiyaya kimataifa jinsi Serikali yetu ilivyo katili. Nawasihi ndugu zangu msiwasikilize wala kuwafuata wanasiasa hawa.Nawaomba, wakiwafuata wakumbusheni kuwa wao wanazo fursanyingi za kusema wayatakayo Bungeni na kwingineko, waachekuwatumia kama chambo au wahanga wa maslahi yao.
Mwisho wa Kumnukuu.
Najua wapo baadhi ya wanasiasa na vyama vya siasa ambavyo vimepanga mikakati ya kuendeleza malumbano yauchaguzi na kutaka Watanzania waishi kama vile nchi ipo kwenye kampeni za uchaguzi.Wamepanga wakati wote kutafuta jambo au hata kuzua jambo ili kuwachochea wananchi waichukie Serikali. Wamepanga kuchochea migomo vyuoni na maandamano ya wananchi mara kwamara. Kwao wao huo ndiyo mkakati wa kujijenga kisiasa ilikujiandalia ushindi kwenye uchaguzi wa mwaka 2015.
Nawatanabaisha ndugu zangu myajue hayo ili msipoteze mudawenu muhimu wa kujiendeleza na kugeuzwa kuwa mbuzi wa kafara kwa ajili ya kuendeleza maslahi ya kisiasa ya watu fulani. Kwa jinsi watu hao walivyokuwa wabinafsi na wasivyokuwa na huruma na wenzao, wako tayari kuchochea ghasia bila kujali madharayatakayo wakuta watu watakaoshiriki. Wao hasa wanachotaka nighasia kutokea na vyombo vya dola kuingilia ati waiambie jumuiyaya kimataifa jinsi Serikali yetu ilivyo katili. Nawasihi ndugu zangu msiwasikilize wala kuwafuata wanasiasa hawa.Nawaomba, wakiwafuata wakumbusheni kuwa wao wanazo fursanyingi za kusema wayatakayo Bungeni na kwingineko, waachekuwatumia kama chambo au wahanga wa maslahi yao.
Mwisho wa Kumnukuu.