wamepandisha gharama mkuu! Mb 400 sasa ni 500 na beijuu kwa buku5.tazama kwenye menu yao kwa kubofya *154*44# yani baada ya kuona hivyo hadi nguvu ziliniishia kwani kabando kangu fasta kameisha na natakiwa kuongeza tena 4/05/2012.mambo sasa magumu!
Hata kwenye simu wanakata kinoma. Mimi nilishawaacha. Sikuhizi situmii line yao.Ni kwamba wamepandisha gharama za Internet au vipi, mbona inaisha haraka hivi. Sisi tuliokuwa tunajikamua na 2500 kwa 400mb si ndio basi tena!!.
Tuma NENO Internet kwenda namba 15444...
Ila inagoma kuangalia salio. I dont know why?
hata modem zao za bure miezi sita ni utapeli mtupu.walaji tuwawekee airtel mgomo
Mimi kimodem chao nimechoma moto na sasa nimehamia ZANTEL
baada ya muda mfupi utaambiwa imeexpire...yamenikuta jana.
gharama za Zantel zikoje kwani?
Gharama zao ni kama ifuatavyo:
SIKU: 1.Mini(40MB,Tsh.1000)
2.Small(150MB,Tsh.3000)
WIKI: Regular(300MB,Tsh.7000)
Mwezi: 1.Mono(750MB,Tsh.15000)
2.Silver(2GB,Tsh.40000)
3.Gold(5GB,Tsh.90000)
4.Platinum(8GB,Tsh.140000)
Unaruhusiwa ku-subscribe tena muda wowote baada ya kumaliza bundle.
Speed yake ni 3.6mb/s downlink and 1.3mb/s uplink.
Enjoy yourself!