Airtel internate na bonus ni dhulumati namba wani!

MDAU JR

JF-Expert Member
Mar 9, 2011
451
82
Jamani Kuna dhuluma inafanyika airtel internate : ukijiunga na bundle au ukiwa na bonus na huku ukiwa na hela ya ziada kwe modem, ile hela inaliwa yote na kubakia sh 4 ambapo huwezi kupata connection ya net, unalazimika uweke hela nyingine nayo italiwa hadi ibakie sh 4 na net inakata tena ilhali una bundle ama bonus ya mb 200.Hili limenitokea zaidi ya mara tatu na hii yangu ni kali zaidi kwa kuwa ukiachilia mbali hiyo ya bonus ya mb 400 hela yangu iliyokuwamo kwe simu ikaliwa, huwa najiunga na bundle ya wiki ya shs 15000 na hela ya ziada inayokuwemo huw inaliwa pia, wizi ulioje airtel? nimejaribu kuongea na customer care kuhusu hili naishia kupewa namba ya kumbukumbu ya tatizo langu na kuambiwa tatizo linatafutiwa ufumbuzi nitapigiwa simu ("mpendwa mteja, tunashughulikia ombi lako, kumbukumbu no. yako ni 516477 tutawasiliana nawe hivi punde") haya ndo majibu yao hii ilikuwa ni tar 20/04/2011 nyingine ni kumb na 530247 ya tar 25/04/2011, hizi ni baadhi tu ninazo ahadi nyingi nilizoahidiwa kutatuliwa tatizo langu lakini bado nikijiunga na bundle hela yangu ya ziada iliyokuwamo inaliwa. Watanzania wenzetu mlioko kwenye airtel mtusaidie ndg zenu tunadhulumiwa, eneo nililopo napata airtel pekee unless ningekwisha hama zamani. Wewe unayejiita ccrairtel humu JF una msaada gani ktk hili au ni kuweka matangazo tu humu jf ya ku-support dhulumati kwa watanzania wenzio? naomba unisaidie niweze kurudishiwa hela zangu zilizokatwa ilihali zimeshakatwa elfu 15 za bundle ya wiki.
 
Mdau its all about busines.so inabidi uwe makini.kama unatumia internet yao ucku.nakushauri uwe unaweka jero..
 
Hili tatizo hata mimi nimeliona lakini sitalalamika,nilinunua internet ya mwezi sep.2010 sijui walisahaua nikatumia mpaka march.2011 kwahiyo hata wakiniibia kidogo nawapenda.
 
bonus wanayotoa inatumika kuanzia saa sita usiku hadi saa kumi na mbili asubuhi na siku hiyo hiyo, ni uhuni tu au labda ni kwa ajili ya watchmen tu.
 
Lazima utawaona ni wezi tu kwanini unanunua ya wiki kwa sh 15000? kwanini ucnunue ya mwezi kwa sh 2500 ili ikiisha unakuwa una renew au unakuwa una vitu vingi sana vya kudownload? Km hauna vitu vingi mi ningekushauri ununue ya sh 2500 na kama unataka kudown load unafanya hivyo saa sita usiku kwa kutumia bonus yako ya mb 200 nadhani utasave sana pesa na matatizo kama hayo hayatajitokeza tena,huo ndio ushauri wangu kwa kuwa mi i use this thing na imenisaidia sana kuliko mitandao mingine ambayo package zake ziko juu sana.
 
kama una bundle ya wiki kwanini uhangaike na hiyo ya usiku? Cheap is expensive.

Si kwa ucku pekee mkuu, hata mchana una bundle either ya 15000 or 2500 kama kuna hela nyingine wanalamba na ikiisha ile ya ziada net inakata ili hali una tayari bundle ya mb 400 kwa 2500 au whatever, caught me?
 
TCRA AU Tume ya mawasiliano inahusika nao. Mkiwashitaki watawalipa na watajirekebisha. Huwa nao wanaadabishwa.
 
Watumiaji wa Internet na watumiaji wa simu hawana mtetezi nchi hii. Hivi kwa nini hao TCRA wasitoe au kuweka matangazo na namba za simu kwa wananchi kila mahali inapowezekana ili tupate kuwapa taarifa juu ya dhuluma hizi zinazoendelea bila soni? Wangapi tunajua kuwa ni haki yetu kutoa taarifa za ubadhirifu wowote tunaofanyiwa na hawa jamaa? TCRA ni kwa wale walio mijini tu au wasomi peke yao na si mkulima au mwananchi aliye popote TZ hata kama iwe Biharamulo au Nanyumbu? Nchi gani hii ambayo mpaka upate wa kukugusa bega ndo ujuwe mambo iko huku? USIPOPATA WA KUKUGUSA BEGA UJUE UTALIWA MPAKA TONE LA MWISHO LA DAMU. TAASISI HII HAINA MIPANGO YA KUMSAIDIA MTANZANIA WA HALI YA CHINI HASA ALIYE KIJIJINI ILI KWENDA SAMABAMBA NA MABADILIKO YA SAYANSI NA TEKNOLOJIA AMBAYO TUNAHUBIRIWA KILA UCHAO.
 
Tena achilia mbali wizi wa aina hiyo unaomba bundle ya wiki unakatwa 15elfu halafu mtandao unasumbua wiki nzima haufaidi chochote labda tu ufaidi masaa3 kwa wiki nzima. Kama mimi niko porini huwa napata habari live kutoka aljeezra sasa hivi siipati kila nikijaribu naambiwa connection failed
 
Jamani Kuna dhuluma inafanyika airtel internate : ukijiunga na bundle au ukiwa na bonus na huku ukiwa na hela ya ziada kwe modem, ile hela inaliwa yote na kubakia sh 4 ambapo huwezi kupata connection ya net, unalazimika uweke hela nyingine nayo italiwa hadi ibakie sh 4 na net inakata tena ilhali una bundle ama bonus ya mb 200.Hili limenitokea zaidi ya mara tatu na hii yangu ni kali zaidi kwa kuwa ukiachilia mbali hiyo ya bonus ya mb 400 hela yangu iliyokuwamo kwe simu ikaliwa, huwa najiunga na bundle ya wiki ya shs 15000 na hela ya ziada inayokuwemo huw inaliwa pia, wizi ulioje airtel? nimejaribu kuongea na customer care kuhusu hili naishia kupewa namba ya kumbukumbu ya tatizo langu na kuambiwa tatizo linatafutiwa ufumbuzi nitapigiwa simu ("mpendwa mteja, tunashughulikia ombi lako, kumbukumbu no. yako ni 516477 tutawasiliana nawe hivi punde") haya ndo majibu yao hii ilikuwa ni tar 20/04/2011 nyingine ni kumb na 530247 ya tar 25/04/2011, hizi ni baadhi tu ninazo ahadi nyingi nilizoahidiwa kutatuliwa tatizo langu lakini bado nikijiunga na bundle hela yangu ya ziada iliyokuwamo inaliwa. Watanzania wenzetu mlioko kwenye airtel mtusaidie ndg zenu tunadhulumiwa, eneo nililopo napata airtel pekee unless ningekwisha hama zamani. Wewe unayejiita ccrairtel humu JF una msaada gani ktk hili au ni kuweka matangazo tu humu jf ya ku-support dhulumati kwa watanzania wenzio? naomba unisaidie niweze kurudishiwa hela zangu zilizokatwa ilihali zimeshakatwa elfu 15 za bundle ya wiki.

Nadhani wakuu hamjamuelewa mdau. Hilo tatizo kuna mtu mwingine limeshamtokea.

Inakuwa hivi: Unanunua na kuweka voucher, lets say ya shilingi 3000 kwenye simu/modem, automatically unapata bonus ya 200MB ambazo utatumia kuanzia saa 6 usiku. Unaingia kwenye bundle kwa mfano ya sh 2500 unapata 400MB, na kwenye simu inabaki sh 500.

Unaanza kutumia internet, inafika saa 5 na dakika 59 usiku unakuwa umetumia kwa mfano lets say 150MB, katika bundle inakuwa imebaki 250MB. Ikifika saa 6 automatically unahamia kwenye ile bonus ya 200MB. Unatumiaaa ikifika saa 7 unaenda kulala, katika ile bundle ya 200MB ya bonus unaweza ukawa umetumia 80MB.

Tatizo sasa, ikifika asubuhi unakuta balance kwenye simu/modem yako ni sh 4, zile 250MB za balance ulizokuwa nazo kabla ya saa sita usiku hazipo, unabaki kushangaa tu. Jamaa wangu imemtokea mara 2.

Nafikiri kuna coding error kwenye system ya airtel bonus - ningeshauri kutumia bonus ingekuwa optional.
 
Mimi nikishasikia kuna ''offer'' sijui promo au Bonus ya kutumika usiku....najua hao ni wezi tu.....Kwanini usiku?na kwanini isiwe mchana bure,tena jpili kabisa wafanye hizo bonus zitumike mchana kweupe bure.Wanasema usiku wakijua kabisa watu wengi wanakuwa wamelala...Mitandao yote jamani acheni wizi huu.....Tumechoka kabisa.
 
Hata mimi imenitokea several times, hata hiyo 200mb ya offer kuanzia saa 6 ucku haitumiki badala yake unakatwa iliyo katika bundle au salio la kwenye simu.
 
kitengo cha oracle database ni kibovu sio hapo tu ata mitandao mengine wana nyima ajira watu ,wanawapa watoto wao na wanao wajua
 
Wabongo bwn,wakipewa dawa na mganga wa kienyeji kuwa ainywe kuanzia sa7 mpaka 11 usiku tunawaita wachawi,lakini wazungu wakitupa dawa ya mawasiliono/bonus 200Mb tunapiga makofi,kwa nini asitoe izo mchana?mzungu bwana!
 
Back
Top Bottom