Aina za wasukuma na kisukuma

Wanyantuzu walio wengi wana vipato vikubwa, ardhi yao ina samani kubwa. Wamezaliana sana hivyo kuifanya ardhi kuwa kitu cha muhimu sana,nyingi za kaya zao zina mifugo na chakula cha kutosha. Hakuna mnyantuzu utakaemfunga jela kwa faini ya milioni moja mahakamani,lazima atailipa tu, ndo viwango vidogo za faini ktk mifumo yao ya kijadi ktk utoaji wa maamuzi. Wana uchumi mkubwa lakini wanaishi kimasikini sana, tajiri anaemiliki ng'ombe elfu 10 wa kinyantuzu anavaa, kula, kulala, hovyo kuliko utegemeavyo. Vivyohivyo na kwa mwenye semi trailer hata 5. Nilimanisha hivyo, kikubwa ni imani za kishirikina na ukale zaidi. Huku bado wana sheria zote za kijadi, mahakama zao (degashida) polisi wao (wasumbantale) na magereza yao (faini au kutengwa) hakuna anayestafu viboko huku hata uwe wa miaka mia, mahakama ikisema fimbo ni fimbo na hata hawagomi. Kuna mengi ya kushangaza kama wewe hujawahi ishi kwenye mifumo ya kiafrika asilia.
Well said
Mkuu umejitahidi sana kufafanua mila na desturi za Ntunzu perhaps ni mtu wa huko au ni mtu wa kujifunza sana cultural sphere/anthropology za maeneo flani
 
Gawiza...!!

Lugha ya kisukuma ina lahaja kuu nne; ginantuzu, ginang'weli, ginangw'agala na gidakama. Vivyo hivyo, Wasukuma wamegawanyika katika misingi ya lahaja za lugha ya kisukuma.

1.Bhadakama. Hawa wanapatikana sehemu za mji wa Shinyanga, sehemu za Gahama na sehemu za Igunga na Nzega. Kwa idadi, hawa ndiyo Wasukuma wachache sana. Ni watu wenye aibu, wakimya mno... wana muingiliano na utamaduni wa Wanyamwezi. Pengine hawa ndiyo Wasukuma masikini kuliko aina yoyote ya Wasukuma!

2. Bhanang'weli.
Hawa ni Wasukuma wenyeji wa mikoa ya Mwanza, Geita, na kusini - Magharibi mwa Mkoa wa SIMIYU. Kiidadi, hawa ndiyo Wasukuma wengi sana... katika ongea yao, wana matumizi mengi ya 'shi' kwa mfano, shikolo, shiliwa. Pia hawatumii 'ng'wadila' katika salamu za jioni. Wao hutumia 'gawiza' au 'dillo gawiza' Kwa sababu wanaishi katika strategic areas, wana muingiliano na watu wa makabila mbalimbali. Au tuseme wamemezwa na watu wa kuja. Ukienda Geita wenyeji hawaonekani, labda kukimbiza daladala za baiskeli. Mwanza ndiyo usiseme kabisa.

3. Bhanang'wagalla.
Hawa ni Wasukuma wenyeji wa Wilaya za Meatu, Kishapu na Maswa na sehemu za Igunga. Ukikutana nao ni rahisi mno kuwasikia wakisema, 'yombaga bhahebhu', ong'wawiya, kaaa, aghayaa... ni nadra sana kuwasikia wakisalimia, 'ng'wadila' Wao hufupisha, 'dilla mayu' au dilla bhabha. Majina ya maeneo mengi huanza na Ng'wa. Kwa mfano, ng'wabagimu, ng'wajidalala, ng'wanhuzi... Utajiri wao uko kwenye mifugo.
Vijana wa huko hulizika mapema. Kwa mfano, kama mavuno ya matobholwa, karanga, alizeti na pamba ni mazuri, vijana wa maeneo haya hushinda kwenye ngoma za jadi. Hawajui kusaka ridhiki nje ya maeneo yao, utafikiri wako kisiwani. Wanaotoka nje ya maeneo yao ni wafugaji tu. Wanawake wa huko hupenda kuvaa shanga kiunoni na shingoni ingawa sio wajuzi wa mambo ya Tanga. Wavulana nao huvaa miguuni. Soko la wasichana liko juu sana. Pengine huu ukanda, hasa Meatu, ndiyo unaongoza kwa kutoa mahari kubwa Tanzania nzima.

4.Bhanantuzu /Wanyantuzu
Hawa ni Wasukuma wenyeji wa Wilaya za Bariadi na Itilima. Hawa ndiyo Wasukuma waliotapakaa kila kona ya nchi hii. Na pengine bila ya hawa kabila la Wasukuma
lisingejulikana kwa namna hii. Kisukuma chao hakina 'shi' bali hutumia 'si' kwa mfano, sikolo, siliwa....Jamaa hawa wanajua kuchakalika kutafuta mali. Hawaogopi kitu, hawaogopi mtu. Jamaa hawa ndiyo Wasukuma pekee wanaothubutu kwenda kupora ng'ombe za Wamasaai. Ni Wasukuma wenye dharau na mikogo mingi. Kama unasikia watu wanaopenda utani na masihara, basi hawa ni kiboko. Si unamjua Danni Makanga? Mambo ya ujanja ujanja na upigaji dili, hapa ndipo penyewe. We mwangalie Chenge tu, au hata Cheyo au hata Mbunge Njaru. Utanipa jibu. Wanaume wa huko hupenda kuoa wake weupe. Kama sio mweupe basi awe na sifa za ziada. Michepuko kwa mwanaume ni kitu cha kawaida.

Swala la ni msukuma yupi anaongoza kwa ushamba na ukilaza, halikuwa lengo la utafiti huu.

Mobheja sana.
Nywanhonko ebhe
 
Wale ambao wakilewa wanaongea kisukuma ata na mzaramo ndio kundi gani?
 
Mambo yote kwetu NG'WELI (Leading Agricultural and mining zone)!
Mimi nimetaja majina ya vijiji ninavyovifahamu kule Unyantuzu na kusema nyumbani ni nyumbani tu. Sasa wewe umekuja na mambo ya kilimo na madini (utafikiri kuwa hayo madini yanawasaidia cho chote; wakati yamegeuka laana ya kimazingira na hata kiuchumi). Sijaelewa lengo lako ni nini. Au umejisahau ukadhani kuwa unamjibu Nyani Ngabu?
 
Kama hujui historia ya wasukuma nenda Bujola ukajifunze cyo kudanganya watu kwenye hii forum. Ulichokiandika siyo sahihi kabisa. Kwanza wanyantuzu siyo wasukuma halisi ni mchanganyiko was wanyiramba na wasukuma. Ndoo maana hata baadhi ya majina wanachangia. Kwa mfano Kuna Mangu MNYANTUZU na Mangu MNYIRAMBA. Kwa taarifa yako lahaja za kisukuma ziko katika makundi manne, 1 Banakiya (wa) mashariki) 2.Banang'weli (wa magharibi) yaani ng'ambo ya ziwa 3. Banasukuma (kaskazini) 4.Badakama (kusini). Hao wanyantuzu Unaowasema wako kwenye kundi na.1 hapo juu.
Uko sahihi kabisa, alipotosha kiasi
 
Ni kweli wasukuma wapo makundi manne lakini ninayoyajua mimi haha 1.bhana keyaa 2.w
Bha salama., 3.bhana ng'weli 4.bha sukuma, ambao kundi hili limebeba eneo kubwa na hasa maeneo Ya Mwanza,hawa wanyantuzu wano kwenye kundi la mhana kiyaa ambao wanapatikana maeneo ya bariadi, maswa na wadakama hawa wanapatikana ya nzega Kahama mashariki lakini bhana ng'weli hawa wanapatikana maeneo ushirombo yaani bukombe!
Hovyo kabisa, kama hujui kaa kimya
 
Kwa nyongeza tu ni kwamba msukuma mnagw,eli asili yake ametokea mwanza kwimba misungwi ngudu nk wote hao walivuka maji wakaingia sengerma busambiro geita buyombe bukoli ndiyo hao walingia biharamulo yaani lusubi yote wasukuma wote hao ni wahamiaji
 
Mimi nimetaja majina ya vijiji ninavyovifahamu kule Unyantuzu na kusema nyumbani ni nyumbani tu. Sasa wewe umekuja na mambo ya kilimo na madini (utafikiri kuwa hayo madini yanawasaidia cho chote; wakati yamegeuka laana ya kimazingira na hata kiuchumi). Sijaelewa lengo lako ni nini. Au umejisahau ukadhani kuwa unamjibu Nyani Ngabu?

Hahaaa...halafu wewe...inawezekana ukawa ndugu yangu wewe.

Hivi unamjua Christopher Sayi wewe?

Heheheee....
 
Back
Top Bottom