KAKA A TAIFA
JF-Expert Member
- Apr 27, 2011
- 566
- 80
Jamani kuweni macho na wezi hawa,akina dada/mama=wanawake kadhaa hapa jijini wamekwapuliwa handbags/pochi wanazoninginiza mabegani na wezi hawa.yaani wao wanatembea na bajaji ,pikipiki, tax,magari madogo ya abiria ,wanaendesha mwendo wa taratibu usawa wa mama /dada mtembea kwa miguu akiwa na pochi/handbag lake begani au mkononi.wakishamfikia tu wanalikwapua /wanakupua kwa nguvu na kisha kuondoka kwa mwendo wa kasi.kwa kuwa mlengwa anakuwa kama ameshitukizwa na pia kushtuka kwa tukio, bado anakuwa haamini kilichotokea na hivyo huduwaa.huku mkupuaji akimwacha kwa mbali na waliokaribu kuanza kuelewa kilichotokea.akina mama /dada chukueni tahadhari na jaribuni kuripoti matukio haya polisi.pia ukiweza chukua/andika namba za chombo husika katika tukio.je wanajamii hili mnalionaje?