The Boss
JF-Expert Member
- Aug 18, 2009
- 49,063
- 115,462
ETI WANAWAKE WANAWEZA....HAYA SOMENI WENYEWE HAPA....
SIJUI HII NI AIBU YA WANAWAKE PEKEE YAO,
AU YA WANAUME PEKE YAO,
AU YA KWETU WOTE, BUT NI AIBU KWA KWELI.....
45% ya Wanawake wenye Ajira wametoa Rushwa ya Ngono!
SIJUI HII NI AIBU YA WANAWAKE PEKEE YAO,
AU YA WANAUME PEKE YAO,
AU YA KWETU WOTE, BUT NI AIBU KWA KWELI.....
45% ya Wanawake wenye Ajira wametoa Rushwa ya Ngono!
?45% wanawake, wasichana wamepata kazi kwa ngono?
Wednesday, 16 March 2011 20:36
Nora Damian
ZAIDI ya asilimia 45 ya wanawake na wasichana walioajiriwa kwenye ofisi mbalimbali nchini, zikiwamo za serikali walipata ajira hizo baada ya kutoa rushwa ya ngono, imeelezwa.
Hayo yalisemwa jijini Dar es Salaam jana na Mwenyekiti wa Asasi ya Ushauri Nasaha na Maisha ya Familia (CAFLO), Mariam Mlugu, kwenye mafunzo kwa viongozi wa serikali za mitaa kuhusu unyanyasaji wanawake na wasichana katika familia.
Mlugu alisema hali ya unyanyasaji wa mwanamke imekuwa ikiongezeka kila siku, hasa ngazi ya familia na kaya, kazini na maofisini.Wengi wa wanawake na wasichana, wamekuwa wakinyanyasika kingono ikiwamo kubakwa, kupigwa na kunyimwa haki ya kurithi mali na hata kuuawa, alisema Mlugu.
Alisema zipo sababu mbalimbali zinazowafanya wanawake kunyanyasika, kama kutofahamu haki za binadamu, mfumo dume, mawazo mgando, mila, desturi na wanawake kutotambua nafasi na majukumu yao kwenye familia.
Pia, Mlugu alisema unyanyasaji wanawake na wasichana haupo Tanzania peke yake, kwani ni tatizo ambalo limeenea sehemu nyingi duniani na kutolea mfano Afrika Kusini kuwa, hadi kufikia mwishoni mwa mwaka jana, wastani wa wanawake watatu walikuwa wakibakwa kila baada ya dakika 90.
Mwenyekiti huyo alisema unyanyasaji mwanamke unaleta madhara makubwa kwenye familia na jamii, kama kushuka kwa kasi ya maendeleo, kuongezeka kwa umaskini, kupotea kwa hadhi na thamani ya utu wa mwanamke.
Kwa mujibu wa mwenyekiti huyo, madhara mengine ni kusambaratika kwa familia, kuongezeka kwa matatizo kama Ukimwi, vifo na watoto wanaoishi kwenye mazingira hatarishi.
Nao viongozi wa serikali za mitaa walioshiriki mafunzo hayo, ambao wanatoka kata za Buguruni na Vingunguti, waliaswa kuwa na mikakati mahsusi ya kutokomeza unyanyasaji huo, kwani wao ni wadau wakubwa wa mapambano hayo.
Pia, viongozi hao walitakiwa kuimarisha mabaraza ya usuluhishi kwa kuwawezesha wadau, kupata mbinu sahihi na utaalamu wa kutatua kesi mbalimbali zinazoletwa kwenye mabaraza yao.Mlugo aliwataka wanaume kutumia nafasi zao kuleta maendeleo ndani ya familia, bila kubagua wanawake kwani wakipewa fursa wanaweza kuleta mabadiliko ya familia na taifa.
Wednesday, 16 March 2011 20:36
Nora Damian
ZAIDI ya asilimia 45 ya wanawake na wasichana walioajiriwa kwenye ofisi mbalimbali nchini, zikiwamo za serikali walipata ajira hizo baada ya kutoa rushwa ya ngono, imeelezwa.
Hayo yalisemwa jijini Dar es Salaam jana na Mwenyekiti wa Asasi ya Ushauri Nasaha na Maisha ya Familia (CAFLO), Mariam Mlugu, kwenye mafunzo kwa viongozi wa serikali za mitaa kuhusu unyanyasaji wanawake na wasichana katika familia.
Mlugu alisema hali ya unyanyasaji wa mwanamke imekuwa ikiongezeka kila siku, hasa ngazi ya familia na kaya, kazini na maofisini.Wengi wa wanawake na wasichana, wamekuwa wakinyanyasika kingono ikiwamo kubakwa, kupigwa na kunyimwa haki ya kurithi mali na hata kuuawa, alisema Mlugu.
Alisema zipo sababu mbalimbali zinazowafanya wanawake kunyanyasika, kama kutofahamu haki za binadamu, mfumo dume, mawazo mgando, mila, desturi na wanawake kutotambua nafasi na majukumu yao kwenye familia.
Pia, Mlugu alisema unyanyasaji wanawake na wasichana haupo Tanzania peke yake, kwani ni tatizo ambalo limeenea sehemu nyingi duniani na kutolea mfano Afrika Kusini kuwa, hadi kufikia mwishoni mwa mwaka jana, wastani wa wanawake watatu walikuwa wakibakwa kila baada ya dakika 90.
Mwenyekiti huyo alisema unyanyasaji mwanamke unaleta madhara makubwa kwenye familia na jamii, kama kushuka kwa kasi ya maendeleo, kuongezeka kwa umaskini, kupotea kwa hadhi na thamani ya utu wa mwanamke.
Kwa mujibu wa mwenyekiti huyo, madhara mengine ni kusambaratika kwa familia, kuongezeka kwa matatizo kama Ukimwi, vifo na watoto wanaoishi kwenye mazingira hatarishi.
Nao viongozi wa serikali za mitaa walioshiriki mafunzo hayo, ambao wanatoka kata za Buguruni na Vingunguti, waliaswa kuwa na mikakati mahsusi ya kutokomeza unyanyasaji huo, kwani wao ni wadau wakubwa wa mapambano hayo.
Pia, viongozi hao walitakiwa kuimarisha mabaraza ya usuluhishi kwa kuwawezesha wadau, kupata mbinu sahihi na utaalamu wa kutatua kesi mbalimbali zinazoletwa kwenye mabaraza yao.Mlugo aliwataka wanaume kutumia nafasi zao kuleta maendeleo ndani ya familia, bila kubagua wanawake kwani wakipewa fursa wanaweza kuleta mabadiliko ya familia na taifa.