Aibu kubwa kwa polisi - hadi sasa wachoma makanisa Zenj na waliomteka Ulimboka hawajakamatwa!

Zak Malang

JF-Expert Member
Dec 30, 2008
5,404
233
Leo hii ni karibu miezi miwili na nusu tangu makanisa yachomwe huko Zanzibar na 'watu wasiojulikana'. Na vile vile ni karibu wiki tatu tangu Dr Ulimboka akamatwe na 'watu wasiojulkana na kupigwa vibaya.

Matukio yote mawili jeshi letu la polisi lilidai kuwa lingefanya uchunguzi wa kina na kuwakamata wahusika na kuwapeleka katika vyombo vya sheria, lakini hata mtu mmoja hajakamatwa.

Hii jamani siyo aibu kubwa kwa jeshi letu la polisi ambalo juzi tu waziri wao, Dr Nchimbi alijidai ni jeshi makini na kwamba yoyote asiyeliamini ana matatizo?

Zanzibar ni sehemu ndogo sana na watu wachache ambao wengi wanajijua. Inakuwaje hadi sasa polisi imeshindwa kuwakamata wahusika wa uchomaji wa makanisa?

Au sasa tuanze kuamini yanayozungumzwa sana, tena sana mitaani kwamba kuna mkono wa serikali katika matukio yote mawili, na polisi kazi yake ni kuilinda tu serikali kwa maovu hayo?
 
Nimesoma jana JF kuwa Erick Shigongo ameshikwa, sijui kwanini? Jee, inaweza kuwa anahusika na hayo matukio?
 
Unajua mwizi anapopigwa na wananchi, polisi hajui amkamate nani ikiwa mwizi huyo amekufa au amefariki.

Sasa kwa hili la makanisa ile ni kama riot imetokea, inaweza nkuwa vibaka,au hao uamsho ambao wamekanusha pia inawezekana ni vikosi kazi mbaya vya serikali ,ili kuwadhibiti watu flani kwa kuwasingizia, ila WaZanzibari ni wamoja hivyo hilo limefeli, la Ulimboka hatujui kinachoendelea kwani waliokuwa na Dr katika hatua za mwanzo wapo, mawasiliano yapo, maana kama simu ya Uli ilipotea data za simu yake zinakuwepo katika kampuni ya simu ,alimpigia nani alipigiwa na nani kwa wakati huo aliotoweka.

Huwezi kupata mazungumzo lakini wapi na wapi alipiga na kupokea simu utaweza kuzijua namba zilizohusika kama CDM wana mshiko ndani ya makampuni ya simu wanaweza kujua alizungumza na kupigiwa na namba ipi au zipi.
 
Leo hii ni karibu miezi miwili na nusu tangu makanisa yachomwe huko Zanzibar na 'watu wasiojulikana'. Na vile vile ni karibu wiki tatu tangu Dr Ulimboka akamatwe na 'watu wasiojulkana na kupigwa vibaya.

Matukio yote mawili jeshi letu la polisi lilidai kuwa lingefanya uchunguzi wa kina na kuwakamata wahusika na kuwapeleka katika vyombo vya sheria, lakini hata mtu mmoja hajakamatwa.

Hii jamani siyo aibu kubwa kwa jeshi letu la polisi ambalo juzi tu waziri wao, Dr Nchimbi alijidai ni jeshi makini na kwamba yoyote asiyeliamini ana matatizo?

Zanzibar ni sehemu ndogo sana na watu wachache ambao wengi wanajijua. Inakuwaje hadi sasa polisi imeshindwa kuwakamata wahusika wa uchomaji wa makanisa?

Au sasa tuanze kuamini yanayozungumzwa sana, tena sana mitaani kwamba kuna mkono wa serikali katika matukio yote mawili, na polisi kazi yake ni kuilinda tu serikali kwa maovu hayo?

watajikamataje wenyewe ilihali jeshi lenyewe linaendeshwa na vichwa sampuli ya ZOMBA.
 
Nimesoma jana JF kuwa Erick Shigongo ameshikwa, sijui kwanini? Jee, inaweza kuwa anahusika na hayo matukio?

Haaahaaa! Asije akawa amewaandika waheshimiwa kwenye vile vigazeti vyake. On a serious note, mbona polisi ina suasua kufanya kazi yake kwenye baadhi ya matukio?
 
Unajua mwizi anapopigwa na wananchi ,polisi hajui amkamate nani ikiwa mwizi huyo amekufa au amefariki.Sasa kwa hili la makanisa ile ni kama riot imetokea ,inaweza nkuwa vibaka,au hao uamsho ambao wamekanusha pia inawezekana ni vikosi kazi mbaya vya serikali ,ili kuwadhibiti watu flani kwa kuwasingizia ,ila WaZanzibari ni wamoja hivyo hilo limefeli ,la ulimboka hatujui kinachoendelea kwani waliokuwa na Dr katika hatua za mwanzo wapo ,mawasiliano yapo ,maana kama simu ya Uli ilipotea data za simu yake zinakuwepo katika kampuni ya simu ,alimpigia nani alipigiwa na nani kwa wakati huo aliotoweka.

Huwezi kupata mazungumzo lakini wapi na wapi alipiga na kupokea simu utaweza kuzijua namba zilizohusika kama CDM wana mshiko ndani ya makampuni ya simu wanaweza kujua alizungumza na kupigiwa na namba ipi au zipi.

Kama serikali ikiamua, inaweza kabisa kutumia mkono wake mrefu kuwakamata wahusika wote. Kimya kingi kina mshindo mkuu. Hii haijakaa vizuri
 
iliwachukua miaka 10 majasusi wa CIA kumnasa na kumuua Osama Bin Laden.

Iliwachukua miezi kadhaa hadi tarehe 31 Mei 2012 kwa Jeshi la polisi kumkamata aliyemuua Mwenyekiti wa chadema Arumeru. Muuaji Alikuwa kakimbilia Singida.

Wahalifu wote wana mbinu zao hakuna muda maalum kwa chombo cha dola wa kumkamata mhalifu. Ni mapema sana kusema polisi wameshindwa kuwasaka na kuwanasa.
 
Nimesoma jana JF kuwa Erick Shigongo ameshikwa, sijui kwanini? Jee, inaweza kuwa anahusika na hayo matukio?

kama ni taarifa zinazoweza kulisaidia jeshi la polisi ni vema zikapolekwa sehemu husika kwa ajili ya kusaidia uchunguzi..... kwa yule mwenye taarifa kwa kina.
 
Leo hii ni karibu miezi miwili na nusu tangu makanisa yachomwe huko Zanzibar na 'watu wasiojulikana'. Na vile vile ni karibu wiki tatu tangu Dr Ulimboka akamatwe na 'watu wasiojulkana na kupigwa vibaya.

Matukio yote mawili jeshi letu la polisi lilidai kuwa lingefanya uchunguzi wa kina na kuwakamata wahusika na kuwapeleka katika vyombo vya sheria, lakini hata mtu mmoja hajakamatwa.

Hii jamani siyo aibu kubwa kwa jeshi letu la polisi ambalo juzi tu waziri wao, Dr Nchimbi alijidai ni jeshi makini na kwamba yoyote asiyeliamini ana matatizo?

Zanzibar ni sehemu ndogo sana na watu wachache ambao wengi wanajijua. Inakuwaje hadi sasa polisi imeshindwa kuwakamata wahusika wa uchomaji wa makanisa?

Au sasa tuanze kuamini yanayozungumzwa sana, tena sana mitaani kwamba kuna mkono wa serikali katika matukio yote mawili, na polisi kazi yake ni kuilinda tu serikali kwa maovu hayo?
Thubutuu!! Polisi awakamate TISS!! haiwezekani!!
 
Kama serikali ikiamua, inaweza kabisa kutumia mkono wake mrefu kuwakamata wahusika wote. Kimya kingi kina mshindo mkuu. Hii haijakaa vizuri

Uchunguzi duniani kote sio suala la serikali kuamua .....

Ningekuelewa kidogo ungesema ni suala la wananchi kuamua kuisaidia serikali kuipa ushirikiano wa kuwakamata wahalifu kwani wahalifu tunaishi nao kwenye jamii.
 
Uchunguzi duniani kote sio suala la serikali kuamua .....

Ningekuelewa kidogo ungesema ni suala la wananchi kuamua kuisaidia serikali kuipa ushirikiano wa kuwakamata wahalifu kwani wahalifu tunaishi nao kwenye jamii.

Kwani kwetu hapa sifa za amani na utulivu ana jipa nani? wananchi wanasifiwa popote pale au ni nyinyi waheshimiwa tu ndio mnahusika na kutunza amani na utulivu? Kama wananchi wanatoa michango yao, ina maana so far hakuna hata mwananchi mmoja aliyetoa mwelekeo wa wahusika wa matukio hayo yote?
 
Thubutuu!! Polisi awakamate TISS!! haiwezekani!!

Hakuna iliye juu ya sheria ni mashaka yako tu.

TISS imeundwa kisheria hivyo kinyume chake ni kukiuka sheria..... polisi hawawezi kushindwa kuwakamata.

Tumeshuhudia wanajeshi (JWTZ) na TISS wamekamatwa na kufikishwa mahakamani.

post yako inataka kuonyesha kuwa TISS wanaweza kufanya lolote na wasiguswe na sheria si kweli.
 
Kwani kwetu hapa sifa za amani na utulivu ana jipa nani? wananchi wanasifiwa popote pale au ni nyinyi waheshimiwa tu ndio mnahusika na kutunza amani na utulivu? Kama wananchi wanatoa michango yao, ina maana so far hakuna hata mwananchi mmoja aliyetoa mwelekeo wa wahusika wa matukio hayo yote?



Anaweza kuwepo polisi mmoja mmoja aliyekosa wajibu kama ilivyo kwa mchungaji, askofu, sheikh na Imam kukosa wajibu wake lakini hiyo haina maana kwamba nyumba za ibada makanisa na misikiti sio mahali patakatifu.

Ingependeza kama wewe mwenyewe ungetoa mfano wa ushiriki wako wa kutoa ushirikiano kwa polisi.... ulikwenda kituo kipi cha polisi, kwa kesi ipi na ulikutana na nani kwa ushaidi upi, na kunyimwa haki yako.

kusimulia hadithi za wengine ndiko kunatupeleka hadi kwenye magomvi mengi kama ya kidini na kikabila.
 
Kamuulize mkuu wa kitengo cha mabwepande jack zoka



Utani kama huu ndio unatufanya kutia mashaka dhidi ya tuhuma za Zoka... kujenga hoja kutatusaidia kuamini dhidi yake.....utani unaongeza mashaka.

Tuhuma zinazoacha shaka hata mahakamani hutupwa
 
sio rahisi kuandika jambo zuri dhidi ya jeshi la polisi kama unalichukia, post imejaa kulichukua jeshi lote na kila Afisa wa jeshi sio fear hata kidogo.

Ni juzi tu polisi walikuja kuniokoa mimi na familia yangu tulipovamiwa na majambazi wakafanikiwa kumuua mmoja na kukamata wawili.
 
HAPO UJUE WAO NDO WAHUSIKA WAKUBWA AU NI INSTRUCTION FR TISS/ UWT NA HATA WANASHINDWA WAMBANE NANI?? aaaahh
 
Kuna kitu ambacho watu hawajui, Polisi ni chombo ambacho kina professional ethics zake, na sio kila anayekamatwa na polisi kwa tuhuma basi ni muhalifu ndo maana upelelezi unafanyika ili kupata ushahidi, tukumbuke sheria zetu zinasema mtuhumiwa anahaki zake hadi pale tuhuma zitakapothibitishwa zidi yake, na hata kama kuna watu wamekamatwa hawawezi kutangazwa kwenye vyombo vya habari kwa sababu upelelezi wake unaweza kuwa mgumu, sasa tujiulize hivi tunauelewa wa kutosha kweli?

Au tunafuata mkumbo tu wa kisiasa kulaumu? Mimi ninachojua polisi ktk mambo ya uchunguzi inafanya kazi kwa usiri mkubwa kwa lengo la kuwalinda mainformer, na vilex2 kulinda haki za watuhumiwa.

Sasa mnapotaka itangaze kila kitu mnataka kuingilia kazi za vyombo vya dola? kama ni hivyo basi nawashauri muingie kazi za polisi ili muone utendaji wake ulivyo. tukumbuke Polisi sio wanasiasa.
 
sio rahisi kuandika jambo zuri dhidi ya jeshi la polisi kama unalichukia, post imejaa kulichukua jeshi lote na kila Afisa wa jeshi sio fear hata kidogo.

Ni juzi tu polisi walikuja kuniokoa mimi na familia yangu tulipovamiwa na majambazi wakafanikiwa kumuua mmoja na kukamata wawili.

Ukiona mtu anachukia Polisi na vyombo vya dola ujuwe huyo ni mhalifu sugu.
 
Back
Top Bottom