Aibu hii ikikutokea utauweka wapi uso wako?

Madame B

JF-Expert Member
Apr 9, 2012
29,948
32,204
Habari wana Jf,
Juzi kwa rafiki yangu kulikuwa na sherehe ya kuvishwa pete ya uchumba mdogo wake,watu tulikuwa wengi tu sebuleni,
Ghafla ktk hali isiyotarajiwa aliibuka mtoto wa mdogo wake akiwa amevaa Ch*pi ya mama yake kichwani,kwa kuwa watu walikuwa busy hakuna aliyemuona,yule mtoto alikuja katikati hadi kwa mama yake na mchumba wake na kukaa pale,
aisee sikuweza kuendelea kukaa, nilitoka nje kwa aibu.

Sasa swali linarudi kwako,ungekuwa wewe ndo bi mdada muolewaji ungefanya nini?
 
Ulitaka afanyaje? Aachea sherehe ya uchumba kisa mtoto kavaa chupi? Chupi ni nguo lakini ni ya ndani ndiyo utofauti ulipo.

Ni tukio la bahati mbaya na haliwezi kuathiri mpangilio wa sherehe.

Mfano upo ukumbini kwenye sherehe ukasikia mdogo wako mgonjwa utaacha ndoa uende kumuona mgonjwa?
 
Tatizo sijaliona mkuu hilo kufuli halina shida ungelichukua tu na kumkabidhi mwenyenalo
 
Hizo burudani tu za watoto......
Mie mwanangu mdogo kusema mjomba hawezi, anasema "Ntomba"!

Sasa wakija wageni na mjomba wake yupo karibu inakuwa balaa!!
 
ningekuwa mimi ningeipost hii uzi kwa jukwaa la jox,utanni na udaku
 
we ukishikwa na tumbo la kuhara wakati wa ndoa utaomba kwenda msala au utasubri adi ujinyee ili watu wajue ni mdhaifu.
 
hiyo si aibu ni kituko...mwisho wa siku watu wataishia kucheka kwa kuwa muhusika ni mtoto mdogo.
 
inategemea kufuli lenyewe likoje bana!kama ni chafu halafu katikati kama limetoboka c aibu hiyo?
 
Aibu gani sasa hapo? Kwani ni mtu mzima huyo hata mtegee mambo tofauti toka kwake?
 
Habari wana Jf,
Juzi kwa rafiki yangu kulikuwa na sherehe ya kuvishwa pete ya uchumba mdogo wake,watu tulikuwa wengi tu sebuleni,
Ghafla ktk hali isiyotarajiwa aliibuka mtoto wa mdogo wake akiwa amevaa Ch*pi ya mama yake kichwani,kwa kuwa watu walikuwa busy hakuna aliyemuona,yule mtoto alikuja katikati hadi kwa mama yake na mchumba wake na kukaa pale,
aisee sikuweza kuendelea kukaa, nilitoka nje kwa aibu.

Sasa swali linarudi kwako,ungekuwa wewe ndo bi mdada muolewaji ungefanya nini?

inaonekana huko chumbani ilikotoka hyo ch...pi kuko vurugumechi, kama leo kotoka na hiyo nguo siku nyingine atatoka na kond....mu
 
Hyo chupi inavaliwa na mtu mwenye umri gan?kama m2 mzma lyk that mum lazma uhc soni
 
Back
Top Bottom