Aibu %25 tu wafaulu mitihani ya NBAA Taifa

Candid Scope

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
11,883
6,884
Wengi waanguka mtihani wa NBAA
MATOKEO ya mtihani wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi Hesabu (NBAA) uliofanyika Novemba mwaka huu, yameidhinishwa na kuonesha kuwa idadi kubwa ya watahiniwa hawakufanya vizuri katika mtihani huo. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi Mtendaji NBAA Pius Maneno, mtihani huo ulihusisha watahiniwa wa ngazi za ATEC I, ATEC II, Foundation Stage Modules A na B, Intermediate Stage Modules C na D na Final Stage Module E na F.

Alisema kati ya watahiniwa 3,414 waliofanya mtihani wa NBAA, watahiniwa 854 sawa na asilimia 25.0 walifaulu na wengine 1,048 sawa na asilimia 30.7 watatakiwa kurudia masomo waliyoshindwa huku watahiniwa 1,512 sawa na asilimia 44.3 hawakufaulu mtihani huo.

Aidha alisema katika ngazi ya mwisho ya F watahiniwa 260 sawa na asilimia 29 kati ya 874 ya watahiniwa waliofanya mtihani wamefaulu, na wengine 284 sawa na asilimia 32.5 watarudia somo moja na watahiniwa 330 sawa na asilimia 37.8 hawakufaulu.

“Vilevile watahiniwa 362 sawa na asilimia 19.2 kati ya watahiniwa 1,883 wamefaulu mtihani wa taaluma ngazi ya Module E na wengine 471 sawa na asilimia 25.0 watarudia somo moja ambapo watahiniwa 1,050 sawa na asilimia 55.8 hawakufaulu,” alisema Maneno.

Alisema kwa upande wa mtihani wa Shahada ya juu ya Uhasibu nchini (CPA) watahiniwa 268 walifaulu na hivyo kufikisha idadi ya watahiniwa waliofaulu mtihani huo wa CPA 3,876 tangu mtihani huo uanze mwaka 1975.

Kwa ngazi ya Module D, watahiniwa 37 sawa na asilimia 33 kati ya 109 wamefaulu na wengine 62 sawa na asilimia 56.9 watarudia somo moja huku watahiniwa 10 sawa na asilimia 9.2 hawakufaulu.

Katika mtihani wa Module C watahiniwa 37 sawa na asilimia 29.8 kati ya 124 wamefaulu na 40 sawa, asilimia 32.3 watarudia somo na 47 sawa na asilimia 37.9 walifeli.

Katika ngazi ya uandishi na utunzaji wa vitabu vya hesabu (ATEC II) watahiniwa 31 sawa na asilimia 25.6 kati ya 121 wamefaulu, 43 sawa na asilimia 35.6 watarudia somo na watahiniwa 47 sawa na asilimia 38.8 hawakufaulu.
 
Full time wako facebook, tutazamie nini ufaulu wao wakati fikra na mawazo ni kuchati na ....? Hayo huliwaza moyo na kupumbaza akili na matokeo ndo hayo.
 
...Mitihani hii wanafanya kama kukomoa watu vile ili kuwahenyesha miaka chungu nzima huku wakijikusanyia michuzi yao kibao.
 
...Mitihani hii wanafanya kama kukomoa watu vile ili kuwahenyesha miaka chungu nzima huku wakijikusanyia michuzi yao kibao.

Hata hivyo kiwango cha kufaulu ni chini mno, labda kuna kasoro katika ufundishaji na pia mfumo wa kutahini wanafunzi.

Jambo moja nakubaliana nawe mitihani Tanzania inatungwa kwa kukomoa wanafunzi, ni mfumo ule wa zamani ambao ulelenga kuchagua wanafunzi wachache ambao wataendelea na masomo ya juu kutokana na shule na vyuo kuwa vichache. Lakini katika hali ya sasa mwelekeo wa utungaji mitihani inabidi utazamwe upya kwa vile hauzingatii mazingira na nafasi ya kazi ambazo wahusika wanaenda kufanya, kuajiriwa na kujiajiri.

Nashangaa "O" atafanya final Exam ya kuanzia kidato cha kwanza hadi cha nne wakati alishafanya mtihani wa kidato cha pili. Ningetazamia mfumo wa kutahini "O" ungekuwa wa kiwango cha miaka miwili ya mwisho yaani kidato cha tatu na nne kwa vile vidato vya awali viwili alishafanyia mtiahni. Kwa maana hiyo mtihani unaonekana kuwa mzigo sana kwa wanafunzi kutokana na upana wa eneo wanalofanyia mtihani, hii husababisha pia baadhi ya wanafunzi kufanya vibya.

 
  • Thanks
Reactions: BAK
hapa ukiangalia performance kichuo ndio utachoka, kuna vyuo unakuta candidates wote wamefail, ukiangalia vyeti vya chuo vinaonesha mtu ana 1st class huku fail
 
hapa ukiangalia performance kichuo ndio utachoka, kuna vyuo unakuta candidates wote wamefail, ukiangalia vyeti vya chuo vinaonesha mtu ana 1st class huku fail
Vyuo vingine vina vilaza wa kutosha,kwa kweli inasikitisha!
 
Vyuo vingine vina vilaza wa kutosha,kwa kweli inasikitisha!

Vyuo vya wenzetu walioendelea kabla ya kupokelewa chuoni kuna entry level test ambayo inapima uwezo na kiwango cha elimu alichonacho mwanachuo mtarajiwa. Na kama hatakubaliwa kuanza masomo kwa sababu ya kupata alama za chini katika majaribio hayo, kuna madarasa ya kuanza ambayo kusaidia kumwinua kiwango hadi aweze kuhimili mikikimikii ya chuo. Lakini vyuo vya bongo ni kujuana, matokeo ndo hayo, aibu tupu.

Nilijaribu kufanya reseach facebook na kugundua over 75% wanaokuwa active ni college student hapa Tanzania, hii ni hatari maana computer na simu zinatumika kwa ajili ya social activities badala ya research studies. Na bado serikali inakusudia upunguza madarasa kutoka 7 hadi 6. Bora wangesema turudi kwenye madarasa nane ya zamani.
 
Vyuo vingine vina vilaza wa kutosha,kwa kweli inasikitisha!

sasa inakuwaje mtu ana 1st class halafu huko afail? maana nilipoangalia zile performance sikuamini kuna universities hazijawahi kutoa candidate aliyepass NBAA
 
Back
Top Bottom