Ahsante wana JF

Shikamoo,

Mimi Mike,.... waliniuliza kwanini najihusisha na siasa na sisomi, nikawambia ilikuwa ni mwanzoni na sasa nasoma niko shule na jf sijihusishi sana.
Asanteni nyote kwa uhshirikiano

Pole sana Mike! Yes ni katika maisha kuna mitihaani mingi sana. Lakini wakati mwingine unapopata adha kwa kuwapigania wanyonge na kusimamia haki hakuna sababu ya kujilaumu.

Nakubaliana na ukweli kuwa JF kama jamii ya watu tunaoipenda nchi yetu na watanzania wenzetu hatupotez muda humu ndani sababu ya kutaka kumdhalilisha mtu na wala hatuungi mkono ugaidi, uchochezi wala kudhalilishana. Tunachofanya ni kutoa sauti kwa niaba ya watanzania wote. Sauti za wanyonge. Watanzania wanaoishi katika mazingira magumu wakati viongozi waliokuwa na jukumu la kuwakomboa wameelekeza interst katika biashara zao binafsi. Kwa upande mwingine tunaisiadia serikali na Mhemshimiwa Rais katika kuijenga nchi. Rais JK katika hotuba yake iliyopita alisisitiza umuhimu wa maadili ya viongozi na kuheshimu kazi zao badala ya kutanguliza maslahi ya biashara binafsi. Uki-summarize mambo mengi yaliyomo ndani ya JF utakuta kuwa ujumbe mkubwa ni huo huo wa kudai discipline ya viongozi kwa maslahi ya taifa.

Hongera sana kwa kuipenda nchi yako. Nawaweka katika list moja na Chief Mkwawa, Mirambo, Isike, Kimweri,Mangis, Mac, Mike, Mwanakijiji, na wengine!

Nakutakia masomo mema mkuu.
 
Poleni Mac na Mike. Tuko pamoja; na kwa umoja huo tutashinda. Mungu awabariki na kuwaimarisha.

Nadhani mengi yameshaongelewa, mimi nijazie kwa kuwapa pole tu kwa masahibu yaliyowapata, na nawaombea kwa Mungu awazidishie nguvu na muendelee na majukumu yenu kama kawaida.
Long Live JF!
 
Jeshi haambiwi pole, ina ninachoweza kusema ni songa mbele,bendera ya JF kwa sasa isiwachwe ikagusa mchanga tena.
 
Wakuu Mac na Mike nawapongeza sana kwa kuwa watulivu mpaka waliotaka kuwaangamiza kushidwa baada ya sara mbalimbali kutoka kwa JF na watanzania kwa ujumla kuomba kwa nguvu zao zote.

Mimi ilinisikitisha sana pale nilipoona mtu anayeangaika kukusanya matangazo ya kazi na kuwapa watanzania hili waweze kupata angalau mlo wa siku moja anashikiriwa eti na polisi kwa sababu zisizokuwa za msingi.


Hila nawahakikishieni next time watakuja kugundua kuwa kila mtanzania mwenye Uzalendo atakuwa mwanachama wa JF. Kuna siku hata akina DCI tutakuwa nao hapa.

Shukurani zimwendee Mwanakijiji aliyeweza kutoa sauti kwa nguvu siku alipoongea na BBC tulifarijika sana ilionekana kama tunaelekea kutoka kwenye giza na makucha ya wadhalimu wasiopenda kuona nchi yetu inakuwa kati ya nchi zinazoweza kusonga mbele.

Katika kumbukumbu zangu nimeweka mahojiano mbalimbali na hilo la DCI na Mwanakijiji nimeliwekea kwa ajili ya vizazi vijavyo ili viweze kusikia jinsi mapambano ya kifikira yasivyo ya mchezo.
 
Mike na Mac poleni sana.

Ninachoweza kusema, kweli nimegundua kuna watanzania wengi out there, wenye uchungu wa kweli na nchi yao na wanakosa tuu opportunity ya kuweka bayana dhamira zao. Na wengi wanafanya maamuzi mengi si kwa sababu wanapenda lakini kwa sababu ya shuruti na kuogopa reprisals. I do believe that the wind of change has come, kama anavyosema Jaluo wa democrat huko USA, just leave those cynicals aside, those who tells you that you cant accomplish anything, those who say it is impossible!
Tanzania is changing and it is changing for the better,. Safari ni ndefu, cha muhimu ni kuianza!

Now, we can easily know that, watawala wetu wanaogopa hoja, mawazo mbadala, wanaogopa jamii yenye mwamko na uelewa. wanaogopa kwamba ideas zao zitakuwa challenged and scrutinized and discredited! Nitakuwa muongo nikisema kwamba ndo maana serikali zetu hazitoi kipaumbele kwenye sector ya elimu kama chuo kikuu na vyuo vingine? kwa sababu ya kuogopa jamii yenye uelewa? we jiulize mawazo ya watu wachache hapa JF yanawakosesha usingizi..what will happen kama nusu ya watanzania wote wakitoka usingizini?

I have a dream, Tanzania if finally, waking up, matching towards its rightful place to that table of the nations! Where all Tanzanians will be equally and justly treated!

What should the governement know for sure is: Tanzanians have finaly woken up after years of manipulation and division of their leaders. The leaders should prepare for accountability and responsibility, short of that they should give space to others.

Viva Tanzania, our mother land!
 
Ilikuwa ni safari ya kifo cha uhuru wa habari Tanzania lakini sasa uhuru umerejea. Ni ushindi wa wana JF (wasomaji na waliojisajili) wote.

Naomba kutoeleza chochote zaidi lakini nipeleke shukrani zangu za kipekee kwa wana habari wote: Magazeti ya HabariLeo, Mtanzania, ThisDay, Kulikoni, Tanzania Daima n.k. Pia blog mbalimbali ambazo nimezipitia ikiwa ni pamoja na KLH News, Michuzi, eThinkTank na wengine wengi. Ukweli ni kuwa bila ninyi kuliweka wazi suala hili basi tulikuwa kwenye wakati mgumu sana.

Aidha niwashukuru watu binafsi ikiwa ni pamoja na Mwanakijiji, Mhariri wa ThisDay, Zitto Kabwe, John Mnyika, Tundu Lissu, Wakili Armao, Mchumba wangu (namhakikishia ndoa ipo tu July), Mbaraka, W. Malecela, Andrew, Abdallah, na watanzania wote ambao kwa namna moja ama nyingine walihakikisha wanapiga simu kwa DCI Manumba na kwingineko kuhakikisha wanaweka wazi kazi inayofanywa na JF.

Mwisho nawashukuru wenzetu William Mushi na Yona Fares Maro kwa jitihada zao.

Wana JF, tulikubali kuwa na collective responsibility kwa ajili yenu tukiamini nanyi hamtotutupa katika hali hiyo. Tulilazimika kubeba kila aina ya lawama kwa ajili yenu. Vitisho kwetu vimeendelea kuongezeka na usalama wetu unazidi kuwa mdogo. Tuombeane uzima tu.

Niseme kuwa tukubaliane kwamba Tanzania ni yetu sote na watu wachache wanaotaka kuzimika kwa harakati za kuisafisha wasipewe nafasi. Pia wanachama hapa tuache kabisa kuandika habari zisizo na uthibitisho ama zenye dhamira ya kulichafua taifa ambazo chanzo chake kina utata ama hakuna kabisa. Zitapelekea wakati mwingine watu kama FD ama Mnyika nao kukamatwa. Huenda nao wakakubali wao kuwa Invisible.

Kisha nadhani kuna watu wana wasiwasi kuwa kuna kitakachofutwa, sijaona kilichofutwa zaidi ya kuona vilivyohamishwa. Hiyo inamaanisha kuwa kila kitu kipo kama kilivyokuwa. Shukrani kwa moderators.

Namshukuru Invisible kwa kuniruhusu kutumia nickname yake kuweza kuwasilisha maoni haya kwa sasa na kuomba ushirikiano naye pindi mambo kama haya yanapotokea.

Sina mengi ya kuandika zaidi ya kusema "Ahsante watanzania, pamoja tutafika mbali".

Nitaendelea kuwawekea nafasi za kazi kadiri ninavyozipata.

Mac

JF imekuwa ni nyumbani kwetu Watanzania wote walio ndani na nje ya nchi. Tunaupenda ukumbi huu kwa mambo mbali mbali lakini kubwa kuliko yote ni la kujadili hatima ya nchi yetu ambayo kila kukicha inaonekana haipigi hatua yoyote ya kimaendeleo pamoja na kuwa tuna 'amani' katika miaka 46 ya uhuru wetu.

Nchi yetu si maskini kama ambavyo 'Viongozi' wanavyotaka kuamini. Tuna rasilimali nyingi sana ambazo kama mikataba ya kuzivuna rasilimali hizo ingekuwa na maslahi kwa Tanzania na Watanzania basi tungeona mabadiliko makubwa sana katika maisha ya Watanzania walio wengi. Kama vile ongezeko la upatikanaji maji safi, ongezeko la upatikanaji umeme tena wa bei nafuu. Ongezeko la shule zenye madawati na walimu waliofuzu katika nyanja hiyo, lakini mambo si hivyo. Kila kukicha 'viongozi' wanazidi kuwa mabilionea matajiri wa kupindukia wakati Watanzania wengi wakiendelea kuishi maisha ya dhiki kubwa ukilinganisha na miaka 20 iliyopita.

Tumeyakaribisha makampuni mbali mbali yavune rasilimali zetu. Wakati makampuni hayo na shareholders wao kama vile Barrick na mengineyo yakiendelea kupata faida kubwa, Watanzania hatujaona faida yoyote ya rasilimali zetu hizo.

Mwalimu Nyerere na TANU waliweza kupambana na wakoloni na hatimaye kuwang'oa Tanganyika bila kunyanyua bunduki wala kutega bomu. Na sisi pia kwa niaba ya Watanzania wote tunaweza kabisa kupambana na mafisadi wanaoiangamiza Tanzania bila kunyanyua bunduki wala kutega bomu na juhudi zetu zimeanza kutoa matunda, pamoja na kuwa ni madogo lakini yanatia moyo.

Nawashukuru sana wanaJF wote popote pale walipo duniani waliohangaika huku na kule kwa hali na mali ili kuhakikisha usalama wa wenzetu waliokamatwa na pia kuhakikisha JF inarudi hewani haraka iwezekanavyo. Inatia moyo sana kuona kwamba kumbe Watanzania tukiamua kufanya chochote kutetea maslahi ya nchi yetu tunaweza kufanya hivyo. YES, WE CAN.

Mungu awajaalie nyote kwa bidii zenu hizo na vita ya kupambana na mafisadi wanaoingamiza itaendelea mpaka pale tupate ushindi wa kweli na 'viongozi uchwara' wanaowania nafasi mbali mbali za uongozi Tanzania ili kukidhi haja yao ya uroho wa utajiri wa haraka haraka kwa kupitia nyadhifa hizo waogope kuwania uongozi. Tunataka viongozi wa kweli ambao siku zote wataweka maslahi ya Tanzania na Watanzania mbele kuliko yale ya chama chao au yao binafsi. Na wenzetu mliokamatwa poleni sana kwa yaliyowakuta na ujasiri mliouonyesha.

Idumu JF
Mungu ibariki Tanzania
 
JF imekuwa ni nyumbani kwetu Watanzania wote walio ndani na nje ya nchi. Tunaupenda ukumbi huu kwa mambo mbali mbali lakini kubwa kuliko yote ni la kujadili hatima ya nchi yetu ambayo kila kukicha inaonekana haipigi hatua yoyote ya kimaendeleo pamoja na kuwa tuna 'amani' katika miaka 46 ya uhuru wetu.

Nchi yetu si maskini kama ambavyo 'Viongozi' wanavyotaka kuamini. Tuna rasilimali nyingi sana ambazo kama mikataba ya kuzivuna rasilimali hizo ingekuwa na maslahi kwa Tanzania na Watanzania basi tungeona mabadiliko makubwa sana katika maisha ya Watanzania walio wengi. Kama vile ongezeko la uptikanaji maji safi, ongezeko la upatikanaji umeme tena wa bei nafuu. Ongezeko la shule zenye madawati na walimu waliofuzu katika nyanja hiyo, lakini mambi si hivyo. Kila kukicha 'viongozi' wanazidi kuwa mabilionea matajiri wa kupindukia wakati Watanzania wengi wakiendelea kuishi maisha ya dhiki kubwa ulinganisha na miaka 20 iliyopita.

Tumeyakaribisha makampuni mbali mbali yavune rasilimali zetu. Wakati makampuni hayo na shareholders wao kama vile Barrick na mengineyo yakiendelea kupata faida kubwa, Watanzania hatujaona faida yoyote ya rasilimali zetu hizo.

Mwalimu Nyerere na TANU waliweza kupambana na wakoloni na hatimaye kuwang'oa Tanzania bila kunyanyua bunduki wala kutega bomu. Na sisi pia kwa niaba ya Watanzania wote tunaweza kabisa kupambana na mafisadi wanaoiangamiza Tanzania bila kunyanyua bunduki wala kutega bomu na juhudi zetu zimeanza kutoa matunda, pamoja na kuwa ni madogo lakini yanatia moyo.

Nawashukuru sana wanaJF wote popote pale walipo duniani waliohangaika huku na kule kwa hali na mali ili kuhakikisha usalama wa wenzetu waliokamatwa na pia kuhakikisha JF inarudi hewani haraka iwezekanavyo. Inatia moyo sana kuona kwamba kumbe Watanzania tukiamua kufanya chochote kutetea maslahi ya nchi yetu tunaweza kufanya hivyo. YES, WE CAN.

Mungu awajaalie nyote kwa bidii zenu hizo na vita ya kupambana na mafisadi wanaoingamiza itaendelea mpaka pale tupate ushindi wa kweli na 'viongozi uchwara' wanaowania nafasi mbali mbali za uongozi Tanzania ili kukidhi haja yao ya uroho wa utajiri wa haraka haraka kwa kupitia nyadhifa hizo waogope kuwania uongozi. Tunataka viongozi wa kweli ambao siku zote wataweka maslahi ya Tanzania na Watanzania mbele kuliko yale ya chama chao au yao binafsi.

Idumu JF
Mungu ibariki Tanzania

Maneno mazito haya hope JK na Pinda mnasoma ama mnaambiwa what we think and know about my Country .
 
Maneno mazito haya hope JK na Pinda mnasoma ama mnaambiwa what we think and know about my Country .

Mkuu Lunyungu, unafikiri hawasomi? wanapita sana humu! Otherwsie IGP Mwema na Mugasa wangepata wapi "instructions" kutoka kwa wale waliochafuliwa majina na JF??? we unafikiri mpaka MKUU wa polisi IGP na majukumu aliyonayo, personally anaamua kudeal na JF..ni baada ya kugundua JF ni moto na ni jamvi makini katika kutoa hoja zilizojisimamia, ambazo watawala wetu hawajazizoea kbisa! I can guess rightly kwamba hapa JF sasa hata viongozi wa juu wanapita humu kusoma na kujifunza. Sema tuu, kikubwa ni kutegemea kama mawazo ya watanzania wenye uchungu na nchi yao watayafanyia kazi!

JF has proved kwamba it is not the other-usual blog/forum tulizozizoea et al. It is a serious forum for all Tanzanians irrespective of their position.

Infact hii ndo inaprove more than ever kwamba JF should never go commercial. wanaoweza wachangie, wasioweza wachote busara tuu! Liwe jamvi la kila mtanzania, mwenye nacho na asiye nacho. Uhuru wa kutoa mawazo usibinafsishwe! This has been and should continue being a unique identity of JF.
 
Honest baada ya kusoma reply ya Mac kisha nikasoma ya Mike, nikajikuta natokwa na machozi. Poleni sana waugwana, mwenyezi mungu yupo nasi.

Hii inadhihirisha ni jinsi gani Serekeli ya Mh. Jakaya Kikwete imetumia udictator kukamata raia wasio na hatia kwa kisingizio cha usalama. Mambo haya ya kinazi tumeyaona kwenye enzi za Hitler, na enzi za umoja wa nchi za Urusi katika karne hizo. Kukamata wachangiaji katika internet sio dawa ya kuzuia watu kuzungumza mawazo yao, bali ni chachu ya kuwaamsha watanzania wengi kuingia kwenye mchakato huu.

Tanzania haiundwi na kundi la watu kumi au elfu moja, Tanzania inaundwa na watanzania zaidi ya million 36, hivyo kila mtanzania ana haki ya kuzungumza lile adhanialo ni muhimu kwa maoni yake pasipo kuvunja sheria.

Kwa mara nyingine pole sana wandugu,
 
Mkuu Lunyungu, unafikiri hawasomi? wanapita sana humu! Otherwsie IGP Mwema na Mugasa wangepata wapi "instructions" kutoka kwa wale waliochafuliwa majina na JF??? we unafikiri mpaka MKUU wa polisi IGP na majukumu aliyonayo, personally anaamua kudeal na JF..ni baada ya kugundua JF ni moto na ni jamvi makini katika kutoa hoja zilizojisimamia, ambazo watawala wetu hawajazizoea kbisa! I can guess rightly kwamba hapa JF sasa hata viongozi wa juu wanapita humu kusoma na kujifunza. Sema tuu, kikubwa ni kutegemea kama mawazo ya watanzania wenye uchungu na nchi yao watayafanyia kazi!

JF has proved kwamba it is not the other-usual blog/forum tulizozizoea et al. It is a serious forum for all Tanzanians irrespective of their position.

Infact hii ndo inaprove more than ever kwamba JF should never go commercial. wanaoweza wachangie, wasioweza wachote busara tuu! Liwe jamvi la kila mtanzania, mwenye nacho na asiye nacho. Uhuru wa kutoa mawazo usibinafsishwe! This has been and should continue being a unique identity of JF.

Mkuu Masanja maneno mazito hayo, na mimi napenda kuunga mkono hiyo hoja hapo juu. Ila nadhani ili JF iendelee kudumu kuchangia sisi members ni muhimu sana kwa wenye uwezo.Mi nadhani hili haya masaga tujifundishe kuwa na back up za nguvu, including an alternative site ili kumkomalia nyani kuendelee bila kuwa interrupted.

Nawapa pole sana wote walioteseka on our behalf(JF Members) na kwa kutetea haki ya msingi ya kila raia wa nchi hii ya uhuru wa kuzungumza.
 
Inauma sana, pia inatia moyo. nami nawapa pole Mac na Mike kwa yaliyowafika. Umoja wetu utadumu no matter what. Shukrani kwa members na wanaharakati wote waliohakikisha wenzetu wanakuwa huru tena na hatimaye mtandao kurudi hewani. Poleni sana niko pamoja nanyi.
 
JF is back again and sorry for any inconvenience during the past 12 hours.




JF-Administration
 
Asante CMB,Mwanakijiji na ole kwa kuhakikisha hili linawezekana,Najua nyumbani kwa sasa Tanzania watu watakuwa wamefurahi kuiona JF ikiwa Hewani tena.

Mambo yatakayokuja kwa wakti huo na ujao ni miziki mipya na mikali,

Kuna Mziki kuhusu Mkurugunzi wa PPF,JE uhusiano wa kifamilia na Mheshimiwa Mzee wa Uwazi Nkapa umesababisha nini kwa taifa letu?

Maendeleo ya Suala la Lowassa,Je Bunge litakubali kudhalilishwa na Mafisadi?Je spika atachukua hatua zipi?

Kaeni mkao wa kula!
 
Back
Top Bottom