Ahsante Mungu, wife amejifungua salama

Kwani kupata mtoto ni big deal, mi kila siku navikataa hivyo vi-kid. Sasa naona kuna umuhimu wa kuanzisha Jukwaa la UJAUZITO NA KUJIFUNGUA. Siyo kila kitu lazima kije hapa, mwisho mtaanza kupost mpaka chakula mnachokula sasa.

mibaba mingine hata haistahili kuitwa baba. sasa we kuvikataa hivo vitoto unaond deal eeh. afu vikitupwa majalalani mnasema wanawake wakatili kumbe nie ndo chanzo.


wengine wanashinda kutwa kucha wakililia baraka hizi za watoto afu we unasema nini agrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrr

hongera kaka jojipoji kwa kupata kababy bana. hebu mbarikiwe sana.
 
Salam wadau,
Ijumaa ya leo imekuwa ya furaha sana baada ya wife kujifungua salama mtoto wa kiume

hongera Mkuu, Umepata wa kumkabidhi mikoba

Hongera Sana Mkuu!!

Hongera kwa kuleta dume la mbegu, Mungu akukuzie.

hongera sana mkuu kwa kuijaza dunia.

Kwani kupata mtoto ni big deal, mi kila siku navikataa hivyo vi-kid. Sasa naona kuna umuhimu wa kuanzisha Jukwaa la UJAUZITO NA KUJIFUNGUA. Siyo kila kitu lazima kije hapa, mwisho mtaanza kupost mpaka chakula mnachokula sasa.

hongera mkuu!

Mungu awape afya njema mama na mtoto... Mungu awajalie pia hekima na busara mumlee vema!

Saa nyingine ni vema kuongea naMdomo kuliko ****** wako ambaoHauna adabu wala kheshima... Eti kila siku navi kataa hivyo vikidiWatakiwa urudi nyumbani ukafunzwe tena.Kuliko kuja hapa na kuharisha ushenzi kama huu umeniudhi kupita kiasi .. kufilia mbaliMuhuni mkubwa we.

Siku hizi ukiwa mjamzito na ukajifungua salama ni bahati ndugu yangu, Joji amefurahia hiyo bahati so akaona si vibaya kushea furaha yake na memba wenzie... Wanawake wanakufa sana wakat wa kujifungua...

Jojipoli
Hongera sana mkuu na
samahani hapo juu

Mambo swahiba?
Hivi kumbe hata wewe wakasirikaga hv?... Msamehe bure huyu manake hajui alinenalo... Kuna siku atavikumbuka hvyo vi kid bt itakuwa too late...

hongereni.

Hongera sana na mungu azidi kuwabariki mkapate kumlea vyema kijana akapate kukua na kuwa raia mwema na mpiganaji.

Matusi uliyotukana mi namwachia Mungu tu, maandiko yananiambia nisamehe saba mara sabini. Malaika wa Mungu wata-deal na wewe tu, we subiri adhabu tu!

Mshukuru Mungu kwa kila jambo.
Hongera

Hongera sana kaka..
naomba nipendekeze jina la mtoto: Eben-ezer/Ebeneza/Ebenezer/Ebenezeri...spelling yoyote utakayopenda.
Soma: 1Samuel 7:12

glory to god bra
usisahau kutoa sadaka chukua weka kwenye bahasha inenee mema mwambie Mungu nakushukuru na pia taja mahitaji yako kwa huyo mtot Mungu akusaidie mtoto akikuwa aende shule nzuri na si shule ale chakula kizuri na si bora chakula na mengine mengi tu Mungu atokuacha

Ahsante ndugu nitalifanyia kazi

wazo tu
kumbuka muwe mnajitahdi kusali sana sana usiku ,,utaona usiku mambo makubwa watoto wanayaona we huoni soln ni maombi ya kufululiza
mpaka kanalala na sio kulia

Unafiki mtupu.. Eti Malaika wa Mungu wata -deal na mimi..Na hao malaika ambao we unawakata ..Wata deal na nani...Usijifanye mtakatifu naomba..

Hongera sana mkuu.. Mwenyezi Mungu amjalie mama na mtoto afya njema!


hongera sana mkuu , 01/07/2011 tarehe nzuri sana ya siku ya kuzaliwa

nawatakia afya njema mama na mtoto

Hongera sana Mungu awajalie afya njema.

Hongera saaaaana kwenu wote,mleeni mtoto katika njia impasayo yaani amjue Mungu wa kweli

Hongera Kwako, Mpe Pole na Hongera my wife wako.

hongeara zenu sana! Namtakia mtoto afya njema na makuzi bora!

mpe jina langu Edson....

Kubeba mimba na kujifungua salama ni jambo jema na la kumshukuru Mungu!..Hongereni sana wazazi wapya! Malezi mema na welcome to the parenthood!!

Majina mengine bana...hivi hilo lina maana gani!?? ama ni just for purposes of classification!??lol

...na baba! (malizia mkuu)

Hongera sana baba. Mtunze vyema jojipoji jnr...

Sweetlady umenena ukweli mtupu! Jojipoji ana kila sababu ya kuonyesha furaha yake hapa.Maana siku hizi ukiwa mjamzito ni kama unatembea na kifo.Hongera sana Joji!!!!!!!!!

Hongera mkuu,
mi mwenyewe Mungu akipenda soon! Endelea na maombi

hehehe hongera mwaya maana kuna wengine hawajaaliwa. Ushauri wangu mengine nimeyatoa kwa imani ya dini yangu hivyo badilisha kwa imani yako kama wewe ni mkristo lkn natumai utazingatia
1. utakapoenda hospitali kumuona mtoto wako hakikisha umechukua udhu na uko tohara kitu cha kwanza mpe salaamu uyo mtoto (asalaam
aleikum au kwa kiswahili amani iwe juu yako na msamaha uwe juu yako)
2. Mpigie adhana kwenye sikio la kulia na kimu sala kwenye sikio lake la kushoto
3. Mshike kichwa na kumuombea dua kwa Mungu amuepushe na mabalaa na awe mtoto mwema
4. Mtolee sadaka siku ya arobaini kwa kupima nywele zake halafu linganisha uzito wa nywele zake na dhahabu na tuo sadaka ya kiasi cha
fedha kulingana na uzito huo kwa masikini
5. Kumbuka kumfanyia hakika mwanao kwani huu ni wajibu wa kila mzazi kwa mwanae
6. Mkumbushe mama kumnyonyesha mtoto wenu kama hana matatizo ya kunyonyesha. Amnyonyeshe mtoto kama ilivyoelezwa kwenye Korani
kuwa mtoto anatakiwa kunyonyeshwa kwa muda usiopungua miaka miwili atamuachisha mapema tu pale ambapo kutakuwa na matatizo
yanayomfanya afanye hivyo.
7. Hakikisha unampa zawadi au pesa mkeo mbali na matumizi kama ahsante ya adha anayopata mkeo kumnyonyesha mwanao kama
ilivyoandikwa kwenye koran.
8. Kama mkeo kajifungua kwa operation jitahidi usijempa ujauzito mwingine angalau baada ya miaka minne.
9. Ni vizuri kutomuingilia mkeo kwa muda walau wa miezi mitatu tangu ajifungue kama kweli unamjali
10. Jiepushe vishawishi kwa kusali na kuomba Mungu huku ukiamini kuwa mkeo ndio mke bora na mzuuri sana kuliko wote duniani kwani ni
kipindi kigumu sana kwako na ndio wakati wanaume wengi wanaiba nje
11. Tumia kondomu kupanga uzazi kuliko vidonge vya vingine kwani vinaweza mfanya mkeo asindwe kucontrol mzunguko wake wa mwezi
12. Kumbuka ukimaliza kazi ofisini ujitahidi kurudi nyumbani mapema kwani hiki ni kipindi ambacho mkeo atakuwa hana amani sana moyoni na ni kipindi ambacho anahitaji kuwa karibu sana na wewe kama kipindi alichokowa mjamzito. Utani wa hapa na pale na kujiepusha lugha za maudhi ni muhimu sana kipindi hiki ili kumfanya apone haraka
13. Kumbuka kusali kabla hamjalala na kushika kichwa mtoto kumuombea dua kabla hamjalala itasaidia mtoto kutolia sana usiku. Waweza chukua udhu kisha somea maji ayatul kursiyu x 7, surat nas, falaq, ikhlas x 3 kila moja alhamdu mara saba mpake haya maji mwilini mwake na mlambishe kidogo vile vile waweza mpaka juice ya vitunguu swaumu kwenye nyayo za miguu kama anasumbua kulia sana usiku
14. Sisitiza usafi kwa mama na mtoto na hasa vyombo anavyotumia mtoto ni vizuri vichemshwe
15. Pempa ni nzuri kutumia lkn mama inabidi awe makini kwani ni chanzo kikubwa cha UTI hivyo bora kutumia nepi kwani pempas kina mama wengi wanajisahau mtoto akikojolea au kujisaidia ni bora nepi au pempa kubadilishwa haraka iwezekanavyo
16. Muanzishie mwanao mafuta ya samaki kwani ni muhimu sana kwake kutengeneza kinga mwilini na kujenga mifupa na kumpatia vit A
17. Mpe dawa za majimaji za maleria walau kila baada ya miezi mitatu dawa hizi waweza zipata pale Natural therapy opposite hindumandal
18.Clinic ni muhimu na ingekuwa bora sana kwenda na mkeo kwani inapendeza zaidi na mkeo atajisikia jinsi unavyojali
19.ukitoka kwenye mizunguko yako kabla ya kumshika mtoto bora uoge kwanza au unawe mikono kwa sabuni kwanza kwani kumbuka ngozi yake bado chango
20. Sali na umshukuru Mungu kwa kukujaliia mtoto muombee mkeo na mtoto pamoja na wewe binafsi afya njema na Muombe mungu awajallie riziki na kuwaepusha na vishawishi, A wajaliie amani na upendo.


Nakuombea kwa Mungu akuzidishie upendo na amfanye mkeo na wewe mwenyewe kuwa wavumilivu. Awajaalie upendo wa dhati amjaliie mwanao awe na tabia njema, amjalie afya njema na awaepushe wewe, mkeo na mtoto na mabalaa yote. Ewe Mwenyeezi mungu ijaliie familia hii riziki na amani mioyoni mwao, Mjalie mama wa mtoto huyu kupona haraka kutokana na maumivu ya kujifungua
A men

Hongera sana!

Trh 1 July duh? Mzee ulicheza vyema na trh za mwanzo, mwanao atakua mfanyabiashara!

Hongera sana..

Kaonane na daktari wa magonjwa ya akili asap!

hongereni na Mwenyezi Mungu awaajalie kwa hali na mali mkalee vizuri....kabinti kangu keko eti!

Ndugu zangu ahsanteni sana, kwa kweli nimefarijika sana
 
Siku hizi ukiwa mjamzito na ukajifungua salama ni bahati ndugu yangu, Joji amefurahia hiyo bahati so akaona si vibaya kushea furaha yake na memba wenzie... Wanawake wanakufa sana wakat wa kujifungua...
kweli ni jambo la kumshukuru mungu.
 
Saa nyingine ni vema kuongea naMdomo kuliko ****** wako ambaoHauna adabu wala kheshima... Eti kila siku navi kataa hivyo vikidiWatakiwa urudi nyumbani ukafunzwe tena.Kuliko kuja hapa na kuharisha ushenzi kama huu umeniudhi kupita kiasi .. kufilia mbaliMuhuni mkubwa we.
Ha ha ha ha ha ha leo umeniwahi nilitaka kutapika haya haya
 
Hakikisha unampunguzia kazi wife wako kazi kama kufua, kupika, kuosha vyombo kwa kufanya wewe mwenyewe kwa miezi 3

Siku hizi wote wanapewa leave ya siku tatu nasikia...so kwa SIKU TATU TU ndo anaruhuiwa kufanya uyasemayo!
Ila vijana wengi wa siku hizi hizi kazi hawazijui..i doubt kama zitafanyika kweli!!!
 
Siku hizi wote wanapewa leave ya siku tatu nasikia...so kwa SIKU TATU TU ndo anaruhuiwa kufanya uyasemayo!
Ila vijana wengi wa siku hizi hizi kazi hawazijui..i doubt kama zitafanyika kweli!!!

Inabidi amsaidie sana kwa kweli ili atoe maziwa mengi
 
lakin mkuu hii habari ya heri mkuu. mtu amevuka kifo hapo.kulikuwa na mawili..kifo au uhai. kwa wote au kwa mmojawapo sio vibaya kuwashikirikisha JF members. Ndio maana ikapewa jina la Jamii.

Kwani kupata mtoto ni big deal, mi kila siku navikataa hivyo vi-kid. Sasa naona kuna umuhimu wa kuanzisha Jukwaa la UJAUZITO NA KUJIFUNGUA. Siyo kila kitu lazima kije hapa, mwisho mtaanza kupost mpaka chakula mnachokula sasa.
 
Back
Top Bottom