Kalunguine
JF-Expert Member
- Jul 27, 2010
- 2,543
- 134
AHADI zinazotolewa na baadhi ya wagombea uongozi nchini katika kampeni zinazoendelea za uchaguzi mkuu zikitekelezwa, huenda zikawaweka Watanzania pabaya, imebainika.
Taarifa ya kitaalamu imebaini, kwamba kuna wagombea urais ambao wamekuwa wakiwaahidi Watanzania kuondoa kodi katika saruji watakapochaguliwa kuingia Ikulu.
Taarifa ya Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki, iliyotolewa jana na Waziri mwenye dhamana, Dk Diodorus Kamala, ilisema ahadi hiyo inapotosha wananchi na kuwapa matumaini ambayo hayatekelezeki.
Alisema chini ya kifungu 2(4)(c) cha Itifaki ya Umoja wa Forodha wa Afrika Mashariki, nchi wanachama zilikubaliana kuweka na kutekeleza wigo wa pamoja wa ushuru wa forodha kwa bidhaa zitokazo nje ya Jumuiya.
Aliongeza kuwa wigo huo ulianza kutekelezwa Januari mosi, 2005 na viwango vilivyokubalika ni asilimia 0 kwa malighafi, pembejeo za kilimo, dawa na mitambo; asilimia 10 kwa bidhaa zilizosindikwa kiasi; na asilimia 25 kwa bidhaa zilizokamilika katika uzalishaji.
Kamala alisema, bidhaa nyeti ushuru wake ni zaidi ya asilimia 25.
Hivyo nchi binafsi mwanachama haina mamlaka ya kurekebisha viwango vya kodi ya forodha mfumo wa uamuzi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) hauruhusu nchi moja mwanachama, kufuta ushuru wa forodha wa bidhaa ya aina yoyote ile, ikiwamo saruji.
Alisema, kuwaahidi wananchi jambo ambalo halijakubaliwa na viongozi wa nchi zingine wanachama ni kuwadanganya. Kwa kawaida muungana na mkweli, hatoi ahadi ya jambo ambalo uamuzi au utekelezaji wake unategemea ridhaa ya mamlaka nyingine iliyo juu yake.
Alihoji: Je, ombi la kufuta ushuru likikataliwa na nchi zingine wanachama itakuwaje? Je, mhusika atawarudia wapiga kura na kuwaambia kuwa alitoa ahadi hewa au isiyo na mantiki?
Alisema, saruji ni miongoni mwa bidhaa zilizowekwa katika kundi la bidhaa nyeti, ambazo wazalishaji wa nchi zinakotoka, hupewa ruzuku ambapo wazalishaji wa EAC hawapewi ruzuku hiyo, lakini wanaweza kuzalisha kwa ufanisi.
Hatua hiyo alisema kuwa inachangia katika maendeleo ya viwanda, ajira, mapato ya Serikali na kuokoa fedha za kigeni, ambapo pia kuweko kwa ruzuku kwa wazalishaji wa nje huku wa ndani wakikosa, kunaweka mazingira ya ushindani usio sawa katika soko la Jumuiya dhidi ya wazalishaji wa Afrika Mashariki.
Alisisitiza, kwamba kwa upande wa saruji, kuanzia Januari mosi 2005 ushuru wake ni asilimia 55 na nchi wanachama zilikubaliana ushuru huo ushuke kila mwaka hadi asilimia 35 kuanzia Januari mwaka huu na ubaki katika kiwango hicho.
Alitaja bidhaa zingine katika kundi hili na kiwango cha ushuru kwenye mabano, kuwa ni sukari (100%), mahindi (50%), ngano (35%), mchele (75%), maziwa (60%), tumbaku (35%), sigara (35%), khanga, kikoi, kitenge (50%), mashuka (50%), magunia ya jute (50%), viberiti na betri za redio (35%).
Kwa hiyo kufutwa ushuru si tu kutasababisha viwanda kufa, lakini mapato ya serikali na ajira vitapungua sambamba na uanachama wa Tanzania katika Jumuiya kuwa shakani.
Sina hakika kama misamaha ya kodi inaendana na ahadi dhaifu za elimu na afya bure kwa Watanzania zinazotolewa na wapinzani.
Huwezi kutoa elimu bure na afya bure na wakati huo huo, usamehe ushuru wa forodha, alisema Kamala.
Alisisitiza pia kuwa, hatua ya kupunguza ushuru wa forodha kwenye saruji ilichukuliwa kitambo, lakini kufutwa kukashindikana kutokana na hali halisi iliyobainishwa awali.
Mwaka 2005 ushuru ulikuwa asilimia 55 ukapunguzwa hadi asilimia 25 ya sasa hatua hii ilichukuliwa kutokana na maandalizi ya Kombe la Dunia, Afrika Kusini na Olimpiki, China.
Alisema, wakati huu ambao ushuru kwa muda umeshushwa hadi asilimia 25 huku ikifikiriwa kama utarejea asilimia 35, tayari wazalishaji saruji wameanza kulalamika kuwa wenzao wa nje hususan Misri, wanapata ruzuku na hivyo kuiuza kwa bei ndogo katika Jumuiya.
Kwa maana hiyo kufutwa kabisa kwa ushuru, kutasababisha viwanda kufa na dhana ya kuwapa wananchi saruji ya bei nafuu kufa pia bei ya bidhaa yoyote duniani, hutegemea upatikanaji wake na mahitaji ya soko.
Pindi viwanda vya saruji vya Afrika Mashariki vikifa, wazalishaji kutoka nje ya Jumuiya, watashawishika kupandisha bei, kwa kuwa sasa watakuwa wamejengewa ukiritimba katika soko kwa kukosa mpinzani wa ndani, alisema Waziri.
Katika kampeni zake nchini, mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, Dk Willibrod Slaa, amekuwa akiwaahidi wananchi kuwa akiingia Ikulu atapunguza bei ya saruji hadi Sh 5,000 kwa mfuko wa kilo 50, ili wananchi wajijengee nyumba bora za kisasa.
CHANZO: habari leo tarehe 20/10/2010
Taarifa ya kitaalamu imebaini, kwamba kuna wagombea urais ambao wamekuwa wakiwaahidi Watanzania kuondoa kodi katika saruji watakapochaguliwa kuingia Ikulu.
Taarifa ya Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki, iliyotolewa jana na Waziri mwenye dhamana, Dk Diodorus Kamala, ilisema ahadi hiyo inapotosha wananchi na kuwapa matumaini ambayo hayatekelezeki.
Alisema chini ya kifungu 2(4)(c) cha Itifaki ya Umoja wa Forodha wa Afrika Mashariki, nchi wanachama zilikubaliana kuweka na kutekeleza wigo wa pamoja wa ushuru wa forodha kwa bidhaa zitokazo nje ya Jumuiya.
Aliongeza kuwa wigo huo ulianza kutekelezwa Januari mosi, 2005 na viwango vilivyokubalika ni asilimia 0 kwa malighafi, pembejeo za kilimo, dawa na mitambo; asilimia 10 kwa bidhaa zilizosindikwa kiasi; na asilimia 25 kwa bidhaa zilizokamilika katika uzalishaji.
Kamala alisema, bidhaa nyeti ushuru wake ni zaidi ya asilimia 25.
Hivyo nchi binafsi mwanachama haina mamlaka ya kurekebisha viwango vya kodi ya forodha mfumo wa uamuzi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) hauruhusu nchi moja mwanachama, kufuta ushuru wa forodha wa bidhaa ya aina yoyote ile, ikiwamo saruji.
Alisema, kuwaahidi wananchi jambo ambalo halijakubaliwa na viongozi wa nchi zingine wanachama ni kuwadanganya. Kwa kawaida muungana na mkweli, hatoi ahadi ya jambo ambalo uamuzi au utekelezaji wake unategemea ridhaa ya mamlaka nyingine iliyo juu yake.
Alihoji: Je, ombi la kufuta ushuru likikataliwa na nchi zingine wanachama itakuwaje? Je, mhusika atawarudia wapiga kura na kuwaambia kuwa alitoa ahadi hewa au isiyo na mantiki?
Alisema, saruji ni miongoni mwa bidhaa zilizowekwa katika kundi la bidhaa nyeti, ambazo wazalishaji wa nchi zinakotoka, hupewa ruzuku ambapo wazalishaji wa EAC hawapewi ruzuku hiyo, lakini wanaweza kuzalisha kwa ufanisi.
Hatua hiyo alisema kuwa inachangia katika maendeleo ya viwanda, ajira, mapato ya Serikali na kuokoa fedha za kigeni, ambapo pia kuweko kwa ruzuku kwa wazalishaji wa nje huku wa ndani wakikosa, kunaweka mazingira ya ushindani usio sawa katika soko la Jumuiya dhidi ya wazalishaji wa Afrika Mashariki.
Alisisitiza, kwamba kwa upande wa saruji, kuanzia Januari mosi 2005 ushuru wake ni asilimia 55 na nchi wanachama zilikubaliana ushuru huo ushuke kila mwaka hadi asilimia 35 kuanzia Januari mwaka huu na ubaki katika kiwango hicho.
Alitaja bidhaa zingine katika kundi hili na kiwango cha ushuru kwenye mabano, kuwa ni sukari (100%), mahindi (50%), ngano (35%), mchele (75%), maziwa (60%), tumbaku (35%), sigara (35%), khanga, kikoi, kitenge (50%), mashuka (50%), magunia ya jute (50%), viberiti na betri za redio (35%).
Kwa hiyo kufutwa ushuru si tu kutasababisha viwanda kufa, lakini mapato ya serikali na ajira vitapungua sambamba na uanachama wa Tanzania katika Jumuiya kuwa shakani.
Sina hakika kama misamaha ya kodi inaendana na ahadi dhaifu za elimu na afya bure kwa Watanzania zinazotolewa na wapinzani.
Huwezi kutoa elimu bure na afya bure na wakati huo huo, usamehe ushuru wa forodha, alisema Kamala.
Alisisitiza pia kuwa, hatua ya kupunguza ushuru wa forodha kwenye saruji ilichukuliwa kitambo, lakini kufutwa kukashindikana kutokana na hali halisi iliyobainishwa awali.
Mwaka 2005 ushuru ulikuwa asilimia 55 ukapunguzwa hadi asilimia 25 ya sasa hatua hii ilichukuliwa kutokana na maandalizi ya Kombe la Dunia, Afrika Kusini na Olimpiki, China.
Alisema, wakati huu ambao ushuru kwa muda umeshushwa hadi asilimia 25 huku ikifikiriwa kama utarejea asilimia 35, tayari wazalishaji saruji wameanza kulalamika kuwa wenzao wa nje hususan Misri, wanapata ruzuku na hivyo kuiuza kwa bei ndogo katika Jumuiya.
Kwa maana hiyo kufutwa kabisa kwa ushuru, kutasababisha viwanda kufa na dhana ya kuwapa wananchi saruji ya bei nafuu kufa pia bei ya bidhaa yoyote duniani, hutegemea upatikanaji wake na mahitaji ya soko.
Pindi viwanda vya saruji vya Afrika Mashariki vikifa, wazalishaji kutoka nje ya Jumuiya, watashawishika kupandisha bei, kwa kuwa sasa watakuwa wamejengewa ukiritimba katika soko kwa kukosa mpinzani wa ndani, alisema Waziri.
Katika kampeni zake nchini, mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, Dk Willibrod Slaa, amekuwa akiwaahidi wananchi kuwa akiingia Ikulu atapunguza bei ya saruji hadi Sh 5,000 kwa mfuko wa kilo 50, ili wananchi wajijengee nyumba bora za kisasa.
CHANZO: habari leo tarehe 20/10/2010