Ahadi ya Bilioni 12.3 ya Rais Magufuli kwa Mahakama, kwa ajili ya uendeshaji wa Mahakama yatimia leo

Serikali ya Media...


"Acha kupiga kelele wee, wacha wayaone wenyewe weee.........."



.
 
HIV mnahis hizo bil 12 zmetoka tu bila kujulikana zinaenda kufanya nin na jins gan zitaleta 1tirion kumbuka katika hyo faida mahakama watapewa 25% ya hyo hela so its win win situation hata kama haitafika Ila itazalisha kias fulan ambacho ni kama faida kwenye hyo 12.3 bilion


Kwahiyo Mahakama inafanya biashara na serikali???
 
Hivi hela za kwenye bajeti huwa zinatolewa kwa mbinja? Awamu hii itavunja rekodi za ukurupukaji? Mpanju naye anasema hundi imesainiwa ameionaje?
 
No one is doing exact perfect, only God. Jamaa atakubalika na wote. It is a matter of time.
Hata huyo unayemsema "God" hakubaliki na wote.

Mimi sikubali kwamba yupo.

Huyo jamaa yako ni nani mpaka akubalike na wote?
 
Ninapata mashaka na washauri wa raisi! Unaipelekea mahakama bilioni 12? Ili iweje maana haiwez pandisha mishahara maana hiyo ni kazi ya hazina, sijaelewa itatumikaje hlf inamaana ndo itatua matatizo yote ya mahakama?? Jamaa anapunguza matumizi kwa kufanya matumizi ya ajabu ajabu! Alitakiwa awekeze kwenye vitu vinavyozalisha hela ! Hizo hela watu wanaenda kila tu maana hazieleweki zinaenda kufanya nn!
Na unaitwa Expert Member?
 
Ukawa hawafurahii Magufuli kutekeleza ilani yao ya kwenye webusaiti
 
View attachment 321890 View attachment 321889

Wizara ya Fedha na Mipango imetoa sh.bilioni 12.3 kwa ajili shughuli za mahakama ikiwa ni sehemu ya ahadi ya Rais Dk. John Pombe Magufuli aliyoiahidi katika kilele cha maadhimisho ya siku ya mahakama.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Philip Mpango amesema fedha hiyo imetolewa kwa kutimiza ahadi ya Rais ya uendeshaji wa shughuli za mahakama.

Mpango amesema kuwa ahadi ya Rais ilikuwa ni ya siku tano ambazo zimetimia kwa kutoa hundi ya sh.bilioni 12.3 ambazo zitakwenda kufanya kazi iliyokusudiwa.

Amesema kuwa Wizara ya Fedha na Mipango kutokana na ahadi hiyo imefanya kuweka wazi juu ya fedha hizo kwa waandishi wa habari.

Nae Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Amon Mpanju amesema lengo ni kuongeza kasi kwa mashauri yaliyopo kuondoshwa pamoja na waliokwepa kodi yashughulilikiwe.

Ahadi ya Rais ilitolewa baada ya maombi ya Jaji Mkuu, Othman Chande katika maadhimisho ya kuanza kwa mwaka wa mahakama kudai kuwa wana uhaba fedha za maendeleo katika kuweza kuendesha shughuli za kimahakama.


Chanzo: Michuzi
Sasa haki ya raia itakanyagwa hadi TRILION MOJA ipatikane.Kama ni AIRBUS zinazopatikana kwa njia hiyo mimi sipandi.
 
Sijaelewa vizuri..naomba ufafanuzi hizo Billion 12 zimetoka kwenye budget ipi na je zimepitishwa na bunge..naomba ufafanuzi
 
Hata CT SCan sijui MRI ya Muhimbili tuliambiwa imenunuliwa kwa bil ngapi hata sikumbuki.

Kumbe wamechukua ya Dodoma!

Sasa huo ni mfano wa cheque tu, hatudanganyiki ng'o!

mkuu Raimondi hiyo kitu hata mimi ilinishangaza sana. yaani kuchukua machine kutoka ben mkapa ultra modern hospital na kututangazia kuwa wamenunua!

Unachanganya mambo. Fanya tafiti. Watanzania wengine hawana jema yaani No appreciation kabisa
kama hujui kitu ni bora kunyamaza.
 
Mm nimependa hii aya 'Makahama zetu zikisimama imara, nchi itaenda mbele (Magufuli, John Pombe)
 
Hata huyo unayemsema "God" hakubaliki na wote.

Mimi sikubali kwamba yupo.

Huyo jamaa yako ni nani mpaka akubalike na wote?


Uliza maswali ambayo majibu yake ni magumu. Unauliza magufuli ni nani while unajua ni Rais wa JMT.
 
DSC00942.jpg
 
Hii ni ulimbukeni. Hivi huu ndiyo utakuwa utaratibu wa serikali wa kutoa pesa kwenye taasisi mbalimbali? Killa inapotoa hela itakuwa inaita waandishi wa habari? Huku ni kutafuta simple popularity!

"Hapa kazitu" ni kaulimbiu inayotimizwa kwa vitendo. Hekima, busara na uaminifu ni misingi mikuu ya maadili mema. Mahakama sasa itimize wajibu wake ipasavyo.

TAFARI CHUKUA HATUA
 
Ni sawa na mzazi kumpa ela ya ada mtoto aliyoipanga kuitoa kwenye akiba yake haya maigizo sijui yataisha lini hawe noma kwenye maswala ya Zanzibar mshindi atangazwe
 
Back
Top Bottom