Agongwa na Treni Akichati na Simu Kwenye Reli Dar

nilkarish

Member
Mar 3, 2012
63
22
Kijana Jackson Thobias mwenye umri wa miaka 17 amefariki dunia baada ya kugongwa na treni kwenye maeneo ya kipawa jijini Dar es Salaam. Aligongwa na treni baada ya kutembea juu ya reli huku akichati kwa simu yake na akisiliza muziki kwa kutumia headphone.
Kijana mdogo wa miaka 17, Jackson Thobias, aliyekuwa akisoma kidato cha nne ESACS Academy, amefariki kwa kugongwa na Treni maeneo ya kwao kipawa.
Aligongwa na treni akiwa anatembea juu ya reli huku akiwa anasikiliza muziki kwa headphones huku pia akichati katika simu yake wakati akitembea kwenye reli.
Pamoja na mlio mkubwa wa treni, na juhudi za watu kumpigia kelele kuwa kuna treni inakuja nyuma yake, Jackson hakusikia.
Marehemu Jackson ndiye aliyeshinda kwenye Tokelezeiyer Inter-School concert iliyoandaliwa na group ya Friends 4 Friends mei 12 mwaka huu.
Pia alishinda dougie competition wakati 5select Event ya EATV ilipotembelea ESACS wiki mbili zilizopita.
Alikuwa ni kijana mwenye kipaji na ndoto nyingi katika umri mdogo wa miaka 17. Mungu aipumzishe roho ya marehemu Jackson Thobias kwa amani, Amen.
 
Apumzike kwa amani,ila kwa sasa vijana wamekuwa addicted na headphone yaani hawafanyi kitu bila kuweka hayo ma dude kokote waliko wako nayo wamekuwa wagonjwa kabisa!!!hata wakiwa wanasoma wanavaa hivyo sielewi kama unaweza kusoma na wakati unasikiliza music!!!
 
RIP Jack, u'll be missed.

:crying: :crying:
:crying:
:crying:
:sad:
 
Back
Top Bottom