Agizo la Rais: Watumishi wa Muhimbili waanza kuhamia Wizara ya Afya kupisha wagonjwa wanaolala chini

Interest

JF-Expert Member
Apr 11, 2015
3,434
7,055
12494926_463189047203881_5125711074879422530_n.jpg

12744572_463189043870548_8425244640278726175_n.jpg


Agizo la Rais Magufuli kuwataka watumishi wa Muhimbili kuhama ofisi ndani ya siku mbili ili kuwaachia majengo wagonjwa waliokosa nafasi hospitalini hapo laanza kutekelezwa.

Rais alitoa agizo hilo alipoenda kumjulia hali Mufti mkuu wa Waislamu Tanzania, sheikh Abubakari Zuberi aliyelazwa hospitalini hapo na kukuta mazingira ya wagonjwa wa wodi ya wazazi yakiwa hayaridhishi, ambapo alikutana na malalamiko ya wakina mama waliomfuata na kumueleza kuwa wamekuwa wakilazwa hadi watano kitanda kimoja huku mazingira yakiwa machafu kutokana na maji kuchuruzika kutoka maliwatoni.

Ofisi hizo zilizokuwa zikitumika na watumishi wa wizara ya afya sasa imeagizwa zirejeshwe chini ya Hospitali ya Taifa Muhimbili walau kupunguza tatizo.

Habari na iwafikie..
 
View attachment 323207

View attachment 323208

Agizo la Rais Magufuli kuwataka watumishi wa Muhimbili kuhama ofisi ndani ya siku mbili ili kuwaachia majengo wagonjwa waliokosa nafasi hospitalini hapo laanza kutekelezwa.

Rais alitoa agizo hilo alipoenda kumjulia hali Mufti mkuu wa Waislamu Tanzania, sheikh Abubakari Zuberi aliyelazwa hospotalini hapo na kukuta mazingira ya wagonjwa wa wodi ya wazazi yakiwa hayaridhishi, ambapo alikutana na malalamiko ya wakina mama waliomfuata na kumueleza kuwa wamekuwa wakilazwa hadi watano kitanda kimoja huku mazingira yakiwa machafu kutokana na maji kuchuruzika kutoa maliwatoni.

Habari na iwafikie..
Hapa kazi tu
 
View attachment 323207
View attachment 323208

Agizo la Rais Magufuli kuwataka watumishi wa Muhimbili kuhama ofisi ndani ya siku mbili ili kuwaachia majengo wagonjwa waliokosa nafasi hospitalini hapo laanza kutekelezwa.

Rais alitoa agizo hilo alipoenda kumjulia hali Mufti mkuu wa Waislamu Tanzania, sheikh Abubakari Zuberi aliyelazwa hospotalini hapo na kukuta mazingira ya wagonjwa wa wodi ya wazazi yakiwa hayaridhishi, ambapo alikutana na malalamiko ya wakina mama waliomfuata na kumueleza kuwa wamekuwa wakilazwa hadi watano kitanda kimoja huku mazingira yakiwa machafu kutokana na maji kuchuruzika kutoa maliwatoni.

Habari na iwafikie..
 
Mkuu masahihisho kidogo, ni kwamba hizo ofisi walikuwa wanazitumia watu wa Wizara ya Afya sasa ameagiza jengo lilejeshwe chini ya Hospitali ya Taifa Muhimbili walau kupunguza tatizo.

Sasa mi nimejiuliza hao maafisa wa Wizara 'pepa work zao' hawajaona mahala pengine ndo waende maeneo kama hayo ya hospitali kubana nafasi ilhali nafasi kwa wagonjwa ni haba wana uzalendo kweli?

Aah Rais wetu endelea kunyoosha nchi, akili zitawarudi tu....!
 
Kwa hiyo wewe ulitaka wakina mama waliojifungua waendelee kulala chini?

Kwani miundo mbinu inatoka mbinguni?

Hivi huu ujinga mlijifunzia/mnajifunzia wapi? Nisaidie na mimi nikajiandikishe ili nijifunze ujinga!
Hivi unadhani unawazidi akili hao walioamua kuweka hiyo ofisi hapo ma siyo sehemu nyingine?unafahamu kazi za hiyo ofisi?majukumu yao ya kila siku?

Siyo kosa kuwepo kwa hiyo ofisi, subiri na hiyo wodi itajaa tena, wataamisha ofisi nyingine zilizopo?

Suluhisho ni kujenga wodi kubwa za wazazi zenye miundo mbinu thabiti na timilifu siyo kuhamisha ofisi halafu wagonjwa waanze kufunga safari za wizara ya afya tena

Anyway kasema boss, inapaswa kutekelezwa
 
Back
Top Bottom