Chakaza
JF-Expert Member
- Mar 10, 2007
- 39,794
- 71,214
Werema, madaraka uliyo nayo yanapaswa kushikwa na mtu mwenye weledi wa hali ya juu katika sheria na mtu anayetumia busara katika kila afanyalo au alisemalo. Mwanasheria Mkuu wa Serikali ndiye mshauri mkuu wa serikali katika mashauri yote ya kisheria na hii si kazi ndogo na ni ya heshima kubwa.
Umejitokeza katika kuipotosha serikali na Bunge mara kwa mara kwa kauli zako zinazoonyesha kuwa hata uwezo wako ni wa kutilia shaka kama kweli ulitimiza vigezo vya kupewa hata huo U jaji wa mahakama kuu.
Mbaya zaidi sasa umeanza na kutoa kauli za kihuni kama wakina Lusinde na Mwigulu. Leo katika kupinga hoja ya Lissu umetamka kuwa "Mtu kuwa na nywele sio kuweza kufikiri" ukimaanisha kauli ya Lissu haikutoka kwa mtu mwenye kuikiri.
Haya ni matusi kwa Mbunge aliyetoa hoja muhimu kama ile inayogusa maisha na mashaka makubwa yaliyowapata watanzania katika ajali ile.
Kama serikali(Rais) haiko makini na kuona wewe kiti hicho kimekuzidi (maana waliopita wote hakuwepo mwenye utendaji mbovu kama wako), SASA NI VEMA WEWE MWENYEWE KUJIPIMA NA KUAMUA KABLA HUJAJIWEKEA HISTORIA CHAFU KUWA AG MBOVU KATIKA NCHI HII.
Umejitokeza katika kuipotosha serikali na Bunge mara kwa mara kwa kauli zako zinazoonyesha kuwa hata uwezo wako ni wa kutilia shaka kama kweli ulitimiza vigezo vya kupewa hata huo U jaji wa mahakama kuu.
Mbaya zaidi sasa umeanza na kutoa kauli za kihuni kama wakina Lusinde na Mwigulu. Leo katika kupinga hoja ya Lissu umetamka kuwa "Mtu kuwa na nywele sio kuweza kufikiri" ukimaanisha kauli ya Lissu haikutoka kwa mtu mwenye kuikiri.
Haya ni matusi kwa Mbunge aliyetoa hoja muhimu kama ile inayogusa maisha na mashaka makubwa yaliyowapata watanzania katika ajali ile.
Kama serikali(Rais) haiko makini na kuona wewe kiti hicho kimekuzidi (maana waliopita wote hakuwepo mwenye utendaji mbovu kama wako), SASA NI VEMA WEWE MWENYEWE KUJIPIMA NA KUAMUA KABLA HUJAJIWEKEA HISTORIA CHAFU KUWA AG MBOVU KATIKA NCHI HII.