Afya ya Mgonjwa!

Zamaulid

JF-Expert Member
May 25, 2009
18,653
13,474
wakuu salaam!
naomba kufahamishwa,mimi ninajua kuwa afya ya mgonjwa ni siri ya mgonjwa na Daktari wake!kama ndivyo,je na halali kwa watanzania kutaka kujua hali ya afya ya rais wao!au hiyo ni siri yake na daktari wake?
 
Rais ni lazima afya yake ijulikane bwana, hatuwezi ongozwa na mtu mahututi atashindwa kututumikia vyena.
Kazi ya uraisi ni ngumu, mikiki mikiki ni mingi, na haswa ikitiliwa maanani kuwa zaidi ya 80% wako vijijini ambako lile dege la kifahari la ikulu halifiki.
 
sipingi kuijua afya yake!je tuitumie hiyo kumhukumu?
 
sipingi kuijua afya yake!je tuitumie hiyo kumhukumu?

Rais mwenye afya mbovu hauwezi kutimiza majukumu yake vizuri ndo maana tuko tayari kutumia gharama yeyote ili mradi rais awe na afya njema kutokana na umuhimu wa nafasi yake. Kama afya mgogoro hafai kuchaguliwa. Atafutiwe kazi nyingine
 
Rais mwenye afya mbovu hauwezi kutimiza majukumu yake vizuri ndo maana tuko tayari kutumia gharama yeyote ili mradi rais awe na afya njema kutokana na umuhimu wa nafasi yake. Kama afya mgogoro hafai kuchaguliwa. Atafutiwe kazi nyingine

the question is what can he do?
 
Afya ni mhimu kujulikana mfano, huwezi kuwa dreva kama una matatizo ya macho, kuna dreva alikuwa anaendesha fuso, kifafa kikamdaka, akiwa akiendesha kutokea Magomeni kuelekea Buguruni, kilicho fanyika Lori hilo liliparamia magari madogo na kusababisha vifo.

Kadharika kwa kazi ya Uraisi inabidi apewe mtu mwenye akili timamu na afya njema. Mi naapa JK akishinda uchaguzi, mi ntaenda mahakamani kupinga make huyu mtu anaweza akaingia mikataba ambayo itakuwa "VOID" kwa kisingizio kuwa ana matatizo ya kupoteza fahamu.
 
sipingi kuijua afya yake!je tuitumie hiyo kumhukumu?

Rais kabla ya kutaka dhamana ya kuongoza watu, anatakiwa awe na udhati wa mawazo wa kukubali kwamba kazi ya urais ni kazi yenye mikiki mingi na haitaki mtu mwenye matatizo ya afya.Na kama ni mkweli, na ana mapenzi ya dhati kwa wananchi, na anajua ana matatizo ya afya, hatataka kuliingiza taifa katika kizungumkati kwa sababu ya matatizo yake ya afya na kutaka utawala bila kuwajali wananchi.

Kwa hiyo rais anapohukumiwa, si kwamba anahukumiwa kwa sababu ana afya mbaya, bali anahukumiwa kwa sababu anataka kuwa rais hata baada ya kujua kwamba ana afya mbaya.

Ni kama baba anayejua kwamba anaweza kuzimia wakati wowote, lakini bado anataka kuendesha gari akibeba familia yote, ingawa kuna watu wengine wana uwezo wa kuendesha gari. Baba huyu ataonekana hawezi kuachia uongozi, anafikiri hakuna mtu mwingine anayeweza kuendesha gari ila yeye tu.
 
wakuu salaam!
naomba kufahamishwa,mimi ninajua kuwa afya ya mgonjwa ni siri ya mgonjwa na Daktari wake!kama ndivyo,je na halali kwa watanzania kutaka kujua hali ya afya ya rais wao!au hiyo ni siri yake na daktari wake?

Kwanza kabisa napenda nikuhakikishie kuwa suala la afya ni siri kati ya mtu na daktari, hadi pale kutakapokuwepo na 'consent' miongoni mwao.
Lakini pia uelewe kuwa kuna kiwango cha umaarufu au hadhi '' fame /celebrity status'' ambacho mhusika anapoteza baadhi ya hifadhi zake ''private life' si kwa kupenda bali kutokana na mazingira. Pia ukumbuke kuwa ni jamii kwa wakati fulani inalipia gharama zinazoambatana na umaarufu au hadhi. Kwa mfano Rais analipiwa matibabu popote atakapo tena kwa maisha yake yote hata akistaafu. Ni kutokana na haki hizi Rais huyo huyo anapoteza ''privacy' yake. Raia watakuja juu sana kama wakisikia Rais wao ametibiwa Uwanja wa fisi na drip fake, na ndiyo hiyo hali inaoyondoa privacy yake kidogo kidogo.
Rais au viongozi ni watu wenye siri na mambo mengi yanayohusu usalama wa taifa. Kunapotokea jambo ambalo linazua hofu na mashaka kuhusu afya yake basi taifa linapatwa na kihoro. Mfano Rais Bush[baba] alipoanguka katika state banquet kule Japan, siku iliyofuata masoko yalipoteza thamani kwa kihoro. Hata sasa hivi kutokana na uchaguzi usiokamilika kule Australia masoko ya ndani na nje yanayumba kwa kutojua hatima ya PM ajaye. Hii nataka nikuonyeshe kidogo umuhimu wa viongozi kitaifa. Ili kuondoa sintofahamu na taharuki kuna wakati Rais analazimika kupotea ''privacy' yake kwa ajili ya Taifa, na hapa ndipo siri inapokuwa si siri tena.

Mwisho, kumbuka kuwa bado kiongozi au mtu maarufu anabaki kuwa na haki ya kutotaja tatizo, ila akasema anaumwa inatosha. Itakapotokea kwa kiongozi kama Rais wananchi wanaweza ambiwa kuwa kiongozi huyo hawezi au anaweza kuendelea na kazi kulingana na afya yake, lakini inakuwa imekwenda mbali sana kama umma unataka kujua anaumwa nini. Kwahiyo suala la privacy katika fame au celebrity status ni ngumu sana ku maintain hasa zama hizi za majarida ya udaku na upaparazi.
Kwa kiwango wananchi wanalipia kodi kwa ajili ya maisha mazuri yenye furaha ya viongozi na familia zao, basi viongozi hao hao wanawajibu kwa wananchi, na moja ya hilo ni kupoteza hata sehemu ya uhuru wao '' private life''. Jibu la swali lako lipo katika Logics zaidi kuliko YES or NO.
 
Kama umepita viwango mbalimbali vya elimu (mashuleni, vyuoni) na ajira utakuwa umeshadaiwa medical check up reports mara nyingi. Ukitaka magonjwa yawe siri yako na daktari usitafute kazi ya kuajiriwa - ambacho ndicho anachofanya Rais.
 
Ni muhimu kujua afya yake kwa kuwa kodi zetu zinatumika katika matibanu yake. Lakini Pia tujifunze yaliyotokea Nigeria baada ya kumchagua marehemu Yaradu ....... nchi ilikaa miezi 3 bila rais kwa kuwa marehemu mtarajiwa alikuwa Saudi Arab akipata matibabu na mipngo nchini mwake illikuwa haieleweki. ..... Hatimaye mzee wa lose balls Goodluck Jonothan kuikwaa ikulu ya Nigeria
 
Back
Top Bottom