Mbonea
JF-Expert Member
- Jul 14, 2009
- 640
- 20
</SPAN>
Sunday, November 08, 2009 4:01 AM
Mwanamke nchini Uingereza amefariki kwa kusagwasagwa na treni baada ya kujilaza kwenye reli wakati treni iliyokuwa kwenye spidi ikikatiza zikiwa ni siku tatu tu baada ya baba yake kujiua sehemu hiyo hiyo na kwa staili hiyo hiyo.
Colleen O'Connor, 39, alikutwa amefariki juu ya reli mwili wake ukiwa umesagwasagwa na treni baada ya kujilaza juu ya reli katika kitongoji cha Kidderminster, Worcestershire.
Colleen aliamua kujiua siku tatu baada ya baba yake Barney O'Connor, 64, kujiua kwa kujilaza kwenye reli wakati treni ikikatiza.
Colleen alijiua katika eneo la reli hiyo ambalo baba yake alijiua siku tatu zilizopita.
Baba yake Colleen inaaminika aliamua kujiua baada ya ndoa yake kuvunjika na mkewe kuolewa na mwanaume mwingine.
Taarifa zilisema kwamba Colleen alisafiri kutoka nyumbani kwake katika mji mwingine wa Dorset hadi katika eneo ambalo baba yake alijiua na yeye pia kujiua kwa njia ile ile aliyoitumia baba yake.
Taarifa iliyotolewa na familia ya O'Connor ilisema kwamba wamehuzunishwa na vifo hivyo na walivitaka vyombo vya habari viwape nafasi ya kuombeleza kwa kukaa mbali na eneo ambalo waombelezaji wamekusanyika.
Bwana OConnor alifariki baada ya kugongwa na treni alipojilaza kwenye reli siku ya alhamisi oktoba 29 kwenye majira ya saa 12 na nusu jioni.
Colleen alijiua kwenye eneo hilo hilo siku ya jumapili novemba 1 kwenye majira ya saa mbili na nusu usiku.</SPAN>
Source: NIFAHAMISHE
Sunday, November 08, 2009 4:01 AM
Mwanamke nchini Uingereza amefariki kwa kusagwasagwa na treni baada ya kujilaza kwenye reli wakati treni iliyokuwa kwenye spidi ikikatiza zikiwa ni siku tatu tu baada ya baba yake kujiua sehemu hiyo hiyo na kwa staili hiyo hiyo.
Colleen O'Connor, 39, alikutwa amefariki juu ya reli mwili wake ukiwa umesagwasagwa na treni baada ya kujilaza juu ya reli katika kitongoji cha Kidderminster, Worcestershire.
Colleen aliamua kujiua siku tatu baada ya baba yake Barney O'Connor, 64, kujiua kwa kujilaza kwenye reli wakati treni ikikatiza.
Colleen alijiua katika eneo la reli hiyo ambalo baba yake alijiua siku tatu zilizopita.
Baba yake Colleen inaaminika aliamua kujiua baada ya ndoa yake kuvunjika na mkewe kuolewa na mwanaume mwingine.
Taarifa zilisema kwamba Colleen alisafiri kutoka nyumbani kwake katika mji mwingine wa Dorset hadi katika eneo ambalo baba yake alijiua na yeye pia kujiua kwa njia ile ile aliyoitumia baba yake.
Taarifa iliyotolewa na familia ya O'Connor ilisema kwamba wamehuzunishwa na vifo hivyo na walivitaka vyombo vya habari viwape nafasi ya kuombeleza kwa kukaa mbali na eneo ambalo waombelezaji wamekusanyika.
Bwana OConnor alifariki baada ya kugongwa na treni alipojilaza kwenye reli siku ya alhamisi oktoba 29 kwenye majira ya saa 12 na nusu jioni.
Colleen alijiua kwenye eneo hilo hilo siku ya jumapili novemba 1 kwenye majira ya saa mbili na nusu usiku.</SPAN>
Source: NIFAHAMISHE