African Unity: Did Nyerere frustrate Nkrumah's Pan-Africanist Visions?

Kosa jingine kubwa ni kujenga Taifa la wananchi waoga katika kila jambo hata katika kujua haki zao za msingi, hivyo kuzalisha jamii ya watu wasiowabunifu katika kuyakabili maendeleo binafsi.
 
Mkuu sahiba heshima mbele.
Tuko pamoja katika hili kama kunakosa ambalo nyerere alilowatendea watanzania ni hili la kutubandikia fisadi Mkapa.Kosa lingine kubwa ambalo bado litaendelea kututesa kwa muda mrefu ni kutengeneza katiba iliyomfanya rais wa Tanzania kuwa mungu mtu.

Mwalimu alikuwa na KURA ngapi kwenye CC, NEC na Mkutano Mkuu wa CCM wakati wa uteuzi wa Mkapa? Mkapa alitubadilikia sana baada kifo cha Mwalimu.
 
Chuki binafsi zitatupeleka pabaya....Waafrika tuna tatizo moja kubwa sana na bila kujirekebisha hatuendi popote katika dunia ya sasa, Tatito hilo hatujui ku- appreciate kiswahili chake naomba mnisaidie.

Katika khali yeyote tu nimeona hata kati ya ndugu,marafiki,na wale wanaosoma pamoja kama mwenzao akifanikiwa darasani/au katika maisha huwa response yake vijembe,vibezo na wakati mwingine anatengwa kabisa.

Hao mnaombeza nyerere ni chuki binafsi kwangu mimi nakubali nyerer alikuwa na matatizo yake lakini mazuri aliyoyafanya ni astounding.Hongera kwake...katika generation yake na generation ya marais wa kwanza wa africa alikuwa among the best na Tanzania tunajulikana au tunakubalika kwasababu ya yeye.

hakumfrastrate yeyoye! wala kwame Nkrumah hakuwahi kuwa frustrated labda kama mna reference.Hiyo yalikuwa mawazo yake na ni democrasia ilitendeka.

Je kikwete ame frustrate Gaddafi kwa kucomment total goverment haitawezekana kwa sasa?
 
je kikwete amemfrustrate gaddafi kwa comment yake ya total african government haiwezekani haraka kma gadaffi alivyopendekeza?
 
Mwalimu alikuwa na KURA ngapi kwenye CC, NEC na Mkutano Mkuu wa CCM wakati wa uteuzi wa Mkapa? Mkapa alitubadilikia sana baada kifo cha Mwalimu.

Mkuu WildCard heshima mbele.

Mwalimu Nyerere alitumia udhaifu wa serekali ya mzee Ruksa ,wanaCCM na wananchi wakati huo kuhakikisha anamweka mtu wake.Mpaka leo napata taabu kubwa kuamini Mkapa alishinda kihalali uchaguzi wa kumtafuta mgambea urais ndani ya chama cha mapinduzi.Kwamba Mkapa alibadilika baada ya kifo cha Nyerere sidhani kama kuna ukweli katika jambo hili isipokuwa ninaamini huu ni mkakati maalumu kuhakikisha nyerere anawekwa mbali na ufisadi wa Mkapa ili kufanikisha mkakati wa kumfanya Nyerere mtakatifu.Dhambi hii ni rahisi kuiondoa kwa watanzania ambao wana sifa moja kubwa ya kusahau haraka.
 
Hamna ushirika kati ya Nyerere Kumuweka Mkapa Na Mkapakuwa Fisadi.

Hata kama Nyerere alimuweka Mkapa kwa Influence yake Kabla ya hapo mkapa hakuwahi kuwa fisadi.

Mnatafuta makosa tu Mbona hamlaani Nyerer kumuweka Mwinyi? maana aliwaweka wote au kwa akili yako mwnyi angekuwa Rais bila ya influence ya Nyerere?

Acheni chuki zisizo na mbele wala nyuma maana najua hakuna corellation kati ya kumuweka Mkapa na Mkapa kubadilika kawa Fisadi.

Naomba muangalie mambo katika taswira kubwa na uchambuzi wa ndani usio na upendeleo. Au hujui Chiluba alimuweka Meanawasa, Muluzi alimuweka Bingu wa mutharika na mifano mingi sana swali ni je kunauhusiano kuwaweka na wao kubadilika na kuwafanyia mizengo hadi kutaka kuwafunga?
 
Katika historia ya Dunia hakuna mtawala aliyewahi kufanya maamuzi yakawa sawa 100% au yakawapendezesha wote. Labda kama mnamfahamu mniambie Nkurumah vile vile alikuwa na matatizo yake...Soma Historia zaidi na utaafiki kwa maelezo hayo basi tukubali Nyerer hakuwa kamili pia ila kuna watu ambao walitaka nyerere sikosea hata kitu kimoja..sasa hiyo haiwezakani lakini katika ulinganisho wa mwisho mazuri ya nyerere yanazidi mabaya aliyotenda na ni viongozi wachache sana wa kiafrika wakati huo unaweza kuwaweka katika mizani sawa na nyerere. He was extraordinary on the other was he was not ordinary.

Kuhusu Umoja wa Afrika Nyerere pekee hawezi kulaumiwa na hapa ninamaanisha hata angekuwa upanda wa nkrumah haimaanishi umaja wa afrika ungeafikiwa. Je labda uniambie kama walipiga kura ratio ya proposing na opposing ulikuwa ngapi? sasa kwa nini kelele hizi? Nyerere ,..nyerere kila siku .Huyo Nyerere hakuwa Mungu na hata angeunga mkono kula yake ilikuwa ni moja tu na haimaanishi vilevile huo muswada ulishidwa kwa kula moja.

Nyerere asilaumiwe labda mlaumu kizazi chote cha utawala kipindi hicho. Halafu Winston Churchil alisema ' Ukianzisha ufitini kati ya wakati huu(present) na uliopita (past)uko kwenye hatari ya kushindwa wakati ujao(future). Ndugu tuangalie mbele, Tuangalie Je Gaddaffi ataweza? Kikwete atasaidiaje? na marais wengine watasaidiaje na Je itawezekana? au ni day dreaming?


Suala si kuwa kamili or 100% right suala ni kuangalia position za Mwalimu katika maamuzi yake si makosa ni maamuzi ya makusudi kabisa kuanzia kwenye uhuru,Biafra,Azimio la Arusha,Umoja wa Africa,Uhujumu uchumi,Mauaji ya Zanzibar 1964,Vita ya Kagera,Uteuzi wa Mkapa,Kifo cha Sokoine n.k.Ukiachilia mbali civil war za nchi ngapi za Africa ambazo Mwalimu ni architect,then everybody knows how inteligent he was and you still call this mistake ? May be we need a therapist to open our eyes because we can help ourself.

SAHIBA.
 
We need a therapist to open our eyes because we can not help ourself.Nyerere kumuweka Mwinyi kwake yeye ilikuwa mistake if you don't get it.Nyerere aliamini Mwinyi angemtukuza na angekuwa kibaraka wake and thank GOD for the different result,Kwa maono yake Mwinyi alimsaliti ingawa wananchi walifaidika na usaliti ule thanks Mzee Rukhsa,then Mwalimu had no choice than to come back na kurudisha sera zake.And that's where fisadi Mkapa fits in.

SAHIBA.
 
Kosa jingine kubwa ni kujenga Taifa la wananchi waoga katika kila jambo hata katika kujua haki zao za msingi, hivyo kuzalisha jamii ya watu wasiowabunifu katika kuyakabili maendeleo binafsi.
Mahmoud,
Nifahamishe utajengaje taifa la watu waoga? Yaani Nyerere alikuwa na uwezo wa kushika akili za kila mtu? Leo karibia miaka 10 tangu Nyerere aondoke duniani mbona wajasiri sijawaona? Kiongozi yeyote hawezi kumfanya mtu awe mbunifu. Ubinifu ni hulka. Tafuta kisingizio kingine cha kumhukumu Nyerere.
 
Jasusi kwa maoni yako unafikiri wakati wa Nyerere watu kama Mengi wangeexist ?
 
Jasusi kwa maoni yako unafikiri wakati wa Nyerere watu kama Mengi wangeexist ?
Sahiba,
For your information Mengi alikuwepo wakati wa Nyerere. Hakuwa na utajiri alionao hivi sasa lakini alikuwepo na alikuwa katika hali nzuri tu. Kamuulize!
 
I don't agree with the editor above about the frustrating the process of formation the African unity as the editor wants us to believe. Mw. Nyerere and Dr. Kwame Nkrumar has the same vision regarding the African unity but in different perspectives/approaches.

While Dr. Nkrumar wanted to unite the 53 Africans nations overnight, Mw. Nyerere was of the opinion that th process shouldn't be rushed. He suggested that instead, the countries had first to unite at the regional levels.
 
Sahiba,
For your information Mengi alikuwepo wakati wa Nyerere. Hakuwa na utajiri alionao hivi sasa lakini alikuwepo na alikuwa katika hali nzuri tu. Kamuulize!


Jasusi hata mimi na wewe tulikuwepo kimya na mipira yetu miguuni na ugari wetu wa yanga nina maana hakuna aliyethubutu kuzungumza against serikali.

SAHIBA.
 
Mahmoud,
Nifahamishe utajengaje taifa la watu waoga? Yaani Nyerere alikuwa na uwezo wa kushika akili za kila mtu? Leo karibia miaka 10 tangu Nyerere aondoke duniani mbona wajasiri sijawaona? Kiongozi yeyote hawezi kumfanya mtu awe mbunifu. Ubinifu ni hulka. Tafuta kisingizio kingine cha kumhukumu Nyerere.

Mtoto anapozaliwa ubongo wake unakuwa mtupu hauna kitu chochote, hivyo mazingira na walezi ndio ambao humfanya mtu akawa alivyo.
Hivyo Nyerere alipochukua nchi alianza na kuandaa mazingira ya wananchi kuiona serikali na raisi wake ni waungu watu. huwezi kusema lolote baya kuhusu seriakali kabla hujapelekwa uhamishoni kama sio kufichwa pabaya.
Siasa ikafundishwa na watu wakatiwa woga wa kutojihusishwa na shughuli binafsi zaidi ya mambo ya kijamaa na ushirika. hununui chochote bila kibali cha serikali, habari haitoki bila kufanyiwa editing kuondosha vinavyoweza kujenga ujasiri wa wananchi wasije ungana nguvu dhidi ya serikali. kuna mengi ndugu kama ulikuwa hujazaliwa hebu take time waulize wazee wakwambie hali ilikuwaje siku hizo na serikali ilikosolewa vp ama watu walikuwa wanazungumza vp kuhusu serikali.
 
Kaka naona we unachuki binfsi na nyerere,

Mimi niliuliza Kama nyerere akilaumiwa kwa mfrustrate Nkruma Je kwanini kikwete asilaumiwe kwa Kumfrastrate Daddafi? Maana last week wote tulisikia Gaddafi akisema anapenda Afrika Union Goverment ianzishwe mapema iwezekanavyo na pesa ya pamoja bali Kikwete (predecessor wake ) alipoulizwa alisema wazi wazi kwa sasa haitawezekana . Je alaumiwe Kikwete au unataka ujirizishe Nyerere akilaumiwa tu au sio.

Huwezi kumconvince Mtanzania yeyote elite na mwenye mtazamo chanya na mapenzi na nchi yake kuhusu hili na kuhusu nyerere. Tafuta Magaidi wanaoongozwa na imani bila kufikiri na mtazamo hasi nafikiri utafanikiwa kuwaconvince.

Viva Nyerere of Tanzania.
 
Mkuu sahiba heshima mbele.
Tuko pamoja katika hili kama kunakosa ambalo nyerere alilowatendea watanzania ni hili la kutubandikia fisadi Mkapa.Kosa lingine kubwa ambalo bado litaendelea kututesa kwa muda mrefu ni kutengeneza katiba iliyomfanya rais wa Tanzania kuwa mungu mtu.
Nimejaribu sana kuwa neutral ili niweze kukuweka katika mzani gani wewe SAHIBA ila nadhani kuwa fair naweza kusema una"KAUJINGA" fulani ka historia ya Africa....thts is much fair i can be
 
Back
Top Bottom