mshikachuma
JF-Expert Member
- Dec 2, 2010
- 2,853
- 626
Wakuu nilikuwa nawatch CNN ya Marekani, nikamkuta yule tajiri number 2 duniani (Bill Gates) akiwa analiongelea bara la Africa kwa ujumla. Mwandishi wa CNN alimuuliza Bill Gates....kwa nini bara la Africa liko nyuma kwa kila kitu? tatizo ni nini?....Eti Bill akasema matatizo yako mengi sana, lakini makubwa sana ni -:
1.Kwanza walitawaliwa kwa mda mrefu
2.Elimu duni
3.Viongozi wa Afrca wanapenda kung'ang'ania madarakani
4.Demokrasia yao ni mdomoni tu.... na si matendo
5.Na vita za wenyewe kwa wenyewe zisizoisha.
Na mwisho akasema eti itachukua takribani miaka 500 bara la Africa kuwa kama America (Marekani) na Ulaya. Akaendelea kusema miaka 500....Africa watakuwa na siasa safi na uongozi bora, watu watakuwa educated, kutakuwa na viwanda vikubwa vya kutengeneza kila kitu, huduma safi za afya, barabara za juu, viwanja vizuri vya michezo yote, kutakuwa na timu kama Arsenal, Manchester, Real madrid nk. na vita za kung'ang'ania madaraka hazitakuwepo tena.
Kusema kweli mimi binafsi nilichoka na almanusra nidondoke chini kwa maneno ya huyu Bill Gates.....Yaani yameninyong'onyesha kabisaaa!.....miaka 500?
Hebu wanaJF tusaidiane tusaidiane kutafakari maneno ya huyu tajiri.... Je, kaongea kweli au uongo? - Nawasilisha
1.Kwanza walitawaliwa kwa mda mrefu
2.Elimu duni
3.Viongozi wa Afrca wanapenda kung'ang'ania madarakani
4.Demokrasia yao ni mdomoni tu.... na si matendo
5.Na vita za wenyewe kwa wenyewe zisizoisha.
Na mwisho akasema eti itachukua takribani miaka 500 bara la Africa kuwa kama America (Marekani) na Ulaya. Akaendelea kusema miaka 500....Africa watakuwa na siasa safi na uongozi bora, watu watakuwa educated, kutakuwa na viwanda vikubwa vya kutengeneza kila kitu, huduma safi za afya, barabara za juu, viwanja vizuri vya michezo yote, kutakuwa na timu kama Arsenal, Manchester, Real madrid nk. na vita za kung'ang'ania madaraka hazitakuwepo tena.
Kusema kweli mimi binafsi nilichoka na almanusra nidondoke chini kwa maneno ya huyu Bill Gates.....Yaani yameninyong'onyesha kabisaaa!.....miaka 500?
Hebu wanaJF tusaidiane tusaidiane kutafakari maneno ya huyu tajiri.... Je, kaongea kweli au uongo? - Nawasilisha