deadteja
JF-Expert Member
- Aug 8, 2011
- 379
- 84
Taarifa nilizozithibitisha muda huu ni kwamba Afisa Mtendaji Kata ya Tandale, anayejulikana kwa jina la Katula, ameng'ag'aniwa na vijana wanaodai kulipwa haki zao kwa ajili ya semina ya zoezi la sensa. Vijana hao ambao inasemekana wanadai hela zao hizo ambazo ni 245,000/- kila mmoja, yaani 35,000/- kwa kila mmoja kwa muda wa siku saba. Inasemekana vijana hao walimkwida na kumvua shati lake la kaunda, na alibakiwa na 'slinglet' na kuanza kumburuza kuelekea Wilayani Magomeni toka maeneo ya shule ya sekondari Kambangwa. Naendelea kufuatilia.