Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,956
- 22,148
Afisa Magereza aacha kazi aolewe na mfungwa mbakaji
Alison kushoto na Royston Wednesday, February 04, 2009 6:01 AM
SRC-NIFAHAMISHE.COM
Alison kushoto na Royston Wednesday, February 04, 2009 6:01 AM
Afisa magereza wa gereza moja nchini Uingereza ameacha kazi yake ili aolewe na mwanaume ambaye alifungwa katika gereza alilokuwa akifanya kazi kwa makosa ya ubakaji.
Afisa magereza huyo aliacha kazi yake na kununua nyumba ili waishi pamoja na mpenzi wake ambaye alifungwa kwa makosa ya ubakaji.
Alison Uyanik alinunua nyumba pamoja na Royston Wells baada ya kuangukia kwenye mapenzi wakati Royston alipokuwa akitumikia kifungo chake jela.
Alison mwenye umri wa miaka 41 ambaye aliachika na mumewe miaka kadhaa iliyopita, aliangukia katika mapenzi ya mbakaji huyo wakati akitumikia kifungo katika jela ya Whatton iliyopo Nottinghamshire, Uingereza ambayo wafungwa wanaume wa makosa ya ubakaji hufungwa jela hiyo.
Wapenzi hao walinunua nyumba katika mji anaokaa Alison na walihamia kwenye nyumba hiyo muda mfupi baada ya Royston kuachiwa huru kuendelea na kifungo cha nje mwaka jana.
Marafiki wa Alison walipigwa na butwaa na kusema kwamba Alison ameitupa kazi nzuri yenye mshahara mzuri na marupurupu kibao.
"Royston amekuwa akijitetea kwamba hakutenda kosa la kubaka, lakini hakuna hata mmoja kati yetu anayeweza kujua ni nini hasa Alison alikigundua kwa Roy mpaka kuamua kuolewa naye" walisema rafiki zake.
Chanzo cha magereza kilisema kwamba uchunguzi uliofanyika haukugundua wapenzi hao kufanya mapenzi ndani ya gereza hilo.
Wazazi wa Alison walikuwa hawajui kwamba Royston mwenye umri wa miaka 37 aliwahi kuhukumiwa kifungo kwa kosa la kubaka kwakuwa Alison aliwaongopea wazazi wake kwamba alikutana na Royston katika sherehe moja mjini humo.
SRC-NIFAHAMISHE.COM