Ambassador
JF-Expert Member
- Jun 2, 2008
- 933
- 75
Wadau, kuna issue serious kidogo toka kwa best yangu mmoja. Ameanza kazi katika shirika fulani na hapo katika ofisi yake mpya amebahatika kumkuta dada mmoja mrembo sana ambaye ana vigezo vyote anavyovipenda mshikaji wangu. Akiwa katika kujizoeza na yule dada wafanyakazi wenzake wamemstua kwamba hapo anacheza na moto kwani huyo binti ni muathirika. Anasema amefuatilia stori za huyo dada kwa watu tofauti tofauti na anapata the same story.
Mshikaji kapagawa na anajipa moyo kwamba kwa kuwa ameshafahamu status ya huyo dada anaona bora endelee nae tu na atahakikisha anajilinda vema asiathirike.
Nimeshindwa kumshauri la maana huyu mshikaji wangiu kwani nilipomuuliza kama ana uhakika na analolifaya amesema "kwani mtu mwenye UKIMWI hana haki ya kuwa na mpenzi?" Nikaishia kumwambia atafakari kwa makini na awe mwangalifu maana "mambo ya rohoni" ni mtu mwenyewe anayependa. Sio baadae aanza kulaumu watu "mlinishauri vibaya".
Mwenzetu kafika bei, wadau mnasemaje?
Mshikaji kapagawa na anajipa moyo kwamba kwa kuwa ameshafahamu status ya huyo dada anaona bora endelee nae tu na atahakikisha anajilinda vema asiathirike.
Nimeshindwa kumshauri la maana huyu mshikaji wangiu kwani nilipomuuliza kama ana uhakika na analolifaya amesema "kwani mtu mwenye UKIMWI hana haki ya kuwa na mpenzi?" Nikaishia kumwambia atafakari kwa makini na awe mwangalifu maana "mambo ya rohoni" ni mtu mwenyewe anayependa. Sio baadae aanza kulaumu watu "mlinishauri vibaya".
Mwenzetu kafika bei, wadau mnasemaje?