Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Nilikuwa na msichana
wa kazi niliyeishi naye kwa miaka 5. Kwa bahati mbaya hana wazazi wala
ndugu anayeweza kumsaidia au kumtegemea kwa lolote. Mwaka jana alipata
mimba na nilipomhoji kijana aliyempa mimba alikubali na kuamua
kumchukuwa na kuishi naye kwa tabu kwani Bwana hana kazi, ni mtu wa day
waka tu.
Jana msichana ananipigia simu na kunieleza kuwa Bwana wake amejiunga na
Kikundi cha Uamsho na ametoa amri inayomtaka Mdada kubadili dini
(alikuwa Mksristo) mara moja la sivyo aondoke na mtoto wake wa miezi
miwili. Mdada hana pa kwenda na hayuko tayari kubadili dini.
Nishaurini nimwambie afanye nini?