Adhabu ya viboko mashuleni - should it be abolished?

Haika

JF-Expert Member
Mar 3, 2008
2,348
559
Naomba maoni yenu na ushauri.

Je ni vizuri au vibaya kumchapa mtoto anapokosea? kwa nini?

je ni vizuri au vibaya kumpa adhabu mtoto anapokosea?

je kuelimisha na kueleza madhara ya kosa kunatosha?

Mimi nilikuwa nachapwa na kupewa adhabu nyumbani na shuleni kadiri wazazi na walimu walivyoona inafaa.

Sasa hivi imeonekana si vyema kuwaumiza watoto na ni budi waelimishwe.

Baada ya kusoma taarifa moja ya mfungwa aliyehukumiwa kifungo, kazi na viboko ilibidi nijiulize, mara kadhaa na kuanza kuwa na mashaka na uamuzi wa kuacha kuwafanyia hivyo watoto wakiwa bado wadogo.

Je, 'mkunje samaki angali mbichi' bado ni msemo unaofaa kwa sasa?

Je kama mtoto anapokuwa mkubwa atapewa adhabu hizohizo kutoka kwa jamii, je mimi kama mzazi, au mwalimu, nikianza kumwonyesha kwa upendo na kumkosoa na kumwelekeza kukiwa kumeandamana na kiboko na adhabu si nitakuwa nimemjenga mapema?

Mzazi au mwalimu anatakiwa amjue mtoto tabia udhaifu na afya yake kwa hiyo adhabu ni rahisi kuipangilia kwa makini zaidi kuliko mahakama ambayo hakuangalii ulikotoka, wanchoangalia ni kosa tu.

Naomba ushauri.
 
Mtoto anapokosea kumuadhibu kwa kumchapa viboko sio adhabu nzuri. Mzazi unachotakiwa kufanya unatakiwa kumuonyesha mwanao uzito wa kosa alilolifanya ili na yeye atambue kosa lake kwa kufanya hivyo utamuondolea uoga na utamjengea mtoto wako kujiamini na kuwa na upendo kwa wazazi wake.
 
ina maana mtoto hatakiwi kuwa na woga? Hatakiwi kupata maumivu?
mimi nadhani kuna vitu ambavyo anatakiwa pamoja nakujua au kutokujua madhara yake ni lazima aviogope.
Ni lazima pia mtoto ajifunze kuwa duniani pia atakapokuja kufanya makosa ataadhibiwa kwa kupatiwa maumivu.
 
Asante dada Haika kwa kuibua mada hii.
Kwa hakika mada hii ni tete siku hizi kutokana na wanaharakati wa jinsia pamoja na wale wa kutetea haki za mtoto wanvyokuja juu. Wenzetu katika nchi za kimagharibi mtakubaliana nami kwamba suala hili wala halina mjadala kwa vile sheria imepitishwa ya marufuku kumchapa mtoto. Sisi katika Tanza bado tuna nafasi ya kujadili hili kabla ya sheria hii ya kutochapa watoto haijapitishwa.

Kwa maoni yangu, nadhani fimbo ni muhimu sana katika malezi ya mtoto lakini hekima ya namna ya kuadhibu ndiyo muhimu zaidi. Kwanza mtoto achapwe na mlezi/mzazi au mwalimu tu na sio kila mtu kweye familia. Pili mtoto aeleweshwe kwa nini anastahili adhabu hiyo wakati huo. Tatu mtoto achapwe katika mazingira yasiyomuathiri kisaikologia yaani asidhalilishwe bali aadhibiwe kwa mfano ukimchapa mtoto mbele ya watu unamdhalilisha na unamuondolea ujasiri(self esteem and confidence). Nne idadi ya fimbo iendane na kosa lenyewe na Tano unapomuadhibu mtoto hakikisha huna hasira inayowaka ndani mwako, ni afadhali usimuadhibu hadi upoe hasira ili usijekumuua bure au ukamchapa hadi akakuona wewe ni mnyama

Those are my few cents!!!
 
Nakubaliana na wewe kabisa katika yote hasa pale pa kutokuwa na hasira unapomchapa mtoto.
Ni budi mzazi/mlezi amuadhubu mtoto kwa lengo la kumuelimisha si kwa lengo la kumalizia hasira zake. (nadhani hapo ndio panapofanya watu wapendekeze iondolewe)
Lakini tukumbuke maumivu kwa kuimbe ni jambo la lazima, na mtoto inabidi ajifunze tangu totoni.
 
Sidhani kama kuchapa ni solution especially that sikuhizi watoto wengi wamekuwa kama broilers yani unaweza kumchapa ukaambulia mengine usiyoyatarajia ... ni kuhatarisha maisha yenu wote

Mimi kama mama ... nina my own way with my kids .. I secured the reputation of their best friend ... sasa in this position wa/mwanangu akikosa ... my biggest punishment ni psychological punishment.. the child in question namuonya if its the 1st time offense .. 2nd time then amezoea .. what i do is that namwambia kwamba kakosa tena 2nd time halafu nam ignore .. simsemeshi ... simfurahii .. akija huku nimekaa na wenziwe nawaambia tunyanyuke .. wengine will enjoy a lot of pampering , outings ... fake hugs and kisses na sifa kemkem na vijizawadi .. yeye hata salamu simwitikii .. yani namuonyesha kabisa sina time naye ...akiomba hela kama ni ya shule namcheleweshea up to even a day .. wengine nawapa immediately ... in time mtoto anajirudi ili kukwepa adhabu ya kutengwa ... i do this purposely ajuwe kwamba nimekasirika ... it really works with me .. kwani i dont have to cain anyone. they are even cautious wanaonyana na wanaambizana usimuudhi mama shauri yako...

In instances za kuwa mwalimu ... ndiyo kabisa usimchape mtoto wa mtu ... give them punishment za kusweep the class/ compound , pick litter na kadhalika .. mtoto akizidi utundu the best way nikumshirikisha mzazi wake ...call the parent .. akiamua kumchapa fine but dont do it
 
hata mimi kuna wakati natumia technics karibu kama zako. ila kuna wakati huwa inahitajika mtoto aliogope lile kosa, kwa hiyo pamoja na elimu husika, huwa naongeza adhabu, au nafinya.
Nakubali adhabu ya kisaikolojia ni nzuri, ila kumtayarisha mtoto kwa ulimwengu ambao kuna vitu vya kuogopeka ni muhimu.
Jambo la muhimu ni kumfundisha na kumueleza sababu ya adhabu, na kumpa alternatives ili asirudie tena ndio unamchapa.
 
Yeah beatings are not the best way of disciplining our kids.

Unaweza ukamuonya kama naimaomari anavyosema then the second time you deny your kid vile vitu anavyovipenda sana next time hata yeye atakuwa more serious.

Unapomchapa mtoto you inflict fear.

Uncle yangu mimi akitokaga kazini kama watoto wake wamekaa livingroom kila mtu anaenda bedroom.yeye akaanza kujishtukia kwamba he is all alone livingroom ikabidi siku moja akawaita watoto wake wakabonga fresh wakaelewana saa hivi nyumba nzima ni masela baba,mama na watoto.

Am not a parent ila parents should seat with their children and discuss issues probably sometimes wewe mzazi ndio causative agent wa mtoto wako misbehaving. Vilevile wazazi should watch out the things they tell watoto wao zinaweza kuwa very hurtful kama pale ambapo mzazi anamwita mtoto ng'ombe.Wewe kama mama ukiitwa mama ng'ombe au baba ng'ombe utafurahi coz wewe ndiye ulimwita mtoto ng'ombe.

Sometimes wazazi angalieni all sides na muepuke kuside na watoto wenu.
 
Hili limewa-cost wenzetu wa magharibi.....! (maana west ndo riferens) wanabaki kukanya kwa mdomo mitoto yenyewe haikanyiki kwa maneno matupu...!

Hilo linaleteleza mpaka binti anadiriki kutambulisha kwa wazazi rafiki yake mpya wa kiume na si yule aliyemtambulisha last week au yule mkiwa likizo....!

Ikaja kubwa yake kijana wa kiume anakutambulisha kwako mzazi HUSBAND TO BE WAKE.....!
huu ndo sisi tunaita mmomonyoko wa maadili, manake unaanzia kwenye kufata (vijihaki vya magharibi) human rights....!

Ila kwenye hiyo Human rights kuna vijinegative vingi vitakonavyo nayo na hili tunalojadili ni mojawapo...!
 
wakati sisi tuna JINSIA (SEX) mbili (male & female), wenzetu wana zaidi ya mbili (male, female, gay/lesbian)......!?!
WAKATI UNAJAZA FOMU UKAULIZWA SEX? SIJUI UTAJAZA IPI?
 
Binafsi ninaafiki uchapaji wa mtoto pale unapoona kosa aliloyafanya linastahili hiyo adhabu. Tatizo linakuja pale mzazi/mwalimu anapotumia adhibu hii kwa kisasi au kukomoa. In fact, adhabu yoyote ile (kuchapa, kufungia ndani, nk) inapofanywa kwa nia nyingine (kisasi, hasira, kukomoa, nk), zaidi ya kuadhibu kunakostaili, sio mzuri.

Haya mambo ya magharibi ya kutochapa watoto ndio yanasababisha u-pyscho kwenye jamii zao...
 
Sometime kustua kwa kucha ( kufinya) inahusika zaidi..maana unampakata mtoto kwenye paja na unampa panishment bila raia wengine kujua wanasikia dogo analia tu..na inauma mno...mimi huiita silence punishment.... Mzee wangu alikua ananipaga hiyo dozi nilipokua mtoto na nafikiri imenisaidia sana.......
 
I personally believe viboko viendelee but viwe limited kwa walimu tu, sio kama shule zetu za kata ambapo za msingi hadi kiranja anakuwa anasimamia na kiboko ukileta mchezo anakuchapa.

Kwa waliopitia shule za "mtakuja" mnaonaje?
 
Hii inatisha, yaanin unamaanisha kuna sehemu ambazo wanafunzi bado wanachapwa? Jaribu hapa kwetu, na utalala korokoroni. Hata hivyo, mtoto akichapwa inazidisha mambo mabaya. Ukitaka kumrudi mtoto, basi tumia ushauri nasaha na italipa zaidi ya viboko.
 
Hii inatisha, yaanin unamaanisha kuna sehemu ambazo wanafunzi bado wanachapwa? Jaribu hapa kwetu, na utalala korokoroni. Hata hivyo, mtoto akichapwa inazidisha mambo mabaya. Ukitaka kumrudi mtoto, basi tumia ushauri nasaha na italipa zaidi ya viboko.
wapi huko mkuu?
bongo aka TZ bakora kama kawaida mazee!, mitoto ya bongo haieleweki na bila bakora haiendi.
ila ndio kama alivyosema mchangiaji mmoja hapo juu, ziwe limited na pia nakumbuka sheria inasema kuna idadi maalum na mchapaji sijui ni mwalimu mkuu(kama nimekosea nisahihishwe), sio kila mwalimu atandike mikwaju tu aka stiki aka mbarati aka bakora!!
 
Wakuu kwa heshma na taadhima naomba mnijuze kuhusu adhabu ya viboko shuleni. Je adhabu hii ni kweli kuwa imekatazwa kisheria kwa wanafunzi wote kuanzia primary mpaka A level? kuna waraka au sheria inayo thibitisha hayo,

Tafadhali namiombeni msaada wenu wenye kuelewa jambo hili:angry:
 
Tangu Education Act ya 1978, inaruhusu walimu kutumia viboko (cane) kuwatandika wanafunzi wa kike mikononi na wa kiume makalio. Waraka unasimamia ni kwa namna gani adhabu itatolewa kwa wanafunzi upo. Waraka huo hata hivyo haukatazi kabisa adhabu ya viboko kutumika mashuleni ila unachofanya ni ku-regulate.


  1. Sheria ina mpa mamlaka Mkuu wa Shule au mwingine yeyote [mwalimu; hata mzazi/mlezi in other cases(tafsiri yangu ya mtu mwingine yeyote)] aliyepewa ruhusa na Mkuu wa Shule kutoa adhabu hiyo.
  2. Unaweka mipaka (limit) ya idadi ya viboko mwanafunzi anavyoweza kuchapwa (si zaidi ya 6 kama nakumbuka vizuri).
Sasa uwepo wa waraka unatoa maelekezo tofauti sina hakika kuhusu hilo.
 
Hodi hodi! NI mara yangu ya kwanza kuingia huku. Naomba uvumilivi! Adhabu ya viboko iwepo! Siyo ya kukomoana bali iwekewe utaratibu wa namna ya kuitoa. Mateke ngumi makofi hapana!
 
Kwa maoni yangu na kwa mujibu wa dini ambayo naiamini inasisitiza fimbo ndiyo inayoweza kumrkebisha mtoto kama akikosea. Fimbo itolewe kwa lengo la kumrudi mtoto na si kukomoa, pia fimbo ikitumika vibaya yaweza kumharibu mtoto. Kwa mujibu wa maandiko matakatifu (Mithali 23:13-14, imeandikwa, usimnyime mtoto wako mapigo maana ukimpiga kwa fimbo hatakufa, utampiga kwa fimbo na kumwokoa nafsi yake na kuzimu) pia katika (Mithali 13:24, imeandikwa Yeye asiyetumia fimbo yake humchukia mwanaye bali yeye ampendaye humrudi mapema),

Hapa ina maanisha kuwa hata walimu ni wazazi kama watamchapa mtoto kwa nia ya kumrekebisha kwa kufuata pia maadili ya ualimu. Kwa upande mwingine baadhi ya walimu hawana maadili na hivyo kutoa adhabu ya fimbo kwa kukomoa watoto. Wachungaji mbalimbali huko Marekani wengi wanailamu serikali yao kwa kuondoa adhabu ya fimbo ambayo kwa kiasi kikubwa imesababisha kushuka kwa nidhamu kwa kiza
zi kilichopo.
. Kuna mwandishi mmoja wa vitabu na mchungaji (Dr. Dale A. Robbins) katika moja ya majarida yake ameandika (It was a significant mistake to ever remove stick punishment from our public school system) Kwa hiyo hata huko marekani watumishi wa mungu na wazazi wenye mapenzi mema wanaona fimbo ni muhimu sana kwa kumrekebisha mtoto.
 
Back
Top Bottom