Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,463
- 113,532
Wanabodi,
Juzi Jumapili ilikuwa siku ya kupinga adhafu ya kifo duniani.
Nimesoma andishi hili la Prof. Chris Peter Maina wa UDSM, nikagundua kuwa licha ya Tanzania kuwa na adhabu ya kifo, Zanzibar adhabu hiyo haijawahi kutekelezwa hata mara moja tangu baada ya Mapinduzi yale matukufu ya Januari, 1964.
Huku bara, Nyerere alisaini hati 3 za adhabu ya kifo, Mwinyi alisaini hati 85 ila Mkapa na Kikwete hawajasaini hata hati moja!
Hii imenishawishi kuuliza tena, hivi kweli kwa Tanzania ya leo, bado tunaihitaji hii adhabu ya kifo, ambayo utekelezwaji wake kwa Tanzania ni very barbaric, kunyongwa mpaka kufa!.
Lengo la hukumu nyingi ni punitive na penitentiary, yaani kutoa adhabu na kufundisha, sasa mtu aliyeuwa, ukimhukumu kufa ndio unakuwa umemuadhibu vipi zaidi ya kumpotezea uhai wake, na kwa upande wa mafunzo, unakuwa umempa funzo gani ili ajirekebishe?.
Public execution ni adhabu ya kidhalimu iliyotumiwa kwa lengo la kutisha na kuogofya wengine wasifanye kosa kama hilo.
Marekani bado inatoa adhabu ya kifo, kasi ya vitendo vya mauaji iko juu kuliko nchi nyingine yoyote duniani, hivyo ni uthibitisho kuwa adhabu ya kifo haipunguzi makosa ya mauaji.
Uingereza imeifuta adhabu ya kifo, vitendo vya mauaji vimeshuka kwa kiasi kikubwa.
Kwa nchi za Afrika, Namibia imeifuta adhabu ya kifo na vitendo vya mauaji vimeshuka sana, lakini Afrika Kusini ambayo imeifuta adhabu hii ya kifo lakini vitendo vya mauaji bado viko juu maradufu.
Jee sisi Tanzania, tusimame wapi?, tuifute au tuendelee kuilea huku mamia wakihukumiwa bila kujua hatma yao ni lini hivyo wanaishi kwa kihoro huko magerezani. Kwa nini tusiifute tukajua moja?.
Juzi Jumapili ilikuwa siku ya kupinga adhafu ya kifo duniani.
Nimesoma andishi hili la Prof. Chris Peter Maina wa UDSM, nikagundua kuwa licha ya Tanzania kuwa na adhabu ya kifo, Zanzibar adhabu hiyo haijawahi kutekelezwa hata mara moja tangu baada ya Mapinduzi yale matukufu ya Januari, 1964.
Huku bara, Nyerere alisaini hati 3 za adhabu ya kifo, Mwinyi alisaini hati 85 ila Mkapa na Kikwete hawajasaini hata hati moja!
Hii imenishawishi kuuliza tena, hivi kweli kwa Tanzania ya leo, bado tunaihitaji hii adhabu ya kifo, ambayo utekelezwaji wake kwa Tanzania ni very barbaric, kunyongwa mpaka kufa!.
Lengo la hukumu nyingi ni punitive na penitentiary, yaani kutoa adhabu na kufundisha, sasa mtu aliyeuwa, ukimhukumu kufa ndio unakuwa umemuadhibu vipi zaidi ya kumpotezea uhai wake, na kwa upande wa mafunzo, unakuwa umempa funzo gani ili ajirekebishe?.
Public execution ni adhabu ya kidhalimu iliyotumiwa kwa lengo la kutisha na kuogofya wengine wasifanye kosa kama hilo.
Marekani bado inatoa adhabu ya kifo, kasi ya vitendo vya mauaji iko juu kuliko nchi nyingine yoyote duniani, hivyo ni uthibitisho kuwa adhabu ya kifo haipunguzi makosa ya mauaji.
Uingereza imeifuta adhabu ya kifo, vitendo vya mauaji vimeshuka kwa kiasi kikubwa.
Kwa nchi za Afrika, Namibia imeifuta adhabu ya kifo na vitendo vya mauaji vimeshuka sana, lakini Afrika Kusini ambayo imeifuta adhabu hii ya kifo lakini vitendo vya mauaji bado viko juu maradufu.
Jee sisi Tanzania, tusimame wapi?, tuifute au tuendelee kuilea huku mamia wakihukumiwa bila kujua hatma yao ni lini hivyo wanaishi kwa kihoro huko magerezani. Kwa nini tusiifute tukajua moja?.