Adha hii itaisha lini!

Katika hili ni vema kujua jamii hiyo ina viupa mbele vipi? Pengine hilo la kukaa chini sio kero kwao. Kwani sehemu nyingine wazazi na wafanyabiashara wamekuwa wakisaidiana na serikali zao za mitaa kuondoa tatizo la madawati.

Pengine BUK anaweza kutuambia kama jamaa wa Vingunguti wanaona ni kero kwa watoto wao kukaa chini madarasani. Au wana kero kubwa zaidi ya hiyo kama ya kukosekana kwa mfumo wa maji safi na maji taka, tatizo la takakata, tatizo la vyoo, tatizo la umeme, ujenzi holela n.k

Jamaa wa vingunguti wanatoa kodi kwa serikali. Kazi ya hiyo kodi ni nini kama sio pamoja na kutengeneza madawati?
 
Kodi ya aina gani wanayotoa? na aina gani ya wakaazi wa hapo ambao wanalipa kodi?

Kwa kuanzia tu,

1. Wanalipa kodi kwa manunuzi wanayofanya - bidhaa wanazonunua zinakuwa zina kodi ya ongezeko la thamani (VAT).

1 (b) Wakinunua vitu kariakoo au kwenye masoko, wananunua vyakula au bidhaa toka kwa wafanyabiashara ambao wanalipa kodi na ushuru kwa serikali na taasisi zinazohusika (local authorities?).

---- Bei ya bidhaa zao inajumuisha kodi hizi na hivyo kuwafanya hawa wakazi kuwa wabeba mzigo (tax burden) wa kodi hizi (na sio wafanyabiashara ambao wanazipitisha kodi hizi kwenda kwa wanunuzi).

2. Kuna wafanyakazi wa serikali na makampuni binafsi wanaoishi vingunguti ambao wanalipa PAYE (nadhani ndilo jina linalotumika) kwa serikali kuu.

3. Wanywaji wa pombe na wavuta sigara wa vingunguti wanalipa kodi au ushuru maalumu kwa serikali (ambao ni part ya bei ya bia na sigara).

4. wasafiri na waendesha magari binafsi wanalipia kodi maalumu inayowekwa kwenye mafuta kila mwaka.

5. itaendelea
 
Kwani wewe shule ya msingi ulisoma wapi? Olympio? na je wewe ni mtanzania kweli ambaye hujui hii?

Hili tatizo ni sugu liko miaka kibao zaidi hata ya ishirini sehemu nyingine hii ndio kawaida kama sheria.

Kwa wale waliosoma shule za msingi TZ nadhani mmelizoea na mmetoa michaango ya madawati mara kibao halafu unashangaa linaletwa dawati moja au mawili kuwazuga.

That was a Socratic question as i understood it, not a literal one.

Wa kushangaza ni yule aliyeulizwa, aliyesema adha hii imeanza baada ya watu wa mikoani kuja Dar. tangu zamani madawati ni issue, sema waliosoma shule za kishua walikuwa wanafanya charity walk, wanatembea na forms kwa wadosi, wengine wanajulikana famila zao Lions Club, Rotary Club na Gymkhana Club wanasawazisha mambo. Huko Vingunguti wamesota sana tu tyangu zamani kabla hata ya massive influx ya wakuja kutoka the hinterland huko, wala msitake kuwasingizia wao.

Nimeomba gharama za dawati moja hapa, mpaka sasa tumeshindwa kuchangia hata kupiga mahesabu nako tushindwe?
 
Kwa kuanzia tu,

1. Wanalipa kodi kwa manunuzi wanayofanya - bidhaa wanazonunua zinakuwa zina kodi ya ongezeko la thamani (VAT).

1 (b) Wakinunua vitu kariakoo au kwenye masoko, wananunua vyakula au bidhaa toka kwa wafanyabiashara ambao wanalipa kodi na ushuru kwa serikali na taasisi zinazohusika (local authorities?).

---- Bei ya bidhaa zao inajumuisha kodi hizi na hivyo kuwafanya hawa wakazi kuwa wabeba mzigo (tax burden) wa kodi hizi (na sio wafanyabiashara ambao wanazipitisha kodi hizi kwenda kwa wanunuzi).

2. Kuna wafanyakazi wa serikali na makampuni binafsi wanaoishi vingunguti ambao wanalipa PAYE (nadhani ndilo jina linalotumika) kwa serikali kuu.

3. Wanywaji wa pombe na wavuta sigara wa vingunguti wanalipa kodi au ushuru maalumu kwa serikali (ambao ni part ya bei ya bia na sigara).

4. wasafiri na waendesha magari binafsi wanalipia kodi maalumu inayowekwa kwenye mafuta kila mwaka.

5. itaendelea

Solomon unabishana na mtu ambaye elimu yake niyamsingi atajua maana ya mlipa kodi?
 
Ujinga mtupu! VaT, kodi ya Sigareti kamwe sio kodi ya kutegemea kuchonga madawati..!

Kibunango,

are you serious?

Ni kodi gani inatumika kwenye madawati? Kazi ya VAT na hivyo vingine kazi yake ni nini? Je ile kodi wanayotozwa wafanyabiashara kwenye masoko ya mitaani (kama lile la mbuzi pale vingunguti) kazi yake ni ipi?
 
Wa kushangaza ni yule aliyeulizwa, aliyesema adha hii imeanza baada ya watu wa mikoani kuja Dar. tangu zamani madawati ni issue, sema waliosoma shule za kishua walikuwa wanafanya charity walk, wanatembea na forms kwa wadosi, wengine wanajulikana famila zao Lions Club, Rotary Club na Gymkhana Club wanasawazisha mambo. Huko Vingunguti wamesota sana tu tyangu zamani kabla hata ya massive influx ya wakuja kutoka the hinterland huko, wala msitake kuwasingizia wao.
Unazungumzia Bongo ya 70 and 80's, ambapo idadi ya wabongo hapo Bongo ilikuwa less ya milioni...
 
Mie naona yote sawa tu. Acha wakae. Sidhani kama baba na mama zao wanajali sana matatizo ya watoto wao. Uchaguzi ukija, wanavuta T-shirt na kuchagua viongozi ambao watawaweka watoto wao chini.

Yes, narudia tena "WACHA WAKAE saaana tu hadi waote hapo ardhini."

Ningelikuwa mgombea wa Urais ningeliwaambia hivyo hivyo. Wakitema wakimeza shauri yao.
 
Hapa tuache kulaumu serikali tu. Hili ni tatizo la jamii nzima. Sasa cha kujiuliza jamii inafanya nini? Kwa nini watu hatu step up to the plate kubadilisha hizi hali? Kwani wazazi wa watoto hao na watu wengine wapenda maendeleo wakikusanya nguvu zao watashindwa kweli kuchongesha madawati au kununua viti vya kukalia hao watoto?

I'm tired of people boohooing govt this govt that....why don't we all step up as a community?

Si ujajua mijitu isivyotaka kuwajibika. Angalia watoto wote walivyo sopusopu. Na hakuna mtoto anayekaa au kulala chini nyumbani kwao. Na wengine wanakwenda shule na cell-phones.
 
Tatizo litamalizwa kwa kuondoa gharama ya workshop moja au seminar moja katika wizara ya elimu..finito..moja tu watoto wote wanakuwa na viti!
Nimewahesabu hawazidi 100 X 50,000 = Tsh.5,000,000/=
 
Tatizo litamalizwa kwa kuondoa gharama ya workshop moja au seminar moja katika wizara ya elimu..finito..moja tu watoto wote wanakuwa na viti!
Nimewahesabu hawazidi 100 X 50,000 = Tsh.5,000,000/=

So dawati moja ni Tsh.5,000,000 ?
 
So dawati moja ni Tsh.5,000,000 ?
Dawati moja ni Tsh. 50,000/= hao watoto wako 100 ukizidisha unapata kama 5Mil. hivi?? watoto wanakaa wote hao...harusi moja budget yake the minimum ambazo nimehudhuria ni Tsh. 10Mil.
 
OK,

Tunaweza kuacha longolongo na kuanza ku- arrange msaada hapa, if only kuonyesha that we can and set an example?

Kama tunataka na tuna moyo hatuwezi kushindwa kupata some $ 5,000 , US.

Less than 40 ppl can take care of this.

1 @ $ 1000
2 @ $ 500
4 @ $ 250
10 @ $ 100
20 @ $ 50

More than Tsh 5,000,000, mnapata mpaka na hela ya visoda viwili vitatu vya kunywa siku ya makabidhiano, lol.

Kutoa ni moyo, usambe utajiri.
 
Back
Top Bottom