Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Adam alihojiwa wiki kadhaa kuhusu tuhuma za rushwa ilikuwa kwenye mojawapo ya vikao vya kujiuza pale jijini Dar; alikanusha na kusema hayo ni maneno ya kisiasa tu na kuwa hakuna wakati ambapo kuna kampeni kama hizi ambapo watu hawatodai kuna rushwa. Lakini siku zilivyokwenda hadi jana jina lake limekuwa likitajwa pembeni kuwa alitumia fedha nyingi!
Watu wanapozungumzia "rushwa" wakati mwingine watu wanasahau kuwa hata baadhi ya viongozi wa mashirika ya umma na taasisi mbalimbali huwa wamekuwa wakitoa kitu kidogo (si lazima iwe fedha tu, bali pia nafasi, n.k) kwa wabunge ili wazungumze vizuri. Hii ni pamoja na kupeleka miradi kwenye majimbo yao au kuwapa 'shukrani fulani'. Rushwa hizo za kitaasisi mara nyingi hazisikiki sana kwa sababu hazihusiani moja kwa moja na kampeni za kisiasa lakini pia zipo na watoa rushwa wakubwa wa kitaasisi wanajulikana au bora zaidi wanapaswa kujulikana kwani hawana siri!
Lakini la Kimbisa inaonekana kama vile ni "common knowledge" lakini hakuna mtu ambaye ameweza kusema kwa uhakika alimuona Kimbisa akitoa rushwa wapi na akimpa nani! Isije kuwa ni yale yale ambayo mtu mmoja alianzisha rumors kuwa "kimbisa katoa rushwa" na kutoka hapo kila mtu amekuwa akirudia hilo. Kama ni kweli ina maan kuna wabunge kama 210 ambao ni wala rushwa!! yaani 2/3 ya Bunge ni wala rushwa!!!! Hilo linatisha!!
Lakini kama siyo yeye ni kina nani hawa ambao wanadaiwa kutoa rushwa na wamempa nani....
Kama ulitoa rushwa kwenye kampeni ya EALA, kupokea au kumuona mtu akitoa na kupokea na unauhakika kuwa ilikuwa ni rushwa siyo mtu alikuwa "analipa deni fulani!"
Watu wanapozungumzia "rushwa" wakati mwingine watu wanasahau kuwa hata baadhi ya viongozi wa mashirika ya umma na taasisi mbalimbali huwa wamekuwa wakitoa kitu kidogo (si lazima iwe fedha tu, bali pia nafasi, n.k) kwa wabunge ili wazungumze vizuri. Hii ni pamoja na kupeleka miradi kwenye majimbo yao au kuwapa 'shukrani fulani'. Rushwa hizo za kitaasisi mara nyingi hazisikiki sana kwa sababu hazihusiani moja kwa moja na kampeni za kisiasa lakini pia zipo na watoa rushwa wakubwa wa kitaasisi wanajulikana au bora zaidi wanapaswa kujulikana kwani hawana siri!
Lakini la Kimbisa inaonekana kama vile ni "common knowledge" lakini hakuna mtu ambaye ameweza kusema kwa uhakika alimuona Kimbisa akitoa rushwa wapi na akimpa nani! Isije kuwa ni yale yale ambayo mtu mmoja alianzisha rumors kuwa "kimbisa katoa rushwa" na kutoka hapo kila mtu amekuwa akirudia hilo. Kama ni kweli ina maan kuna wabunge kama 210 ambao ni wala rushwa!! yaani 2/3 ya Bunge ni wala rushwa!!!! Hilo linatisha!!
Lakini kama siyo yeye ni kina nani hawa ambao wanadaiwa kutoa rushwa na wamempa nani....
Kama ulitoa rushwa kwenye kampeni ya EALA, kupokea au kumuona mtu akitoa na kupokea na unauhakika kuwa ilikuwa ni rushwa siyo mtu alikuwa "analipa deni fulani!"