Fidel80
JF-Expert Member
- May 3, 2008
- 21,947
- 4,444
POLISI mkoani Morogoro, wanamshikilia mwanamke mmoja wa Kijiji cha Mambegwa, Msowelo wilayani Kilosa, kwa tuhuma za kumuua mume kwa kumvuta sehemu za siri.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana, Kamanda wa Polisi mkoani humu, Thobias Andengenye, alisema tukio hilo lilitokea usiku wa Agosti 17 mwaka huu, katika kijiji cha Mambegwa.
Kamanda huyo alimtaja mwanaume aliyeuawa kuwa ni, Masanja Kakoro (40) na kwamba kuuawa kwake, kunafuatia ugomvi uliozuka wakati wakiwa wamelala.
Kamanda huyo alisema hata hivyo chanzo cha ugomvi huo, hakijafahamika na kwamba mtuhumiwa anahojiwa zaidi na polisi na kabla ya kumfikisha mahakamani.
Source;http://www.mwananchi.co.tz/newsrids.asp?id=14025
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana, Kamanda wa Polisi mkoani humu, Thobias Andengenye, alisema tukio hilo lilitokea usiku wa Agosti 17 mwaka huu, katika kijiji cha Mambegwa.
Kamanda huyo alimtaja mwanaume aliyeuawa kuwa ni, Masanja Kakoro (40) na kwamba kuuawa kwake, kunafuatia ugomvi uliozuka wakati wakiwa wamelala.
Kamanda huyo alisema hata hivyo chanzo cha ugomvi huo, hakijafahamika na kwamba mtuhumiwa anahojiwa zaidi na polisi na kabla ya kumfikisha mahakamani.
Source;http://www.mwananchi.co.tz/newsrids.asp?id=14025