Gang Chomba
JF-Expert Member
- Feb 29, 2008
- 20,301
- 4,681
jina kamili: Associazione Calcio Milan.
a.k.a: Rossoneli ''red & black'', Diavolo ''the Devil''.
Kuanzishwa: 16/dec/1899.
Uwanja: Sansiro Meazza.
Uwezo: unabeba watu 80,074...
President: Paolo Scaloni.
Kocha: Stefano Pioli.
Nahodha; David Calabria.
Daktari: Mauro Gevi.
Ac Milan ni klabu kubwa na yenye mafanikio ya kimataifa zaidi ya timu yoyote ile hapa Duniani.
AC Milan ilianzishwa na waingereza wawili Alfred Edward na Albert kilpin ktk mwaka huo wa 1899 ambapo makao makuu ya klabu yalikuwa Fiaschetteria Toscana ktk Barabara ya Beschet hapahapa Milan
Mpaka sasa Milan ndio klabu inayoongoza kwa mafanikio ya kimataifa ikiwa imekusanya
Intercontinental cup mara 4
European super cups mara 5
Cup winner cup mara 2
UEFA champions league mara 7.
Pia Milan imebeba ndoo 18 za ligi kuu ya Italia maarufu kama Scudeto.
for more info visit www.acmilan.com
....................................................................
Hah hah ha hah ahaaah dah nianze kwa kicheko kilichojaa dharau na kebehi kisha nashushia na Bia aina ya Peroni inayopatikana kila Bar au Night Club au sehemu yoyote ya anasa katika jiji la Milan.
kikubwa kinachonichekesha ni kitendo cha makusudi cha washabiki wa soka wa siku hizi kujitia uzezeta na kutoa maneno ya kipumbavu ambayo kwa siku za karibuni wamezidi kuambukizana hivyo matapishi hayo wanayoongea yanatapakaa kila kona.
mwanzo niliposikia nikasema labda niliemsikia alitoka chooni bila kuchamba, lakini kwa sasa mambo ni tofauti.
soka lina misingi yake, soka lina sheria zake, lakini soka lina kitu kimoja muhimu mno ambacho hicho ndio kinaleta ladha halisi, kitu kicho ni historia.
unapozungumzia Historia ya Soka kwa ngazi za vilabu basi hutaacha kuitaja klabu yenye mafanikio zaidi hapa ulimwenguni, hapa naizungumzia AC Milan, ambayo pia ndio klabu iliochezewa na nyota wengi zaidi kuliko klabu yoyote mpaka sasa.
basi wakati nafungua Peroni ya 4 huku nikivuta shisha nikawa navuta kumbukumbu huku natafakari kauli kauli za wakurupukaji hawa wanaodai eti AC Milan ni katimu kadoogo sana, tena huwa wanakwenda mbali zaidi kwa kusema eti katimu haka hakana lolote.
ukiwauliza vilaza hawa watakwambia kwao timu bora ni Barcelona, Manchester, Madrid, Chelsea eti na hata Arsenal nayo imo sasa wakati nilipokuwa na Peroni ya 9 huku moshi wa Fleva ya Minti ukiingia mpaka kwenye Bandama na kupanda hadi kwenye mishipa midogo inayoingia ndani ya Ubongo nikarejea tukio la kusisimua na kuchekesha ndani yake.
nilikumbuka tukio la tarehe 19/04/1989 mwendo wa saa mbili na na nusu usiku, katika usiku huu usiosahaulika na Los blancos ulikuwa ni wa mechi ya nusu fainali ya marudiano ya AC Milan dhidi ya Real Madrid, ikumbukwe ktk mechi ya kwanza iliofanyika katika dimba la El Santiago Bernabeu, Madrid walilazimisha suluhu ya goli 1-1.
na ktk mechi iliofuata sasa na kushuhudiwa na washabiki 73112 waliofurika Sansiro, Real Madrid walicharazwa goli 5-0 huku magoli ya Milan yakifungwa na Carlo Ancelotti, Frank Rijkaard, Ruud Gulitt, Marco Van Basten na Roberto Donadoni na hatimae Milan kutinga fainali.
kama hio haitoshi May/24/1989 milango ya saa mbili na robo usiku ktk dimba la Camp Nou ambapo mashuhuda wapatao 97,000 walishuhudia Milan wakiifunga Steau Bucharesti kwa jumla ya magoli 4-0 magoli yaliowekwa kimiani na Ruud Gullit aliefunga 2 na Marco Van Basten alietupia goli mbili pia na kuchukua tuzo ya mfungaji bora akiwa na jumla ya magoli 10.
eti watu wanajisahaulisha hayo pamoja na kujitoa akili kabisaa na kuishi bila kukumbuka kuwa hata msimu uliofuata baada ya hapo ilikuwa ni AC Milan pia iliobeba ndoo hio na rekodi hio hakuna alieweka mpaka sasa.
hivi leo hii nani hajui kuwa Milan ilitengeneza timu bora ambayo haitakuja kutokea ktk historia ya Soka?
hivi ni strikers gani wangeweza kupita beki imara ilioongozwa na Franco Baresi huku akisaidiwa na Alesandro Billy Costacurta, Paolo Maldini na Mauro Tasotti?
hivi ni nani alietimamu ambae anaweza kusahau kipigo cha Mbwa koko ndani ya uzio walichokipata Barcelona iliowahi kuwa bora kuliko Barcelona yoyote ile katika mechi ya fainali ya ligi hiohio ya mabingwa mwaka 1994?
kama mnajisaulisha well naomba kesho muanze kuvaa suruali kisha juu mvae chupi. ila mimi nawakumbusha kuwa Milan waliwasasambua Barca jumla ya goli 4-0 goli zilizopachikwa na Savicevic, Daniele Masaro, Roberto Donadoni na mkoba Marcel Desailly ktk mechi iliopigwa tarehe 18/04/1994 ktk dimba la Olimpico hapo Athens jumla ya watazamaji 70000 walishuhudia Pep Guardiola na Romalio wakishindwa kugusa mpira takriban dakika 30 za mwisho.
cha kuchekesha zaidi Milan walicheza bila top striker Van basten wala nahodha Franco Baresi na bila mchezaji ghali duniani kwa wakati huo yaani Gianluigi Lentini...hivi ni kipi Milan wafanye ili muwashimu?
je mlikuwa wadogo kipindi George Wear anatwaa tuzo ya mwanasoka bora wa Dunia, Ulaya na Africa? je hamkumbuki alikuwa striker wa timu gani?
hivi kweli mnajisahaulisha ukuta bora kwa karne hii umeundwa na Dida, Cafu, Maldini, Stam na Nesta?
niwaweke kundi gani kama mnashindwa kuheshimu triple R toka Brazil yaani Rivaldo, Ronaldo na Ronaldinho kuwa wote walicheza Milan?
sawa Seedorf, Rui Costa, Boban na Pirlo hamuwaheshimu, basi hata Redondo?
eti mtu alieitwa Super pipo hamumtambui, je Mtakatifu Baggio nae? au mnataka Mbwana Samatta acheze Milan ndio muiheshimu?
Bayern walishapigwa goli 4 Sansiro wakaonekana hawajui, je nani asiekumbuka kuwa washabiki wa Man UTD waligoma kurudia kuangalia kipindi cha pili baada ya wachezaji wao kuusaka mpira takriban dakika 45 za mwanzo huku Gatusso akibweka na kumficha Christiano?
[/QUOTE]
TO BE CONTINUA...