Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,299
- 33,082
ABIRIA zaidi ya 60 waliokuwa wakisafiri katika basi la abiria linalotambulika kwa jina la Harambee Bus linalofanya safari zake kati ya Dar Arusha walinusurika kufa baada ya basi hilo kupinduka huko Msata Wilayani Bagamoyo Tukio hilo lilitokea jana ambapo basi la abiria lililokuwa na namba za usajili T362 AFN na lori lililokuwa na namba za usajili T714 ALM kutaka kuvaana na kupelekea basi hilo kupinduka wakati likijaribu kukwepa lori hilo.
Eneo lililotokea ajali hiyo Msata kuna kona kali ambapo lori hilo lilikuwa likitokea Arusha kuja jijini Dar es Salaam.
Lori hilo bila kuonyesha ishara yoyote kama linataka kuingia kwenye kituo cha mafuta lilikata kona kuingia kituoni hapo na kusababisha dereva wa basi ambaye alikuwa anaendelea kunyoosha barabara bila kutambua kuwa lori hilo litaingia kituoni hapo kuwa katika wakati mgumu wa kulikwepa lori hilo.
Katika jitihada za kuokoa maisha ya watu hao na kukwepa wasivaane na lori hilo basi hilo lilipinduka pembezoni mwa barabara.
Hata hivyo katika tukio hilo hakuna abiria aliyepoteza maisha bali kulipatikana na majeruhi kadhaa ambapo walikimbizwa katika hospitali ya Msata Wilayani Bagamoyo kwa matibabu.
nifahamishe.com
Eneo lililotokea ajali hiyo Msata kuna kona kali ambapo lori hilo lilikuwa likitokea Arusha kuja jijini Dar es Salaam.
Lori hilo bila kuonyesha ishara yoyote kama linataka kuingia kwenye kituo cha mafuta lilikata kona kuingia kituoni hapo na kusababisha dereva wa basi ambaye alikuwa anaendelea kunyoosha barabara bila kutambua kuwa lori hilo litaingia kituoni hapo kuwa katika wakati mgumu wa kulikwepa lori hilo.
Katika jitihada za kuokoa maisha ya watu hao na kukwepa wasivaane na lori hilo basi hilo lilipinduka pembezoni mwa barabara.
Hata hivyo katika tukio hilo hakuna abiria aliyepoteza maisha bali kulipatikana na majeruhi kadhaa ambapo walikimbizwa katika hospitali ya Msata Wilayani Bagamoyo kwa matibabu.
nifahamishe.com
Last edited by a moderator: