Andre02150
JF-Expert Member
- Feb 2, 2010
- 332
- 128
Siku za hivi karibuni nilisafiri kwenda Mwanza na Bukoba kwa kutumia bus. Wasafiri tulipatwa na adha nyingi njiani ukianzia kusimamishwa bila mpango na maaskari usalama barabarani, mizani, na mbaya zaidi - pengine kuliko zote ni sheria ya kuyataka mabasi yaingie kwenye Stendi za kila Wilaya! Sielewi TABOA, SUMATRA na Wananchi kwa ujumla walikuwa/tulikuwa wapi kutafafuta njia mbadala ya kuwezesha Halmashauri kukusanya mapato bila kutubugudhi cc wasafiri.
Kero nyingine ambayo kusema ukweli wadau inawabidi waitupie macho ni sheria ya kuzuia mabasi ya abiria kusafiri ifikapo saa nne usiku, na mikoa mingine ifikapo saa 5 usiku (sasa cjui hii discrepancy inatoka wapi!). Inawezekanaje bus linatoka mkoani kuja jijini Dar, kisha likifika Morogoro saa nne usiku linazuiliwa kutembea masaa mawili yaliyobakia? Au bus linasafiri kutoka Dar na kisha likifika Kahama saa tatu usiku linazuiliwa kuendelea na safari kisa kuna maharamia njiani!! Yaani kweli cc Watanzania, na Viongozi wetu wa serikali tumekubali kuwa terrorized na maharamia kiasi kwamba hatuwezi kusafiri hadi kukesha!!
Binafsi nafikiri viongozi wabuni mikakati ya kuondoa karaha kwa wasafiri tunaosafiri safari hizi ndefu badala ya kutuongezea sheria zilizojaa adha (au zenye kulinda maslahi ya watu wachache) na pengine sasa wakati muafaka umewadia wa ku-revise Sheria ya Usalama barabarani na ikibidi wa-institute Public Safety Act?! Duniani kote, usafiri wa uhakika na salama ni usiku. Ni hapa Tanzania peke yake ambako kusafiri usiku inaonekana hatari...ni imani yangu kwamba ukiwekwa utaratibu makini, tena utaratibu shirikishi mabasi yatasafiri safe usiku.
Kero nyingine ambayo kusema ukweli wadau inawabidi waitupie macho ni sheria ya kuzuia mabasi ya abiria kusafiri ifikapo saa nne usiku, na mikoa mingine ifikapo saa 5 usiku (sasa cjui hii discrepancy inatoka wapi!). Inawezekanaje bus linatoka mkoani kuja jijini Dar, kisha likifika Morogoro saa nne usiku linazuiliwa kutembea masaa mawili yaliyobakia? Au bus linasafiri kutoka Dar na kisha likifika Kahama saa tatu usiku linazuiliwa kuendelea na safari kisa kuna maharamia njiani!! Yaani kweli cc Watanzania, na Viongozi wetu wa serikali tumekubali kuwa terrorized na maharamia kiasi kwamba hatuwezi kusafiri hadi kukesha!!
Binafsi nafikiri viongozi wabuni mikakati ya kuondoa karaha kwa wasafiri tunaosafiri safari hizi ndefu badala ya kutuongezea sheria zilizojaa adha (au zenye kulinda maslahi ya watu wachache) na pengine sasa wakati muafaka umewadia wa ku-revise Sheria ya Usalama barabarani na ikibidi wa-institute Public Safety Act?! Duniani kote, usafiri wa uhakika na salama ni usiku. Ni hapa Tanzania peke yake ambako kusafiri usiku inaonekana hatari...ni imani yangu kwamba ukiwekwa utaratibu makini, tena utaratibu shirikishi mabasi yatasafiri safe usiku.