Mgogoro CUF: Abdul Kambaya awashambulia CHADEMA, JamiiForums

barafu

JF-Expert Member
Apr 28, 2013
6,726
32,818
image.jpeg
image.jpeg

Akiongea na Azam Two...Abdul Kambaya anasema sio kweli kuwa Prof Lipumba amewafukuza Katibu Mkuu na baadhi ya viongozi wa CUF.

Kambaya anasema kuwa kwa sasa Lipumba bado anasuka uongozi wake na leo alikutana na walinzi wa Chama Makao Makuu ya CUF ili kuona ni namna gani wanaimarisha ulinzi wa chama na viongozi waliorudishwa na msajili na pia kuhakikisha ulinziMakao Makuu ya Chama.

Abdul Kambaya anasema amekuja Azam Tv kukanusha habari hizo ambazo zimeanzia JAMII FORUM, huku akisema JF ni mtandao unaoongozwa na member wengi wa CHADEMA ambao nyuma ya mgogoro huu wa CUF wao wanafaidika.

Akihojiwa na Raymond Nyamwihula kama Prof Lipumba ataweza kufanya kazi na waliotofautiana naye? Kambaya anasema hilo linabaki kuwa suala la Lipumba mwenyewe, japo anakiri kuwa ni ngumu kuweza kufanya nao kazi pamoja kwani anaweza kuhitaji team mpya ya kukisuka chama kwa mikakati mipya

Kambaya anasema JF ndio inaeneza habari nyingi za CUF zisizo na ukweli na anasema kwa sasa mgogoro wa CUF umekuwa deal na biashara kwa vyombo vya habari vingi, akitolea mfano kuwa magazeti mengi ya leo yameandika kuwa "Prof Lipumba aingizwa makao makuu kwa Mtutu wa Bunduki". Kambaya anasema kuwa na si kweli kuwa Prof Lipumba anadhaminiwa na CCM.

Kuhusu kumuondoa Maalim Seif ktk nafasi yake,Kambaya anasema kwa sasa Lipumba ana mamlka ya kuwaondoa manaibu katibu mkuu wote isipokuwa Katibu Mkuu anayepatikana kwa mkutano kwa kuchaguliwa na mkutano Mkuu. Hivyo wao kama Wanachama wenye haki na walio madarakani kwa mujibu wa katiba,kesho wataenda kusikiliza walichoitiwa ktk Baraza la CUF makao Makuu ili wakajieleze na haki itendeke.

My Take:
Hii ya Abdul Kambaya kuhusisha JF na CHADEMA imekaaje? Ni kweli kuwa mpaka leo Kambaya anaamini JF ninaongozwa na member wengi wa CHADEMA?
 
Hii ni mission iliosukwa na wasioitakia mema UKAWA kwa lengo la kuisambaratisha.

Ni hivi, kwa mtazamo wangu,baada ya kuivuruga CUF, tusishange zikaanza kuenezwa propaganda kuwa CHADEMA ndio wanaohusika na mgogoro wa CUF kwa lengo la kuisambaratisha CUF ili CHADEMA kibaki kuwa chama pekee cha upinzani nchini.

Kingine nachokiana hapa ni kutaka kutumia mgogoro huu kuvunja ushirikiano wa CHADEMA na CUF ulioko Bungeni na pia umoja wa vyama hivi katika ngazi zaa Halmashauri ili ikiwezekana wasiwe kitu kimoja kwenye uchaguzi wa Umeya jijini Dar-es-salaam.

Huu ni mtazamo wangu na umekuwa kichwani mwangu mara baada ya vurumai hizi kuanza na hivi ndivyo ninavyoamini mpka sasa.
 
Barua ya msajili ni - ushauri na maoni yake. KATIBA NA SHERIA YA CHAMA HAIWEZI KUINGILIWA NA MSAJILI.

Magdalena Sakaya alimuomba Mh. Ndugai aingilie suala hili kama spika wabunge na akatoa maoni yake ambayo hayakukubalika. Kila chama kina sheria zake wala haziingiliani na vyama vengine.

Abdul Kambaya na wenzake wamesimamishwa mpaka hapo watakapo fika kujieleza kwenye kamati kuu. Sasa kuna kosa gani?. siku zenu zikifika mutakwenda kujieleza.

Lakini kwa hali hii, mumewakosea wananchi wenye akili timamu kwa kuwafanya ni wajinga wasio fahamu kitu.

Kwa hali hii mumewatukana na kuwadharau viongozi wa chama ambao ndio nguzo ya chama hiki. Kama alivosema Pof; Lipumba,- CUF ni taasisi kubwa haitingishwi na mtu mmoja au watu kikundi. CUF ina katiba yake na mihimili yake.

Sasa hii tabia ya kuvamia Buguruni na kuharibu mali ya chama itawasaidia nini. Kesi inayokuja jitayarisheni vizuri maana Segerea bado kuna nafasi.
 
Siamini kama barua ya Ushauri wa masajili wa vyama vya siasa inaweza kukulevya kiasi cha kufikia kuanza kuwatukana na kuwakejeli vijana wenzio mitandaoni.

Hivi barua ya msajili wa vyama inaweza kukupa kiburi kuungana na wanaCCM kutokuutambua ushindi wa maalim Seif kule Zanzibar? Kweli? Hivi unafunguka kutoa siri zote za Chama ambacho unalilia kuendelea nacho sasa kweli? Wewe ni mwanaCUF kweli?

Kumbe watu walioikwamisha CUF kusonga mbele siku zote ndio mnaanza kujitangaza umma uwatambue, si bora ungekaa kimya tu brother? Hivi ukiangalia na kufikiria kwa makini wewe na hawa unaowalaumu ni nani mwenye possibility ya kuondoka na kusahaulika CUF?

Kwanini usitambue kua Prof Lipumba hata kama akikalia kiti cha uenyekiti kwa sasa hana mamlaka kikatiba yeye kama yeye kumtimua kiongozi yeyote? Huoni kinachompa kichwa Sasa Lipumba ni angle ndogo tu ya barua yake ya kujiuzulu kutosainiwa na uongozi wa chama kumkubalia kua alijiuzulu? Kwani Lipumba amilitumuliwa uanachama na kamati kuu kwa sababu gani? Huoni kua bado kamati ya Mtatiro inayo mamlaka ya kumkataa Prof Lipumba kwa sababu ya Utovu wa nidhamu?

Kama wabunge wote wa CUF ispokua wawili tu hawamtaki hata kumsikia Lipumba, Sasa yeye anataka aendeshe Chama na nani? CUF yake itakua CUF ya namna gani?

Kwa tabia hizi kweli Msomi kama Maalim Seif angekubalije kufanya kazi na ninyi? Alishawashtukua ndio maana mlikua mnadai kua anawatenga hawashirikishi kwenye maamuzi.
 
Back
Top Bottom